Waziri ataka wapiga debe waondolewe Dar

Waziri ataka wapiga debe waondolewe Dar

Hata humu ndani kuna wapiga debe tena wanatukana zaidi ya wale wa Ubungo. Naomba admin wa jf tumia sheria Kwa wapiga debe wa matusi ndani ya jf
 
Chukua na wale wavivu wa kuongea Wapeleke maporini huko wakafyeke mashamba,
 
Hawa watu waondolewe haraka kwani wanachafua hali ya hewa na mazingira. Angalia vituo kama magomeni,tegeta,kawe,mombasa,tazara.buguruni
 
Mmmmh mkuu Mh Magu kasema wakamatwe wakalime, ndo twauliza wapi wataenda fanyia hicho kilimo, si dhambi tukijua

Mapenzi hayana samahani, Na mimi sita omba samahani:-
Unapajua matombo mkuu? Napendekeza kambi nyingi zijengwe huku na wawalete huku.....muda wote ardhi inamelemeta kwa kushiba virutubisho.....maji bado yanatiririka toka miliman.....waje matombooo....
Oyaaaa mwanangu hili shamba linaenda moro...moro...
Akishtuka kumbe yupo shamba
 
Hawa jamaa huwa wanaingiza zaid ya buku 10 kwa siku .. Mi naona watafutiwe utaratibu , sabab hii haitapunguza uhalifu , bali itaongeza mara dufu , awa jamaa wengi wao ni watu walioadhirika na unga / weed .. Serikali isikurupuke hapa , hawa watu sio wacheza pooltable , hii ni kazi yao , inayowaingizia kipato chao cha kila siku , though inawezekana kuwa ni kweli wanafanya uhalifu ,lakin lets admit , in the past few years vitendo vingi vya upakuaji vimepungua kwa asilimia kubwa sana , hata wezi kuchomwa moto siku Dar hatusikii sana . kuna uwezekano wa kuzika vijana wengi sana kama serikali itakurupuka na kuziba hata hii mianya michache wanaotumia hawa vijana kujipatia ulaji wao .
Upiga debe umepunguza Wezi ila umeongeza Vibaka na Wala unga.

Ubodaboda ndio at least umepunguza wezi na vibaka.
 
Watawasafirisha kwenda vijijini kwa gharama zipi na watakaa kwa nani? Watalima shamba la nani? Wengine wamezaliwa dar.
 
Unapajua matombo mkuu? Napendekeza kambi nyingi zijengwe huku na wawalete huku.....muda wote ardhi inamelemeta kwa kushiba virutubisho.....maji bado yanatiririka toka miliman.....waje matombooo....
Oyaaaa mwanangu hili shamba linaenda moro...moro...
Akishtuka kumbe yupo shamba
Matombo kilugha chetu ni tusi mkuu
 
mtajifunza kidogokidogo maana kila mkiambiwa ccm ni ileile hamsikii mnahaidiwa maisha bora mnakurupuka leo mmehaidiwa viwanda badala yake mnatakiwa muondolewe mjini mkalime, sasa jiulizeni hivyo viwanda nani anatakiwa kuajiriwa? mtadanganywa sana
 
Ni sahihi kuwaondoa ila wahakikishe wanaweka askari wa kutosha huko mitaani maana wakiondoka hao kwenye kupiga debe panya raod wtaongezeka sana
 
SIKU moja kupita baada ya Rais John Magufuli kuwaagiza wakuu wa mikoa wapya kuwakamata vijana wote ambao wanacheza (poolTable) nyakati za asubuhi,kwa madai kuwa wajiingize kwenye shughuli za ufanyaji kazi,

Naye,Waziri nchi ofisi ya Rais Tawala za mikoa na serikali za mtaa,George Simbachawane amemtaka mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda kuhakikisha anawaaondoa wapiga “debe” wote kwenye vituo vya mabasi kwa madai kuwa wanafanya vitendo vya kihalifu. Waziri Simbachawene ametoa agizo hilo leo Jijini Dar es Salaam,wakati wa semina kwa wakuu wa mikoa wote nchini ambao waliapishwa jana na Rais Magufuli,

Ambapo alitumia nafasi hiyo kwa kusema kazi ya kupiga debe sio rasmi na aina kipato kitachoweza kumkwamua kijana kuondokana na tatizo la umasikini,

“Yaani hata hapa Dar es salaam namuomba mkuu wa mkoa ahakikishe anawondoa hawa wapiga debe kwenye vituo vya mabasi kwani wamekuwa wakichangia kutokea kwa uharifu,kipato cha mpiga debe kwa siku hakiwezi kumkwamua kimaisha sana sana wanatumia nafasi hiyo kufanya uharifu wanatakiwa kuondolewa haraka waende kwenye kazi hata za kilimo”amesema Simbachawene.

Hata Hivyo Waziri Simbachane ametumia nafasi hiyo kuwataka wakuu wa mikoa kufanya kazi kwa ufasaha na kuwatumikia wananchi ikiwemo kutekeleza ilani ya chama cha Mapinduzi CCM.

