Waziri Bashungwa atoa siku 7 mabasi yote ya mikoani yawe yanaingia Magufuli Bus Terminal, si Shekilango

zandrano

JF-Expert Member
Jan 24, 2017
7,129
7,710
Waziri wa Tamisemi Mhe. Bashungwa leo amesisitiza mabasi yote yaendayo Mikoani pamoja na nchi jirani lazima yapakie na kushushia abiria katika kituo kikuu cha Mabasi cha Magufuli ameyasema hayo leo wakati akizungumza na wadau wa usafirishaji.

Ni vyema waziri kalizungumzia hilo maana hali ilipo kuwa imefikia ilikuwa ni vurugu yaani kama vile hakuna wasimamizi wa sheria au hakuna viongozi maana kila basi illikuwa inaamua ikapakie abiria wapi na ikashushie wapi!! askari wapo! wanaangalia jinsi watu wanavyo vunja sheria!!

Hapana, lazima kituo chetu cha Magufuli kitumiwe kama ilivyo kusudiwa, hivyo ni vyema wenye mamlaka wakasimamia hilo.

===

Waziri Bashungwa atoa siku saba Stendi Kuu ya Magufuli-Dar​


WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Innocent Bashungwa ametoa siku saba kwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Amos Makalla kukutana na LATRA, Wadau na Wamiliki wa Mabasi kuweka uratibu mzuri wa kusimamia maelekezo ya Serikali kwa mabasi yote kushusha na kupakia abiria ndani ya Kituo Kikuu cha Mabasi cha Magufuli jijini Dar es Salaam.


Bashungwa ametoa maelekezo hayo leo Mei 30, 2022 wakati akikagua mradi wa Kituo Kikuu cha Mabasi cha Magufuli (Magufuli Bus Terminal) kilichopo Wilaya ya Ubungo jijini Dar es Salaam.

Amesema, Serikali imetumia kiasi cha shilingi bilioni 50 kujenga kituo hicho, hivyo Serikali haitakubaliana na watu ambao hawazingatii utaratibu uliowekwa katika kituo hicho.

“Ninafahamu kuwa Mkuu wa Mkoa, Amos Makalla ameshapokea changamoto ya Mabasi kutoingia ndani ya kituo hiki cha Magufuli na mimi nimekuta changamoto bado iko pale pale, sasa kwa sababu ameshanza kulifanyia kazi nampa siku saba awe amekutana na LATRA pamoja na wadu wa mabasi (TABOA) kuangalia utaratibu wa mabasi yote kuingia ndani ya kituo kushusha na kupakia abiria,”amesema Bashungwa.

Pia Mheshimiwa Bashungwa amemuagiza Mkuu wa Wilaya Ubungo, Kheri James kuweka utaratibu wa kukutana mara kwa mara na Wadau wa Kituo cha Magufuli, Mawakala na Makalani ili kusikiza na kuweka utaratibu wa kutatua changamoto ambazo zimekuwa zikijitokeza katika kituo hicho na kuzifanyia kazi kwa ushirikiano.
 
Tatizo moja la stendi ya Magufuli ni kwamba haliko accesible kwa mabasi madogo yanayoleta na kupokea wasafiri.

Magufuli alisema anatambua ile ni stendi ya wanyonge na akataka iwahudumie accordingy.

Sasa watu wanaosafiri na mabasi ya mikoani hawaletwi pale au kupokelewa pale na ma landcruisers binafsi.

Lakini stendi kuu ya daladala, Mbezi Louis, iko opposite side of the highway. Wengi watapondwa na magari.

Tatizo la nchi yetu, watu wanao design miundombinu na mifumo mbali mbali ya umma, wao hawaitumii, kwa hiyo hawajui inavyofanya na isivyofanya kazi.

Disastrously poor designing.
 
Nashauri trafiki wasimamie hili jambo ipasavyo, piga faini kali kwa basi lolote litakalo kiuka utaratibu.
Lakini pia viongozi wetu kamilisheni maboresho ktk stendi hiyo ya kimataifa.
Stendi ya Magufuli ni UCHUMI WA NCHI tuache mzaha na masihara
 
Mtoa mada unafurahia ujinga tu bila kutumia Busara, Basi likianzia Mbagala halafu likaingia hapo Magufuli likalipa ushuru kama kawaida nini kitapungua? Kuna abiria wanatoka mbali sana kumbuka
Mkuu, Kuna magari hayaingii kabisa pale. Mfano, tahmeed, Kilimanjaro, bm, etc.

Kifupi gari nyingi za kwenda kaskazini zinazopaki Shekilango hazipiti Mbezi(asubuhi) na haziingii(kwa zinazotoka mkoani).
 
