Nikupateje
JF-Expert Member
- Dec 22, 2009
- 1,334
- 989
- Thread starter
-
- #81
Kiongozi hujaelewa mantiki. Vyote viwili vinatubana. Ramani ndio iliyopelekea mkataba ambao inaondoa ziwa nyasa lote kwenye miliki ya Tanganyika. Wote mfahamu pia kuwa huyo huyo Mwingereza ambae ni chanzo cha ramani au mkataba (as the case may be) ndie aliyetawala nchi hizi mbili (South Rhodesia -Malawi) na Tanganyika (TZ). Ndie ambae sasa anahusika na exploration kwenye ziwa Nyasa au Malawi. Tunachopaswa kuangalia ni msingi wa hoja zetu! Kwani mipaka na nchi nyingine tumenaithibitisha kwa kutumia nini kati ya Ramani au Mikataba? Kama tukienda kwa staili hii eti mipaka iliwekwa na wakoloni hatuwezi kushinda hoja kwani bila hiyo mipaka ya wakoloni hata leo sisi tusingejiita nchi huru Tanzanian na hata ile kesi yetu na wakenya kuhusu mlima kilimanjaro au ujenzi wa uwanja wa ndege wa kimataifa pale Taveta tutakosa hoja za msingi kwa nini hilo eneo lisiwe la Kenya (nini kinatulinda)?!. Kwa hili hata tukienda kidiplomasia tutaingia kwenye chaka la kutengeneza mkataba mpya kama sio kuambiwa tumilikishwe sehemu ndogo ya ziwa nyasa kwa kuwa kisheria hatuna haki ya moja kwa moja. Kuwapiga stop Malawi wasifanye utafiti kwny ziwa lote hatuwezi, wao wanatueleza wamenza kwa eneo wanalotumia sasa na wanaweza kuendelea au kuacha pindi mgogoro wa umiliki wa ziwa ukiisha. Umakini unahitajika kwa hili, wabongo siku zote tunaishi kwa kutumaini huruma za wenzetu.
Hakuna Heligoland Treaty ya Tanzania au ya Malawi. Heligoland Treaty kwa siku zote ni ileile moja na jina jingine inaitwa Anglo-German Agreement of 1890.
Hata Membe hajasema kwamba kuna mkataba mwingine zaidi ya huu (Helligoland) ama katika archive za Tanzania au za Malawi zinazoeleza ugawaji mpya wa mpaka huu uliopita kwenye kingo za ziwa {Eastern shore of Lake Malawi}.
Mkataba wenye mipaka ni huu tu. Hayo maneno au michoro mingine kama una justification nenda kai-submit kwa Membe upate award tushinde kesi hii.
Kumbe muda wote unakomaa hapa Nikupateje unatafuta tuzo?
Kwanini sasa hujampelekea membe hizi latitudes sahihi bali umezileta JF!?
Duh ama kweli!!! Ivi ni kwamba unatafuta kushinda au? Sawa inawezekana hawakupata uelewa huo kipind hicho sasa mambo ndo yameibuka, ivi kweli ndugu yangu kwa mfano ukaitwa kama shaidi huo utakua utetezi wako kweli , eti walikua wapi muda wote!!!
Sijaona popote pale alipo watetea wamalawi kinacho kushinda wewe ni uvivu wa kuelewa na kuamini hoja za Membe as if yeye awezi kukosea na kwamba eti kwakua ni waziri basi anaelewa kila kitu. Hili swala tusilifanye kiitikadi cse litatugarimu.Mleta mada ni mwenzetu na anachosema kinaeleweka sana hata huyo membe hataonekana mshamba akifuata ushauri wa huyu bwana.
Hivi unadhani haya uliyoeleza yanamsaidia Membe atakapokaa na wamalawi hapo August 20, 2012? Mbona kakaa nao majuzi lakini akienda hewani na mwenzake wa Malawi ni kama vile Membe anafundishwa geography and history?!
Ngoja nilale tutakutana asubuhi.
Kwa nini hupingi sisi kupata
sehemu ndogo? Kwa mawazo yako, hiyo sehemu ndogo, ni haki yetu kuipata
au unaona tupewe kwa fadhila ya Wamalawi?
