Waziri awataka Wachina kuoa Watanzania, si kusimama nao vichochoroni

Kumbe Mwijage alikua ni mlango sasa ulitolewa mlango wa debe ikawekwa pazia, Tanzania yangu jamanii.
Dar es Salaam. Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji Joseph Kakunda amewataka raia wa China nchini wakitaka kuwa na uhusiano wa kimapenzi na wanawake wa Watanzania wafuate taratibu.

Kakunda ametoa kauli hiyo jana jioni Desemba 7, 2018 wakati akizindua kituo cha maonyesho ya bidhaa za Kichina kilichopo Keko jijini Dar es Salaam.

Amesema nafasi za uwekezaji Tanzania na kuwakaribisha Wachina kuwekeza, kuwataka pale wanapotaka wanawake wanapaswa kufuata sheria na taratibu na kuachana na tabia ya kusimama na mabinti vichochoroni na kuwaachia watoto.

“Huku kwetu huwa tunakwenda kwa wazazi kujitambulisha kwa kutoa posa na kuoa kwa sherehe kubwa na mdundiko unapigwa,” amesema Kakunda.

“Fuateni taratibu hizo acheni kusimama simama vichochoroni na wasichana wa watu, hii nchi ya amani mkifanya hivyo mnawakera wazazi wao.”

Kakunda amewataka Wachina hao kuendeleza urafiki wa nchi hizo mbili kwa kuishi kwa kufuata sheria na taratibu za nchi.

“Njooni muwekeze lakini dumisheni urafiki ulioanzishwa na waasisi wa nchi yetu na China kwa kufuata mila, tamaduni za nchi, mziheshimu.

Ameongeza, “Mkienda Arusha kuna Wamasai wana taratibu zao wakati mwingine wanavaa shuka pekee bila kitu kingine ndani msistuke ndiyo tamaduni zao, hivyo mnapaswa kuziheshimu.”

Wakati akizungumza alikuwa na mkalimani aliyekuwa akitafsiri kwa Kichina na kuwafanya raia wa nchi hiyo waliokuwa eneo hilo kuangua kicheko.

Chanzo: Mwananchi
 
Huyu jamaa yuko na logic sema kwa akili za watanzania ataambulia matusi mpaka achoke. Binafsi nawafahamu wadada 3 walipewa mimba na wachina siku ya siku wakaenda zao na familia zinapata shida. Society cohesion is an inevitable evidence for an human centered development. Watanzania tuachane na kufikiri kwa kutumia utumbo
 
Msisahau na Yeye ni binadamu.Ambapo si muda wote atakuwa anaimba viwanda,wakati mwingine lazima a joke,kutoa stress anazozipata kwa Jiwe
hawezi kufanya jokes nje ya majukumu ya umma?

Ebu acheni kuwafariji na neno joke, joke ina mahala pake na muda wake!

uko mbele ya watu kama kiongozi wanakusikiliza halafu unatoa boko baadae uje utwambie ni jokes,? hii jokes itakua imeanza na hawa wa season ya tano tu!
 
Huyu waziri hajakurupuka, yuko sahihi kabisa kwa sababu kafanya uchunguzi na amegundua Dada zetu wanapewa sana mimba na wachina halafu wanatokemea wanatuachia vitoto tulee. Sio hao tu pia suala la mapenzi ni gumu sana kushauri au kuzuia mtu asifanye. Ameona Dada zetu wanapapalika sana na wachina ambao sio waoaji zaidi ya kuwachezea na kuwaacha ndo maana ameshauri waoe maana sisi watanzania hatuna mipaka kwenye masuala ya ndoa mtu anaolewa popote atakapo
 
Huyu waziri hajakurupuka, yuko sahihi kabisa kwa sababu kafanya uchunguzi na amegundua Dada zetu wanapewa sana mimba na wachina halafu wanatokemea wanatuachia vitoto tulee. Sio hao tu pia suala la mapenzi ni gumu sana kushauri au kuzuia mtu asifanye. Ameona Dada zetu wanapapalika sana na wachina ambao sio waoaji zaidi ya kuwachezea na kuwaacha ndo maana ameshauri waoe maana sisi watanzania hatuna mipaka kwenye masuala ya ndoa mtu anaolewa popote atakapo
Mkuu hili watu hawawezi lifikiria kabisa ila kwa sababu ya kupuuzia kila jambo wanakurupuka na kuaanza kumbeza bila ya kufikiri
 
hawezi kufanya jokes nje ya majukumu ya umma?

