Waziri ataka wapiga debe waondolewe Dar

Waziri ataka wapiga debe waondolewe Dar

Ukienda pale ubungo wanasumbia sana waondolewe bila kusahau hawa wezi waliopewa jina la polisi jamii hawa nao ni jipu
 
Kweli maskini akipata matako hulia mbwata tulikuwa nae huyu Dom stendi enzi hizo.. Haya tuache maidha yaendeleee
 
sipati picha hizo kabali na ngeta tutakazo pigwa mitaani.chezeya wapiga debe wewe.
ha ha ha ha! kuna vijana wapiga debe walikuwa wakipewa pakiti za viroba wakilewa utasikia ccm eyoooo! then hapa kazi tu! nahisi huu msemo hawakuuelewa SASA KAZI TU NA NI KAZI KWELI KWELI Sizonje oyeeeee!
 
Hata mimi huwa sioni umuhimu wa wapiga debe.
Mkuu ukiona tumbili mjini jua ana mwenyewe, mtazamo wa haraka utaona wapiga debe waliochoka kwa kutumia unga bangi na viroba lakini behind the scene sivyooo!,hao wanatumiwa tu lakini kuna wenyewe wanaomiliki hivyo vilinge na kila siku hupita vilingeni kukusanya mapato yao kila siku.
Ni jambo ambalo linakera mno kwa kuwa most of tanzanian wanajua kusoma na pia wanajua kutofautisha rangi za daladala lakini unashangaa kuna watu bado wanatufanya kama vipofu,mkuu narudia tena ukimwona ngedere mjini jua ana mwenyewe.
Tena wengine ni watu na nyadhifa xao jiulizeni hivi watu wanaosimamia usalama wa raia na mali zao hawalijui hili au? Jiulize kisha fanya tafiti utaona.
 
mhh nahisi wataamia mitaani sasa si kabali izo labda wawataftie kazi ya kufanya
 
Waondolewe tu vijana wana nguvu kazi yao kupiga kelele stendi tu
 
Tatizo siyo kuwaondoa bali waende wapi?
Sidhani kama wakazi wa Tandale wamemiss kabari za misumari mitaani kwao
 
huwezi kuishi kutegemea kutafuniwa kila kitu, wanaolima wametafutiwa na nani maeneo?
Mmmmh mkuu Mh Magu kasema wakamatwe wakalime, ndo twauliza wapi wataenda fanyia hicho kilimo, si dhambi tukijua

Mapenzi hayana samahani, Na mimi sita omba samahani:-
 
SIKU moja kupita baada ya Rais John Magufuli kuwaagiza wakuu wa mikoa wapya kuwakamata vijana wote ambao wanacheza (poolTable) nyakati za asubuhi,kwa madai kuwa wajiingize kwenye shughuli za ufanyaji kazi,

Naye,Waziri nchi ofisi ya Rais Tawala za mikoa na serikali za mtaa,George Simbachawane amemtaka mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda kuhakikisha anawaaondoa wapiga “debe” wote kwenye vituo vya mabasi kwa madai kuwa wanafanya vitendo vya kihalifu. Waziri Simbachawene ametoa agizo hilo leo Jijini Dar es Salaam,wakati wa semina kwa wakuu wa mikoa wote nchini ambao waliapishwa jana na Rais Magufuli,

Ambapo alitumia nafasi hiyo kwa kusema kazi ya kupiga debe sio rasmi na aina kipato kitachoweza kumkwamua kijana kuondokana na tatizo la umasikini,

“Yaani hata hapa Dar es salaam namuomba mkuu wa mkoa ahakikishe anawondoa hawa wapiga debe kwenye vituo vya mabasi kwani wamekuwa wakichangia kutokea kwa uharifu,kipato cha mpiga debe kwa siku hakiwezi kumkwamua kimaisha sana sana wanatumia nafasi hiyo kufanya uharifu wanatakiwa kuondolewa haraka waende kwenye kazi hata za kilimo”amesema Simbachawene.

Hata Hivyo Waziri Simbachane ametumia nafasi hiyo kuwataka wakuu wa mikoa kufanya kazi kwa ufasaha na kuwatumikia wananchi ikiwemo kutekeleza ilani ya chama cha Mapinduzi CCM.
Yeye alishakuwa kondakta kwa hiyo anaijua vema shughuli ya stendi. Je atawaweza mziki wa hao jamaa?
 
Back
Top Bottom