Waziri Bashe, bei elekezi ya Sukari inaanza kutumika lini?

Lady Whistledown

JF-Expert Member
Aug 2, 2021
1,024
1,616
Habari Wakuu, baada ya Bodi ya Sukari Nchini kutangaza bei elekezi ya Sukari, kuwa 2,700 hadi 3,200, kwa Kilogramu 1, siku 6 baadaye bado Wananchi wana sintofahamu nyingi sana

Mimi binafsi nina Maswali kadhaa ambayo natamani yapate Majibu kutoka katika Wizara husika

1. Bei elekezi inaanza lini? Baada ya tamko la Waziri au baada ya zile Tani 100,000 zilizoagizwa kuingizwa sokoni? Maana hadi sasa bei bado ni changamoto kila mtu ana bei yake

2. Mtu akiuziwa Sukari Kilo 4,000 anaripoti wapi? Maana Waziri aliishia tuu kusema Wafanyabiashara wasiotiii tamko watakuwa wamevunja Sheria. Mamlaka inapaswa kuweka wazi hili na pia hatua ziwe zina uhalisia. Maana ukimwambia tuu mtu 'ukikuta bei tofauti ripoti' ana ripoti wapi? Nilitarajia tamko liseme watu waripoti kwa Viongozi wa Mtaa au wapige namba fulani kwa utatuzi wa haraka

3. Halafu Serikali inasubiri nini kuweka Kikosi kazi cha kupita mtaani na kukamata WafanyaBiashara wanaokiuka Tamko la Waziri? Kwa sababu kutoa tamko bila Ufuatiliaji ni sawa na kuwaachia maamuzi wafanyabiashara, kwamba waamue wanafuata Tamko au laa.

Nawasilisha!
 
UKWELI ni kuwa sukari ni pungufu nchini,

Bashe anafanya maigizo,wizara yake imefail kuagiza sukari JIT kufidia upungufu mapema.

Bei hiyo elekezi itaanza pale sukari Toka nje itakapowasili.
 
Habari Wakuu, baada ya Bodi ya Sukari Nchini kutangaza bei elekezi ya Sukari, kuwa 2,700 hadi 3,200, kwa Kilogramu 1, siku 6 baadaye bado Wananchi wana sintofahamu nyingi sana

Mimi binafsi nina Maswali kadhaa ambayo natamani yapate Majibu kutoka katika Wizara husika

1. Bei elekezi inaanza lini? Baada ya tamko la Waziri au baada ya zile Tani 100,000 zilizoagizwa kuingizwa sokoni? Maana hadi sasa bei bado ni changamoto kila mtu ana bei yake

2. Mtu akiuziwa Sukari Kilo 4,000 anaripoti wapi? Maana Waziri aliishia tuu kusema Wafanyabiashara wasiotiii tamko watakuwa wamevunja Sheria. Mamlaka inapaswa kuweka wazi hili na pia hatua ziwe zina uhalisia. Maana ukimwambia tuu mtu 'ukikuta bei tofauti ripoti' ana ripoti wapi? Nilitarajia tamko liseme watu waripoti kwa Viongozi wa Mtaa au wapige namba fulani kwa utatuzi wa haraka

3. Halafu Serikali inasubiri nini kuweka Kikosi kazi cha kupita mtaani na kukamata WafanyaBiashara wanaokiuka Tamko la Waziri? Kwa sababu kutoa tamko bila Ufuatiliaji ni sawa na kuwaachia maamuzi wafanyabiashara, kwamba waamue wanafuata Tamko au laa.

Nawasilisha!
Wafanyabiashara wanapata changamoto kwenye hili, Kwa sababu unakuta yeye amenunua sugari Kwa bei kabla ya tamko ambayo ni kubwa ,kisha uwaambie wauze Kwa bei baada ya maelekezo ya serikali ambayo ni ya bei chini ,Hali ambayo inaleta hasara kwao .Hii aswaaswa inawakumba wafanyabiashara wadogo.
 
Habari Wakuu, baada ya Bodi ya Sukari Nchini kutangaza bei elekezi ya Sukari, kuwa 2,700 hadi 3,200, kwa Kilogramu 1, siku 6 baadaye bado Wananchi wana sintofahamu nyingi sana

Mimi binafsi nina Maswali kadhaa ambayo natamani yapate Majibu kutoka katika Wizara husika

1. Bei elekezi inaanza lini? Baada ya tamko la Waziri au baada ya zile Tani 100,000 zilizoagizwa kuingizwa sokoni? Maana hadi sasa bei bado ni changamoto kila mtu ana bei yake

2. Mtu akiuziwa Sukari Kilo 4,000 anaripoti wapi? Maana Waziri aliishia tuu kusema Wafanyabiashara wasiotiii tamko watakuwa wamevunja Sheria. Mamlaka inapaswa kuweka wazi hili na pia hatua ziwe zina uhalisia. Maana ukimwambia tuu mtu 'ukikuta bei tofauti ripoti' ana ripoti wapi? Nilitarajia tamko liseme watu waripoti kwa Viongozi wa Mtaa au wapige namba fulani kwa utatuzi wa haraka

3. Halafu Serikali inasubiri nini kuweka Kikosi kazi cha kupita mtaani na kukamata WafanyaBiashara wanaokiuka Tamko la Waziri? Kwa sababu kutoa tamko bila Ufuatiliaji ni sawa na kuwaachia maamuzi wafanyabiashara, kwamba waamue wanafuata Tamko au laa.

Nawasilisha!
Hawa jamaa wa Ccm majibu yao hayana tofauti na mwenye tumbo la kuharisha. Ukisha toa uchafu tumbo hutulia kwa muda. Vivyo na Ccm hutoa majibu ya funika kombe mwana haramu apite. Hakuna ufuatiliaji.
 
Wafanyabiashara wanapata changamoto kwenye hili, Kwa sababu unakuta yeye amenunua sugari Kwa bei kabla ya tamko ambayo ni kubwa ,kisha uwaambie wauze Kwa bei baada ya maelekezo ya serikali ambayo ni ya bei chini ,Hali ambayo inaleta hasara kwao .Hii aswaaswa inawakumba wafanyabiashara wadogo.
Mbona mafuta huwezekanaa? Wao hawa pati hasara?
 
Haipitagi miak miwili bila mgogoro wa sukari

By the way tunakwenda kuagiza sukari nnje ya nchi wakt sukari imejaa uaganda na Zambia

Kwanin wasinunue huko na Bei ikawa ndogo
 
Back
Top Bottom