Waziri George Simbachawene: Waliowashambulia wapenzi wakiwa faragha kwa madai ya kuwafumania wakamatwe

Nyendo

JF-Expert Member
Jun 4, 2017
1,194
4,112

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Geoge Simbachawene ameliagiza Jeshi la Polisi kuwakamata watuhumiwa waliowashambulia wapenzi wakiwa kwenye faragha wakidai kuwa wamewafumania.

Ametoa agizo hilo leo Agosti 6, 2021 jijini Dar es Salaama baada ya kuiona video iliyosambaa katika mitandao ya kijamii ikionyesha kundi la watu wakiwavamia wapenzi hao na kuwadhalilisha.
 
.

IMG_20210806_175228.jpg
 
Waziri wa Mambo ya Ndani George Simbachawene amekea tabia ya watu kukusanyana na kuvamia watu walioko kwenye faragha kwa kisingizio cha fumanizi akisema kufanya hivyo ni kinyume cha sheria na utu na watakamatwa wakigundilika.

Simbachawene ametoa kauli hiyo leo Ijumaa Agosti 6,2021 ambapo amesema baadhi ya watu wamejingea mazoea ya kuwavamia watu wenye uhusiano ya kimapenzi wakiwa kwenye faragha zao mahali wanapokuwa katika nyumba au hotelini.

“Tabia hii imeshamiri sasa kama ambavyo video nyingi zinarushwa rushwa mitandaoni, leo nitumie fursa hii kutoa msingi wa kisheria lakini kukemea tabia hii ambayo imeanza kuonekana inaota mizizi. Ni kinyume cha sheria kabisa kuwaingilia watu walio kwenye faragha,” alisema

“Wakati mwingine watu wanafanya hivyo kwa kisingizo kuwa wamefumania, hakuna fumanizi ambalo linaweza kupangwa na kikundi cha watu, wanawake na wanaume wanapanga kwenda kuwavamia na kuwaingilia uhuru wao waliopo faraghani, kitendo hicho ni kinyume cha sheria ,”

Amesema hata kama ni fumanizi litakuwa pale ambapo si jambo la kupangwa na huyo anayefumania awe na ndoa halali na cheti halali cha ndoa lakini sio kwa mtu ambaye ulikuwa naye tu “Huwezi kusema umemfumania hawala yako, mahusiano ya hawala ni ya kupita”.

Amesema tabia hiyo inakiuka misingi ya utawala bora, heshima na utu na hasa heshima ya wanawake kwakuwa wanaodhalilishwa sana katika hilo ni kina mama ambao walishakuwa na uhusiano na mwanaume fulani wakaachana akawa na mwingine halafu yule wa mwanzo anamfumania.

“Suala la kudhalilisha watu wako uchi wa mnyama na wanapata kipigo hilo haliwezi kukubalika katika nchi yetu, kwa nafasi yangu nachukua nafasi hii kuliagiza jeshi la polisi wahakikishe wanafuatilia matukio haya hususani hili linalozunguka kuanzia jana, wahakikishe wale wote waliohusika wanakamatwa,” amesema Simbachawene.

Chanzo: Mwananchi online.

Tuongee kikubwa, kumbe sheria ya faragha inaruhusu hadi kunyandua mbususu za wake za watu?
 
Waziri wa mambo ya ndani ya nchi ndugu Gorgeous simbachawene amewanya wale wanaokusanyika ama kuandaa mafumanizi kuwa Hilo ni Jambo lililo kinyume Cha sheria hivyo ukifanya hivyo utakamatwa .

Amedai watu waachwe maana hizo ni faragha zao,.

Chanzo:
mwananchi online.

Tuongee kikubwa ,kumbe sheria ya faragha inaruhusu hadi kunyandua mbususu za wake za watu??
Hili neno Mbususu nalikubali sana yani linaifunika neno papuchi vibaya sana. Halafu hizi mada zenye mrengo wa tasnia ya ngono ziko poa sana na zinasisimua. Mleta mada big up mwanangu.
 
Waziri wa mambo ya ndani ya nchi ndugu Gorgeous simbachawene amewanya wale wanaokusanyika ama kuandaa mafumanizi kuwa Hilo ni Jambo lililo kinyume Cha sheria hivyo ukifanya hivyo utakamatwa .

Amedai watu waachwe maana hizo ni faragha zao,.

Chanzo:
mwananchi online.

Tuongee kikubwa ,kumbe sheria ya faragha inaruhusu hadi kunyandua mbususu za wake za watu??
Huyu waziri kalewa madaraka,aliongea haya akiwa wapi?Hivi haoni aibu kwa wizara anayoongoza na idara zake inavyoboronga?Siyo POLISI,Zimàmoto ama Magereza? Ufanisi wao ungekuwa kipaumbele vya waziri lakini mafumanzi!
Too low for Internal Affairs Minister.
 
Nimemuelewa Waziri, na ndivyo ilivyo.

Nia tu ya kwenda kufumania huwa na lengo ovu la kudhuru...na sheria za nchi haziruhusu kujichukulia sheria mkononi.

Suala la kuzuia Watu wazima wasirubuniane mpaka kupelekana faragha lianzie kwa Wenza wenyewe huko kwenye ndoa zao.
 
Waziri wa mambo ya ndani ya nchi ndugu Gorgeous simbachawene amewanya wale wanaokusanyika ama kuandaa mafumanizi kuwa Hilo ni Jambo lililo kinyume Cha sheria hivyo ukifanya hivyo utakamatwa .

Amedai watu waachwe maana hizo ni faragha zao,.

Chanzo:
mwananchi online.

Tuongee kikubwa ,kumbe sheria ya faragha inaruhusu hadi kunyandua mbususu za wake za watu??
Faragha zote zinakubalika, isipokuwa faragha za mikutano ya vyama vya upinzani tu! Huo ndio msimamo wa serikali yetu.
 
Nimemsikiliza vizuri,amesema hivi wale ambao mnakaa na wanawake bila ndoa au mtu ana hawara lakini hakai nae halafu asikie hawara yupo Gest na mtu,huyo hana haki ya kumfumania mtu

Ila kama unataka kwenda kufumania hakikisha una cheti halali cha ndoa,Sio mtu ni demu au hawara yako kaamua kuachana na wewe au hata kama bado mpo nae halafu kaenda faragha na mtu mwingine wewe unatafuta watu mkafanye fumanizi,huna haki hio.

Unataka kwenda kufumania hakikisha una Cheti halali cha ndoa mkononi

Hata hivyo,ukifumania usijchukulie sheria mkononi
 
Ngoja uibiwe mkeo/demu wako ndio utaujua vizuri utamu wa hiyo sheria.
Huko nchi zilizotutangulia hata kumpiga Mwizi risasi zaidi ya moja bila ya sababu una kesi ya kujibu..wanakwambia ukishaimaliza hatari inatosha.

Huku kwetu sio tu kama hatufuati sheria, bali hata kuua tunadhani ni jambo halali ili mradi Mtu amekukosea.
 
Back
Top Bottom