Waziri Bashungwa Apiga Kambi Lindi, Barabara ya Liwale - Nangurukuru Yaanza Kupitika

Stephano Mgendanyi

JF-Expert Member
May 16, 2020
1,898
943
Waziri wa Ujenzi, Innocent Bashungwa ameipongeza timu ya Wataalam kutoka Wizara ya Ujenzi na Wakala wa Barabara Nchini (TANROADS), kwa kufanya kazi usiku na mchana kuhakikisha wanarejesha mawasiliano ya barabara ya Liwale - Nangurukuru ambayo imeanza kupitika.

Waziri Bashungwa ameeleza hayo leo Machi 08, 2024 mkoani Lindi wakati akikagua urejeshwaji wa miundombinu ya barabara na madaraja kutokana na mvua kubwa iliyonyesha na kusababisha barabara kuu na madaraja yanayounganisha wilaya ya Liwale na maeneo mengine kufungwa.

Bashungwa amemuagiza Mtendaji Mkuu wa TANROADS Eng. Mohamed Besta kuweka Wakandarasi watatu kwa wakati mmoja kufanya ukarabati upya barabara ya Nangurukuru - Liwale yenye urefu wa kilometa 230.

“Sasa hivi tumefungua barabara ya Nangurukuru - Liwale, maelekezo yangu kwa TANROADS ni kuweka Makandarasi watatu kila mmoja na kipande chake kukarabati upya barabara hii na kuhakikisha barabara inapitika vizuri, hicho ndicho kipimo ninachowaachia Wahandisi na Makandarasi” amesema Bashungwa.

Aidha, Bashungwa ametoa wito kwa Makandarasi nchi nzima kuzingatia taratibu na Sheria za taaluma ya Ukandarasi na kuondokana na hali ya kufanya kazi kwa mazoea na amewataka kuwa Wazalendo na kutanguliza masilahi ya nchi wakati wakitekeleza Majukumu yao.

“Bodi ya Usajili ya Wahandisi (ERB) na Bodi ya Usajili wa Makandarasi (CRB) ninataka msimamie taaluma hizi, hata TANROADS mnaposaini mikataba simamieni vigezo na masharti yaliyopo kwenye mikataba na kuhakikisha wanaopewa kazi hizo wanakuwa na taaluma na kazi” amesisitiza Bashungwa.

Bashungwa amewahakikishia Wananchi wa wilaya Liwale na Mkoa wa Lindi kwa ujumla kuwa Serikali itaendelea kufanya kila jitihada za kuhakikisha hali ya miundombinu na huduma nyingine muhimu zinarejea na kuendelea kutolewa.

Vile vile, Bashungwa ametumia fursa hiyo kutuma salamu za heri siku ya Wanawake duniani kwa Mheshimiwa Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan na Wanawake wote nchini.

WhatsApp Image 2024-03-08 at 13.45.01.jpeg
WhatsApp Image 2024-03-08 at 13.45.01(1).jpeg
WhatsApp Image 2024-03-08 at 13.45.07.jpeg
WhatsApp Image 2024-03-08 at 13.45.07(1).jpeg
WhatsApp Image 2024-03-08 at 13.45.08.jpeg
WhatsApp Image 2024-03-08 at 13.45.09.jpeg
WhatsApp Image 2024-03-08 at 13.45.10.jpeg
WhatsApp Image 2024-03-08 at 13.45.11.jpeg
WhatsApp Image 2024-03-08 at 13.45.11(1).jpeg
 
Waziri wa Ujenzi, Innocent Bashungwa ameipongeza timu ya Wataalam kutoka Wizara ya Ujenzi na Wakala wa Barabara Nchini (TANROADS), kwa kufanya kazi usiku na mchana kuhakikisha wanarejesha mawasiliano ya barabara ya Liwale - Nangurukuru ambayo imeanza kupitika.

Waziri Bashungwa ameeleza hayo leo Machi 08, 2024 mkoani Lindi wakati akikagua urejeshwaji wa miundombinu ya barabara na madaraja kutokana na mvua kubwa iliyonyesha na kusababisha barabara kuu na madaraja yanayounganisha wilaya ya Liwale na maeneo mengine kufungwa.

Bashungwa amemuagiza Mtendaji Mkuu wa TANROADS Eng. Mohamed Besta kuweka Wakandarasi watatu kwa wakati mmoja kufanya ukarabati upya barabara ya Nangurukuru - Liwale yenye urefu wa kilometa 230.

“Sasa hivi tumefungua barabara ya Nangurukuru - Liwale, maelekezo yangu kwa TANROADS ni kuweka Makandarasi watatu kila mmoja na kipande chake kukarabati upya barabara hii na kuhakikisha barabara inapitika vizuri, hicho ndicho kipimo ninachowaachia Wahandisi na Makandarasi” amesema Bashungwa.

Aidha, Bashungwa ametoa wito kwa Makandarasi nchi nzima kuzingatia taratibu na Sheria za taaluma ya Ukandarasi na kuondokana na hali ya kufanya kazi kwa mazoea na amewataka kuwa Wazalendo na kutanguliza masilahi ya nchi wakati wakitekeleza Majukumu yao.

“Bodi ya Usajili ya Wahandisi (ERB) na Bodi ya Usajili wa Makandarasi (CRB) ninataka msimamie taaluma hizi, hata TANROADS mnaposaini mikataba simamieni vigezo na masharti yaliyopo kwenye mikataba na kuhakikisha wanaopewa kazi hizo wanakuwa na taaluma na kazi” amesisitiza Bashungwa.

Bashungwa amewahakikishia Wananchi wa wilaya Liwale na Mkoa wa Lindi kwa ujumla kuwa Serikali itaendelea kufanya kila jitihada za kuhakikisha hali ya miundombinu na huduma nyingine muhimu zinarejea na kuendelea kutolewa.

Vile vile, Bashungwa ametumia fursa hiyo kutuma salamu za heri siku ya Wanawake duniani kwa Mheshimiwa Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan na Wanawake wote nchini.

View attachment 2928475View attachment 2928476View attachment 2928477View attachment 2928478View attachment 2928479View attachment 2928480View attachment 2928482View attachment 2928483View attachment 2928484View attachment 2928485
Barabara ya Liwale-Nangurukuru iwekwe lami

Barabara ya Liwale-Nachingwea-Masasi-Newala-Tandahimba-Mtwara iwekwe lami


Huo ndio MuaRubaini.



Kukarabati kila mwaka mi naona ni michongo tu ya makampuni ya watu fulani kuvuta hela za wananchi.
 
Barabara ya Liwale-Nangurukuru iwekwe lami

Barabara ya Liwale-Nachingwea-Masasi-Newala-Tandahimba-Mtwara iwekwe lami


Huo ndio MuaRubaini.



Kukarabati kila mwaka mi naona ni michongo tu ya makampuni ya watu fulani kuvuta hela za wananchi.
Nakubaliana na wewe, barabara ya mkoa mpaka mkoa bila lami ni kupoteza mda
 
Kuna wilaya inaitwa Malinyi sijawahi kuona wilaya inabarabara mbovu kama ile wilaya na mvua ikinyesha ndo hatari zaidi sijawahi kusikia kiongozi yeyote anaongelea wilaya ile
#miaka 60 ya uhuru
 
Back
Top Bottom