Serikali ya Tanzania kwa kweli inaumiza matumbo sana, sasa kama wapiga debe waondoke serikali kwanza ilipaswa kutoa ajira kwa hawa vijana kwanini marufuku zimekuwa nyingi toke magufuli lakini bado hakujakuwa na tija ya maisha?

Serikali ikilala ikiamka ni marufuku au umefukuzwa kazi ivi mwananchi mmoja mmoja atafadika lini bei za chakula zimepanda maradufu kazi ndio imezidi kuwa ndoto kwa mtanzania
 
hivyo inaonesha anasema kitu anachokifaham kabisa. kama kasema hailipi na unasema aliwah kuwa mpiga debe basi ni wazi kuwa ana ushahidi na hiyo kazi kuwa hailipi. hongera sana waziri.

Wapiga debe sioni la maana walifanyalo zaidi ya kuwaibia abiria, kuharibu taratibu ktk maeneo hayo ikiwa ni pamoja kufanya usumbufu kwa abiria pamoja na wapita njia yaani saana ninaloliona kwa wapiga debe ni kufanya vituo vya mabasi kuwa sio sehemu ya kistaarabu ni sehemu ya kihunihuni tu maana hata maneno yasiyokuwa na staha kama matusi kwa asilimia kubwa yanatoka midomoni mwa Wapiga debe ni kero tupu.

Kwa kuwa mabasi NA daladala zinazo alama zenye kutambulisha ni wapi zinakoelekea je kulikuwa na sababu gani ya kupigiwa debe?na abiria kusukumwa huku na kule akinyang'anywa begi ama mfuko alioubeba kwamba 'njoo panda hii inawahi zaidi' na maneno mengine kama hayo wanakufanya ni mjinga hata huna uamuzi wala hujui uendako tena baya zaidi utapata ya kwamba yale mabasi ambayo huduma zake ni mbovu ama hafifu ndiyo yanayokuwa na wapiga debe wengi zaidi.makampuni ya usafiri yenye kutoa huduma bora na stahiki kwa wateja hawana wapiga debe na wala hawahitaji kuwa nao hii ni kwa wale wanaosafiri kwenda mbali(mikoani na mataifa ya nje).

Kwa daladala ni utaratibu ukiwekwa wapiga debe hawatahitajika .
Kwa
Mfano ingetakiwa kuwepo na vibao kwenye vituo kuonesha ITAKAPOSIMAMA BASI KWENY HIYO POINT ITAKUWA NI YA KWENDA WAPI NA KUPITIA NJIA ZIPI,NA TENA KUWEPO NA MUDA MAALUM WA KUSIMAMA KITUONI KUPAKIA NA KUSHUSHA ABIRIA. NAO ABIRIA WAKIFIKA KITUONI WAKATI WA KUPANDA KWENYE DALADALA WASIMAME KWA FOLENI ILI ALIYEWAHI WA KWANZA AWE NI WA KWANZA KUINGIA KWENYE BASI HII ITAKUWA NI USTAARABU WA KUTOSHA MNO KWANI HAKUTAKUWEPO NA VURUGU WALA NINI.HAYA PENGINE KWETU WATANZANIA YANAWEZA KUWA NI MAMBO MAGENI ILA KWA NCHI ZA WENZETU NI UTARATIBU WA KAWAIDA KABISA.

WAZIRI NAKUPA BIG UP KWA MAELEKEZO YAKO ILA PIA NAKUOMBA NA KUSHAURI USIISHIE HAPO NA ISIWE NI DAR PEKE YAKE KWANI HATA MIKOANI HUO USUMBUFU UPO PIA NAOMBA PIA UWAAGIGIZE IDARA ZINAZOHUSIKA KUSIMAMI NA KUWEKA UTARATIBU WA NAMNA GANI MABASI NA ABIRIA WAJIBANGE KUINGIA NA KUSHUKA KTK MABASI HAYO ILI KUONDOA KERO KWA UJUMLA.
 
Watengeneze viwanda watu wapate ajira kwanza hayo maigizo mengine baadaye
 
Hawa jamaa huwa wanaingiza zaid ya buku 10 kwa siku .. Mi naona watafutiwe utaratibu , sabab hii haitapunguza uhalifu , bali itaongeza mara dufu , awa jamaa wengi wao ni watu walioadhirika na unga / weed .. Serikali isikurupuke hapa , hawa watu sio wacheza pooltable , hii ni kazi yao , inayowaingizia kipato chao cha kila siku , though inawezekana kuwa ni kweli wanafanya uhalifu ,lakin lets admit , in the past few years vitendo vingi vya upakuaji vimepungua kwa asilimia kubwa sana , hata wezi kuchomwa moto siku Dar hatusikii sana . kuna uwezekano wa kuzika vijana wengi sana kama serikali itakurupuka na kuziba hata hii mianya michache wanaotumia hawa vijana kujipatia ulaji wao .
Nasubiri kuona hilo likitekelezwa uone robber zitakavyoongezeka mtaani,hapo teja kakosa pesa ya kete ukikoswa kabali watapita nyumba kwa nyumba kuiba hata malapa ,itafutwe njia sahihi ya kupunguza vijana kuingia kwenye madawa
 
Back
Top Bottom