NANGERA ECHUNGUKE
Member
- Sep 26, 2013
- 33
- 10
Heshima kwenu wana JF
Hili ni jambo linaloweza kuwa la kuchekesha lakini ndipo CCM ilipotufikisha
Ndugu wadau siku chache zilizopita kulikuwa na shamra shamra,hoi hoi na nderemo hapa jimboni Mwanga kwa Profesa maghembe. Kulikuwa na tukio la ajabu kidogo kufanywa na kiongozi wa Kitaifa hasa level ya Uwaziri
Naam! ni kuzindua choo cha wanafunzi wa Shule ya Msingi Mwanga ambapo Mheshimiwa Wazir Profesa Maghembe ndie alikuwa mgeni Rasmi! Gharama za ujenzi wa choo hicho zimegharamikiwa kwa kiasi kikubwa na wananchi na wafadhili wa Ahsante Tours ya Moshi. Mfuko wa jimbo ulichangia Tsh 600,000/= kwenye ujenzi huo ambao umegharimu jumla ya fedha za kitanzani tsh 9,000,000/=
Kioja ni kuwa choo hicho ni cha kawaida sana na wala hapakuhitajika sherehe ya gharama kubwa kukizindua huku shule hiyo ikiwa haina vitabu vya kutosha , walimu kununua chaki kwa pesa zao wenyewe.
All in All Cheo cha Uwaziri ni Cheo kikubwa sana kufanya shughuli hiyo ya Uzinduzi wa Choo. Hii ni kudhalilisha kabisa serikali kwani fedha/ Muda huo uliotumika kwa watumishi na watendaji wa Halmashauri plus mafuta ya magari vingetosha kabisa kufanya kitu kingine cha maana kama kuwanunulia watoto hao vitabu na mahitaji mengine ya kuendesha shule.
Hiyo ndio serikali ya CCM ya miaka hii sasa sijui tukiwaongezea 2015 itakuwaje! maana kwa upuuzi huu mdogo tu sijui
Source: mimi mwenyewe na kamera niliopigia picha imechukuliwa na wasaidizi wa Waziri!
Hili ni jambo linaloweza kuwa la kuchekesha lakini ndipo CCM ilipotufikisha
Ndugu wadau siku chache zilizopita kulikuwa na shamra shamra,hoi hoi na nderemo hapa jimboni Mwanga kwa Profesa maghembe. Kulikuwa na tukio la ajabu kidogo kufanywa na kiongozi wa Kitaifa hasa level ya Uwaziri
Naam! ni kuzindua choo cha wanafunzi wa Shule ya Msingi Mwanga ambapo Mheshimiwa Wazir Profesa Maghembe ndie alikuwa mgeni Rasmi! Gharama za ujenzi wa choo hicho zimegharamikiwa kwa kiasi kikubwa na wananchi na wafadhili wa Ahsante Tours ya Moshi. Mfuko wa jimbo ulichangia Tsh 600,000/= kwenye ujenzi huo ambao umegharimu jumla ya fedha za kitanzani tsh 9,000,000/=
Kioja ni kuwa choo hicho ni cha kawaida sana na wala hapakuhitajika sherehe ya gharama kubwa kukizindua huku shule hiyo ikiwa haina vitabu vya kutosha , walimu kununua chaki kwa pesa zao wenyewe.
All in All Cheo cha Uwaziri ni Cheo kikubwa sana kufanya shughuli hiyo ya Uzinduzi wa Choo. Hii ni kudhalilisha kabisa serikali kwani fedha/ Muda huo uliotumika kwa watumishi na watendaji wa Halmashauri plus mafuta ya magari vingetosha kabisa kufanya kitu kingine cha maana kama kuwanunulia watoto hao vitabu na mahitaji mengine ya kuendesha shule.
Hiyo ndio serikali ya CCM ya miaka hii sasa sijui tukiwaongezea 2015 itakuwaje! maana kwa upuuzi huu mdogo tu sijui
Source: mimi mwenyewe na kamera niliopigia picha imechukuliwa na wasaidizi wa Waziri!