Ebu acheni kuwafariji na neno joke, joke ina mahala pake na muda wake!

uko mbele ya watu kama kiongozi wanakusikiliza halafu unatoa boko baadae uje utwambie ni jokes,? hii jokes itakua imeanza na hawa wa season ya tano tu!
Halafu watu wenyewe wageni! E ti joke naunga mkono hoja yako. Tusifarijiane ujinga
 
Huyu jamaa yuko na logic sema kwa akili za watanzania ataambulia matusi mpaka achoke. Binafsi nawafahamu wadada 3 walipewa mimba na wachina siku ya siku wakaenda zao na familia zinapata shida. Society cohesion is an inevitable evidence for an human centered development. Watanzania tuachane na kufikiri kwa kutumia utumbo
Watanzania wangapi wanawapa mimba wasichana na wanawaterekeza? Kwa sababu ni wachina ndo walaumiwe? Walifanya kwa ihari, condom zipo na vidonge vya majira.
 
Wanawake wa kitanzania watasema hawataki kuolewa na vibamia wanataka hela yao tu.


Ndukiiiii 🏃‍♂️🏃‍♂️🏃‍♂️
 
Watanzania wangapi wanawapa mimba wasichana na wanawaterekeza? Kwa sababu ni wachina ndo walaumiwe? Walifanya kwa ihari, condom zipo na vidonge vya majira.
Pathetic..siwezi argue na low minded kama wewe. Very simple logic...kama watanzania wanauana kwa kupigana risasi hii haimpi uhalali mtu wa nje kuja kuwaua watanzania. Nimeamua kutumia mfano mkali kidogo ili uelewe. Waziri amesisitiza tu pamoja na mchango wao lazima waangalie utamaduni na mila zetu tulizojiwekea. Sasa nini shida hapo.
 
Tunapenda binadamu tuchanganyike lkn kutafuta wajukuu wenye vibamia ni kuwatafutia matatizo.
 
Pathetic..siwezi argue na low minded kama wewe. Very simple logic...kama watanzania wanauana kwa kupigana risasi hii haimpi uhalali mtu wa nje kuja kuwaua watanzania. Nimeamua kutumia mfano mkali kidogo ili uelewe. Waziri amesisitiza tu pamoja na mchango wao lazima waangalie utamaduni na mila zetu tulizojiwekea. Sasa nini shida hapo.
I may be low minded person but someone with common sense. You can not compare murder with sex! Is there any case of rape there? Usinijibu ukapoteza muda wako.
 
I may be low minded person but someone with common sense. You can not compare murder with sex! Is there any case of rape there? Usinijibu ukapoteza muda wako.
sikutaka kukujibu ila nimeumia sana na uwezo wako wa kufikiri. Kama umeshindwa kuelewa maneno ya waziri basi mfano wangu huwezi elewa kabisa. Your literally an ignorant person and still you feel your smart.
 
Wanawake wa kitanzania watasema hawataki kuolewa na vibamia wanataka hela yao tu.


Ndukiiiii 🏃‍♂️🏃‍♂️🏃‍♂️
Watu mnajua mambo mengi sana aise; we ni ke au me? Nataka kujua hilo cause najiuliza, we umejuaje kama Wachina wana bamia au vibamia na anyway, sorry kwa kwenda mbali zaidi, umewajua Wachina wangapi hadi uka conclude kwamba wana vibamia!?
 
Dar es Salaam. Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji Joseph Kakunda amewataka raia wa China nchini wakitaka kuwa na uhusiano wa kimapenzi na wanawake wa Watanzania wafuate taratibu.

Kakunda ametoa kauli hiyo jana jioni Desemba 7, 2018 wakati akizindua kituo cha maonyesho ya bidhaa za Kichina kilichopo Keko jijini Dar es Salaam.

Amesema nafasi za uwekezaji Tanzania na kuwakaribisha Wachina kuwekeza, kuwataka pale wanapotaka wanawake wanapaswa kufuata sheria na taratibu na kuachana na tabia ya kusimama na mabinti vichochoroni na kuwaachia watoto.

“Huku kwetu huwa tunakwenda kwa wazazi kujitambulisha kwa kutoa posa na kuoa kwa sherehe kubwa na mdundiko unapigwa,” amesema Kakunda.

“Fuateni taratibu hizo acheni kusimama simama vichochoroni na wasichana wa watu, hii nchi ya amani mkifanya hivyo mnawakera wazazi wao.”

Kakunda amewataka Wachina hao kuendeleza urafiki wa nchi hizo mbili kwa kuishi kwa kufuata sheria na taratibu za nchi.

“Njooni muwekeze lakini dumisheni urafiki ulioanzishwa na waasisi wa nchi yetu na China kwa kufuata mila, tamaduni za nchi, mziheshimu.

Ameongeza, “Mkienda Arusha kuna Wamasai wana taratibu zao wakati mwingine wanavaa shuka pekee bila kitu kingine ndani msistuke ndiyo tamaduni zao, hivyo mnapaswa kuziheshimu.”

Wakati akizungumza alikuwa na mkalimani aliyekuwa akitafsiri kwa Kichina na kuwafanya raia wa nchi hiyo waliokuwa eneo hilo kuangua kicheko.

Chanzo: Mwananchi
Wachina ni washenzi kupitiliza hawana utu kama baadhi ya wahindi walivyo
 
Back
Top Bottom