Mtoa mada unafurahia ujinga tu bila kutumia Busara, Basi likianzia Mbagala halafu likaingia hapo Magufuli likalipa ushuru kama kawaida nini kitapungua? Kuna abiria wanatoka mbali sana kumbuka
Mkuu, Kuna magari hayaingii kabisa pale. Mfano, tahmeed, Kilimanjaro, bm, etc. Kifupi gari nyingi za kwenda kaskazini zinazopaki shekilango hazipiti mbezi(asubuhi) na haziingii(kwa zinazotoka mkoani).
 
Hapa ni pigo kwa wale wazee wa big brother pale urafik
Atofautishe gari zinapolala na zinapopakia.

Pia akumbuke hizi basi nyingi zina booking office sehemu ambayo basi pia lazima lifike lichukue na mizigo.

Sasa si vibaya abiria wengine hasa wenye mizigo wapandie hapo au washukie hapo ukizingatia stendi nyingi hizi mpya zimejengwa mbali na mji.
 
Waziri wa Tamisemi Mhe. Bashungwa leo amesisitiza mabasi yote yaendayo Mikoani pamoja na nchi jirani lazima yapakie na kushushia abiria katika kituo kikuu cha Mabasi cha Magufuli ameyasema hayo leo wakati akizungumza na wadau wa usafirishaji.

Ni vyema waziri kalizungumzia hilo maana hali ilipo kuwa imefikia ilikuwa ni vurugu yaani kama vile hakuna wasimamizi wa sheria au hakuna viongozi maana kila basi illikuwa inaamua ikapakie abiria wapi na ikashushie wapi!! askari wapo! wanaangalia jinsi watu wanavyo vunja sheria!!

Hapana, lazima kituo chetu cha Magufuli kitumiwe kama ilivyo kusudiwa, hivyo ni vyema wenye mamlaka wakasimamia hilo.
Kauli imeamrisha. Lakini subiri kwenye kusimamia utekelezaji ndio utajua hujui
 
Waziri wa Tamisemi Mhe. Bashungwa leo amesisitiza mabasi yote yaendayo Mikoani pamoja na nchi jirani lazima yapakie na kushushia abiria katika kituo kikuu cha Mabasi cha Magufuli ameyasema hayo leo wakati akizungumza na wadau wa usafirishaji.

Ni vyema waziri kalizungumzia hilo maana hali ilipo kuwa imefikia ilikuwa ni vurugu yaani kama vile hakuna wasimamizi wa sheria au hakuna viongozi maana kila basi illikuwa inaamua ikapakie abiria wapi na ikashushie wapi!! askari wapo! wanaangalia jinsi watu wanavyo vunja sheria!!

Hapana, lazima kituo chetu cha Magufuli kitumiwe kama ilivyo kusudiwa, hivyo ni vyema wenye mamlaka wakasimamia hilo.
Ugomvi wa weyewe kwa wenyewe huku Zhabibu huku Machungwa!
 
Hii ya stendi magari kutokuingia kule ni uzembe tu.

Kila kitu kinakwenda kwa mkakati.

Mimi Binafsi waziri ningemshauri kitu kidogo hayo mabasi yote yangekuwa yanapaki kule, lazima tukubaliane.
 
Kauli imeamrisha. Lakini subiri kwenye kusimamia utekelezaji ndio utajua hujui
Naamini Jeshi la Polisi ndio jukumu lao kusimamia utekelezaji wa sheria na taratibu, hivyo watakuwa imara zaidi.
ni aibu kuona sheria zinavunjwa wakati wasimamizi wapo, viongozi wapo!

Stendi ya Kimataifa ya Magufuli imekuwa Gumzo ktk nchi zingine kwa kuwa kituo kikubwa na cha kisasa, hivyo ni muhimu viongozi wetu wakaelewa kuwa STENDI YA MABASI YA MAGUFULI ni UCHUMI wa NCHI.

SERIKALI imewekeza 50Billion sasa tunaanza kufanya mzaha na kupuuza kwa nini? Hapana hii haikubaliki.
 
Waziri wa Tamisemi Mhe. Bashungwa leo amesisitiza mabasi yote yaendayo Mikoani pamoja na nchi jirani lazima yapakie na kushushia abiria katika kituo kikuu cha Mabasi cha Magufuli ameyasema hayo leo wakati akizungumza na wadau wa usafirishaji.

Ni vyema waziri kalizungumzia hilo maana hali ilipo kuwa imefikia ilikuwa ni vurugu yaani kama vile hakuna wasimamizi wa sheria au hakuna viongozi maana kila basi illikuwa inaamua ikapakie abiria wapi na ikashushie wapi!! askari wapo! wanaangalia jinsi watu wanavyo vunja sheria!!

Hapana, lazima kituo chetu cha Magufuli kitumiwe kama ilivyo kusudiwa, hivyo ni vyema wenye mamlaka wakasimamia hilo.
Safi sana Waziri simamia hapo hapo tena wafatilie kwa karibu haiwezekani kila mtu apaki anakojua yeye.
 
Back
Top Bottom