Roving Journalist
JF Roving Journalist
- Apr 18, 2017
- 4,783
- 14,975
Aweso ametoa malekezo hayo kupitia kwa Meneja wa RUWASA Mkoa, Eng Boazi Piusi Matundali ikiwa ni baada ya Mdau wa JamiiForums.com kueleza kuwa Wakazi wa eneo hilo wanapitia changamoto ya kukosa huduma ya maji tangu mwezi wa 11, 2025 mwanzoni baada ya Uchaguzi Mkuu.
Mhandisi Matundali amesema “Kulitokea uharibifu wa mabomba na kilichochelewesha matengenezo ni kwa kuwa suala hilo lilikuwa linafanyiwa uchunguzi na Mamlaka za Kiusalama, lakini utaratibu umefanyika na tayari Waziri Aweso ameshatoa maelekezo ya matengenezo ambayo yatafanyika ndani ya wiki moja.