Wewe Mmalawi usitake kutufanya sisi wabongo hatujuwi haya mambo, kukufahamisha ziwa Nyasa kwa juu liko latitude ya 9 degree na dakika 40 kwa longitude ya 34 degree na dakika 15 (kwenye lamani ya QDS 273/2) ambayo inaitwa Lupila.
Kusini ziwa liko kwenye longitude ya 34 degree na dakika 40 ambalo ni eneo la Lundu kwa wenyeji wa huko watakuwa wanapafaham na latitude yake ni 10 degree na dakika 45 (QDS 297-1 Lituhi).
Naomba nikukumbushe kitu kimoja unapotaja hizi point huwezi kutaja latitude pake yake bila kutaja longitude yake na kwa UTM Ssystem huwezi kutaje X- cordinate bila Y - cordinate na ARC1960 kwa WGS84 ni conversion tu ndugu yangu 300m kwa X na 200m kwa Y.
We gamba chama hapa tunazungumzia masuala ya kitaifa. Hizo siasa zako za mataputapu ya mabwepande ziache huko huko lumumba.
Nikupateje kwanza niseme tu kwamba sihitaji kukupata kama jina lako lilivyo.
Pili nikuulize unachohangaikia ni kitu gani? Ile thread yako nyingine ulipewa hoja za kutosha kukujibu hoja zako. Sasa umekuja kuanzisha nyingine yenye hoja zile zile.
Hii bidii unayofanya kujaribu kuhadaa watu na vilatitudes hapa wala haikusaidii wewe mnyasa na makuwadi wenzako wa kinyasa mliojazana hapa nchini.
Malawi hawawezi kumiliki ziwa lote, watake wasitake lazima kuna kipande chetu ndani ya ziwa nyasa.
Hebu waelez maana hata mimi nimesahau kukitaja unachokitaja. Kwamba baada ya Wordl Wara the first kwamba kuna ramani zilionyesha hivyo, na Waziri anatamka hivyo Bungeni na anapata washangiliaji huko Bungeni na huku mitandaoni. Ni uvivu wa kusoma na kutafiti kiasi kwamba inatia aibu.
Temporary treaty aimed at resolving the boundaries between British sphere of influence and German sphere of influence.Nimeisoma Heligoland Treaty neno kwa neno na nimerudia mara kadhaa. Na kila nikiisoma sioni tutachomokea wapi kuhusu hili la Malawi.
ni vita za 2015 ndani ya ccm mkuu... kitu gani huoni hapo??? yani unaona mkia halafu bado unauliza mku**du wa mbwa uko wapi??? nyanyua mkia utaona tunduNikupateje kwanza niseme tu kwamba sihitaji kukupata kama jina lako lilivyo.
Pili nikuulize unachohangaikia ni kitu gani? Ile thread yako nyingine ulipewa hoja za kutosha kukujibu hoja zako. Sasa umekuja kuanzisha nyingine yenye hoja zile zile.
Hii bidii unayofanya kujaribu kuhadaa watu na vilatitudes hapa wala haikusaidii wewe mnyasa na makuwadi wenzako wa kinyasa mliojazana hapa nchini.
Malawi hawawezi kumiliki ziwa lote, watake wasitake lazima kuna kipande chetu ndani ya ziwa nyasa.
asante kwa masahihisho, hilo ziwa unataka kuniambia kuwa kabla ya kuja kwa wakoloni lilikuwa linatumika na upande mmoja tu yaani malawi?? halafu mbaya zaidi watershed ipo upande wetu yaani milima inayotiririsha maji ipo kwetu kwa nn tunyimwe haki ya kulitumia kisa wakoloni??OSOKONI miaka ya 70 inamaanisha kati ya mwaka 1970 na 1980 siyo 1979! right?
By the way nafurahi kujua kuwa huyu@Nikupatejew ni Mnyasa na ndiyo maana anatokwa mishipa ya shingo kutetea Malawi kwamba inamiliki ziwa Nyasa kwa 100%!
Basi nazipuuza threads zake tangu sasa!
mimi naona hapa kuna hoja, hebu tuchangie badala ya kuhukumu mleta hoja kama mnyasa wa malawi au wa TZ! Kesho akichangia mmakonde utasema nae ni wa msumbiji?Mnyasa wa Maravi huyu ...:hat: