Waziri Aweso aiagiza DAWASA kushirikiana na wenye visima

Izia maji

JF-Expert Member
Dec 1, 2021
2,155
3,797
Kutokana na kupungua kwa maji katika Mto Ruvu ambao unatumika kusambaza maji katika baadhi ya maeneo ya mkoa wa Pwani na mkoa wa Dar es Salaam, Waziri wa Maji Jumaa Aweso ameiagiza DAWASA kushirikiana na wenye visima vya maji kutoa huduma hiyo ili kupunguza madhira yanayowapata wakazi wa mikoa hiyo.

Agizo hilo linatengua amri ya DAWASA iliyokuwa inawazuia wenye visima kusambaza maji.

=======
Waziri wa Maji Jumaa Aweso ameiagiza Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA) kushirikiana na wadau wengine wenye visima vikubwa vya maji kutoa huduma ya maji kwa kipindi chote cha ukame.

Akikagua zoezi la uunganishaji wa mabomba ya maji eneo la Wazo mkoani Dar es Salaam, Waziri Aweso amesema wizara yake itashirikiana na DAWASA kuhakikisha wananchi wanapata huduma ya maji katika kipindi chote cha ukame.

Pia ameielekeza DAWASA kuzingatia vema ratiba ya mgao wa maji na kugawa maji bila ya upendeo.

Kwa upande wake Afisa Mtendaji Mkuu wa DAWASA mhandisi Cyprian Luhemeja amesema, mradi wa maji ya visima wa Kigamboni utakamilika siku ya Jumapili na hivyo kuwawezesha wananchi kupata huduma ya maji.

Tarehe 25 mwezi huu mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam, Amos Makalla alitangaza kuanza rasmi kwa mgao wa maji mkoani humo na katika baadhi ya maeneo ya mkoa wa Pwani, kufuatia kupungua kwa kina cha maji katika mto Ruvu.

TBC Online
 
Hivi zile sheria pindi zinatungwa, walifikiria nje ya box au hizo mamlaka zinataka tu kujipendelea zenyewe..Basi inabidi wazitengue hazina msaada kwetu,
 
Futeni hio sheria inayomonopolize huduma ya maji kwa mamlaka za maji nchini.

Hata wafanye vipi hawawezi jitosheleza kusupply maji.
 
Kutokana na kupungua kwa maji katika Mto Ruvu ambao unatumika kusambaza maji katika baadhi ya maeneo ya mkoa wa Pwani na mkoa wa Dar es Salaam, Waziri wa Maji Jumaa Aweso ameiagiza DAWASA kushirikiana na wenye visima vya maji kutoa huduma hiyo ili kupunguza madhira yanayowapata wakazi wa mikoa hiyo.

Agizo hilo linatengua amri ya DAWASA iliyokuwa inawazuia wenye visima kusambaza maji.
Dawasa wapuuzi,wao maji wameshindwa kusambaza, wananchi wenye visima wamehamua kuwasaidia wenzao,eti Dawasa hawataki, inamaana wanataka tufe kwa kukosa maji wapuuzi hawa
 
Yani naona Mnazunguka Mbuyu Tu....!.
Kweli mpaka leo hamjajua Mchawi kwenye nchi hii ni nani...
 
Kutokana na kupungua kwa maji katika Mto Ruvu ambao unatumika kusambaza maji katika baadhi ya maeneo ya mkoa wa Pwani na mkoa wa Dar es Salaam, Waziri wa Maji Jumaa Aweso ameiagiza DAWASA kushirikiana na wenye visima vya maji kutoa huduma hiyo ili kupunguza madhira yanayowapata wakazi wa mikoa hiyo.

Agizo hilo linatengua amri ya DAWASA iliyokuwa inawazuia wenye visima kusambaza maji.

=======
Waziri wa Maji Jumaa Aweso ameiagiza Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA) kushirikiana na wadau wengine wenye visima vikubwa vya maji kutoa huduma ya maji kwa kipindi chote cha ukame.

Akikagua zoezi la uunganishaji wa mabomba ya maji eneo la Wazo mkoani Dar es Salaam, Waziri Aweso amesema wizara yake itashirikiana na DAWASA kuhakikisha wananchi wanapata huduma ya maji katika kipindi chote cha ukame.

Pia ameielekeza DAWASA kuzingatia vema ratiba ya mgao wa maji na kugawa maji bila ya upendeo.

Kwa upande wake Afisa Mtendaji Mkuu wa DAWASA mhandisi Cyprian Luhemeja amesema, mradi wa maji ya visima wa Kigamboni utakamilika siku ya Jumapili na hivyo kuwawezesha wananchi kupata huduma ya maji.

Tarehe 25 mwezi huu mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam, Amos Makalla alitangaza kuanza rasmi kwa mgao wa maji mkoani humo na katika baadhi ya maeneo ya mkoa wa Pwani, kufuatia kupungua kwa kina cha maji katika mto Ruvu.

TBC Online
KAULI YA MHESHIMIWA WAZIRI WA MAJI YAIPINGA DAWASA.

DAWASA yatoa notisi ya kusitisha usambazaji wa maji ya Visima kwa baadhi ya Maeneo ya Jiji la Dar es salaam.​

Mamlaka ya Huduma za Usambazaji wa Maji na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam(DAWASA) imetoa agizo la kusitisha biashara ya usambazaji wa maji ya visima katika baadhi ya maeneo ya jiji la Dar es salaam ndani ya siku thelathini (30) kabla hatua kali za kisheria hazijachukuliwa kwa wahusika.

Agizo hili linatokana na kupanuka na kuongezeka kwa wigo wa miundombinu ya DAWASA katika kufikia wateja wengi ambao awali walikuwa hawawezi kupata huduma hii pamoja na ukiukwaji wa sheria ya huduma za usambazaji wa maji ya kisima kinyume cha Sheria ya huduma ya usambazaji maji na usafi wa mazingira Namba 5 ya mwaka 2019 ambapo imepiga marufuku mtu yoyote kujihusisha na usambazji wa maji isipokuwa mamlaka husika tu.

Oktoba 25, 2022, Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe. Amos Makalla alithibitisha uwepo wa upungufu mkubwa wa maji mto Ruvu, hivyo kuwataka wakazi wa jiji hilo wajiandae na mgao wa maji.

BB8E150B-D931-42E3-BC2A-F38317454899.jpg

Kuhusu uwepo wa mgao wa maji kwenye jiji la Dar es salaam unaweza kusoma hapa: Rasmi Dar yakumbwa na uhaba wa Maji, RC Makalla athibitisha uwepo wa Mgao
 
Back
Top Bottom