Waziri analeta bajeti inayomkamua mlalahoi huku amekunja ndita, zikiliwa hawajibiki wala hatimuliwi. Hili lifike mwisho

Pslmp

JF-Expert Member
Mar 18, 2021
1,622
2,459
Inauma sana!

Kulipa Kodi ni wajibu wa kila mtu aliyeko ktk dunia hii

Wananchi hasa walalahoi wamekuwa kama ni shamba la Bibi, walaji wa mavuno hayo ni hao wanaowapangia wananchi kulipa Kodi za ajabu ajabu,

Bajeti hii, inapokuja na Kodi ya nyumba kuingizwa kwenye mfumo wa Luku, aliyelengwa hapo si mwingine, ni mlala hoi huyuhyu anayelipa Kodi Kwa mijeredi ya police, wenye nyumba na matajiri wakiendelea kuneemeka.

Wananchi walalahoi hukamuliwa kama sweta, mbali na kuendelea kuwa waaminifu katika kulipa Kodi, ajabu ni pale Kodi nyingi zinapoishia mikononi mwa waliojuu, wenye kuwapangia maisha Yao yaweje

Kodi nyingi zinazokuwa zinapangwa, utadhani mtu huwa anakelekwa Sana na uwepo wa watu wa chini, na pengine huwa wanajiambia hawa watu ni wa kukamua haswaa, na kwa sababu hiyo, wananchi wa kawaida ndio haswaa, hufunga mikanda Kwa kukamliwa ili mambo ya nchi Yao yaende, ni Jambo jema.

Kinachouma sana ni pale walipa kodi wamefanya wajibu wao, halafu wasimamizi wa fedha hizo, wanazigawana ju kwa juu.

Hivi majuzi, kumetokea uotevu wa mabilioni ya fedha katika wizara ya fedha, Fedha hizi, hakuna aliyewajibika, na fedha zimepotea

Inauma sana pale mlalahoi anapotoa kodi yake akiamini huduma za kijamii atazipata, kumbe kuna genge la watu wachache waliojifanya mchwa, wakula pesa za walala Hoi na hawawajibishwi.

Kitendo cha kupotea mabilioni ya fedha katika wizara husika, waziri kuendelea kuwepo, ni kuruhusu wanyonge na walipa kodi waendelee kuishi maisha magumu katika hali ya kukosa miundombinu ya uhakika na kukosa huduma mhimu, mbaya zaidi, kitendo hiki kinaweza kutafsiliwa kwamba, ni kuendelea kuwanyonga walala Hoi walipa kodi na wao kufurahia kugawana jasho lao bila ya kuchukuliwa hatua.

Ni vyema sasa, kila mtu anapobainika amekula fedha za walipa kodi, awajibishwe kama mlalahoi anapofuatiliwa kiasi cha kufikishwa police akidaiwa Kodi ya Tsh 20000.

Inakuwaje kwa hao wanaoiba mabilioni ya fedha wakiachwa bila kuchukuliwa hatua, upotevu wa mabilioni ya juzi, waziri na katibu wake wanafanya nini ofisini?

Wananchi, hawajawahi kukataa kulipa Kodi kwa kuwa Kodi ndiyo inayowasogezea wananchi huduma

Tuwajibishane bila kuoneana aibu.
 
Kama wew ni Mtanzania inatakiwa ulipe kodi kwa ajiili ya nchi yako sio kupenda kubebwa kila siku msilipe kodi huku mnajipa majina ya huruma Kama wanyonge mara walalahoi nk.

Hakuna aliezaliwa mnyonge Tz hii kila mtu apambane alipe kodi tuijenge hii nchi pamoja kwa umoja wetu sio kuwaachia watu waliotafuta pesa wajenge nchi huku sisi wengine tukijificha kwenye kivuli cha umaskin

LIPA KODI KWA MAENDELEO YA NCHI YAKO SIO KULIA LIA OVYO

Kama hutaki hama nchi tu
 
Ndiyo mkuu, Kodi inalipwa, kinachoumiza, Kodi zikilipwa, zinaenda kugawanwa ju Kwa ju, wanazigawana hawachukuliwi hatua, inaumiza sana
 
Ndiyo mkuu, Kodi inalipwa, kinachoumiza, Kodi zikilipwa, zinaenda kugawanwa ju Kwa ju, wanazigawana hawachukuliwi hatua, inaumiza sana

Basi usiandike kulalamika kodi lalamika ufisadi uliotukuka kwenye nchi yetu
 
Hata biblia imesema aliye na kitu atapewa zaidi; asiye na kitu, hata kile alicho nacho kitachukuliwa....acheni neno litimie🤸🤣🐒
 
Hii kodi ya kukatana hela kwenye line za simu kila siku hii, itakuja kufutwa tu kabla ya 2025! CCM ni mabingwa wa kutengeneza matatizo halafu mwisho wa siku, wao wenyewe wanakuja kujigeuza kuwa wakombozi!

Yaani hawatosheki tu kuongeza kodi kwenye miamala! Wanahamia mpaka kwenye line za simu! Bora hata kodi zenyewe zingekuwa zinatumika kwenye matumizi sahihi basi! Karibia robo au nusu ya hayo mabilioni yote yatakayo kuja kukusanywa, usikute yakaishia tu mikononi mwa wapigaji wachache.
 
Ndiyo mkuu, Kodi inalipwa, kinachoumiza, Kodi zikilipwa, zinaenda kugawanwa ju Kwa ju, wanazigawana hawachukuliwi hatua, inaumiza sana
Acha kuishi kwa kukariri. Kodi zinasomesha wanafunzi wa vyuo, zinanunua mashine ghali za mahospitalini. Zinanunua ndege, zinatengeneza meli mpya maziwani.

Kodi zinafanya mengi sana tatizo letu watanzania ni mafundi wa kulalamika na kunyooshea watu vidole. Tunapenda sana kutafuta mchawi kumbe uchawi ni akili zetu zisizojua maendeleo yana gharama zipi na yanatafutwa vipi.

Ulaya, Marekani na kwingineko asiyelipa kodi jela inamhusu. Tubadilike hii ni 2021 miaka 60 tangu tuanze kujitawala.
 
Yeye ndiyo chanzo cha yote haya.
Najua .KE. Sasa Ina remotiwa na kjk kjkkk. Sasa hiv ni mwendo wa
FB_IMG_1616683051842.jpg
 
Hii kodi ya kukatana hela kwenye line za simu kila siku hii, itakuja kufutwa tu kabla ya 2025! Ccm ni mabingwa wa kutengeneza matatizo halafu mwisho wa siku, wao wenyewe wanakuja kujigeuza kuwa wakombozi!...
Umeongea ukweli tupu mkuu
 
Hii kodi ya kukatana hela kwenye line za simu kila siku hii, itakuja kufutwa tu kabla ya 2025! Ccm ni mabingwa wa kutengeneza matatizo halafu mwisho wa siku, wao wenyewe wanakuja kujigeuza kuwa wakombozi!..
Kweli shida iko hapo, wangekuwa wanakata hela alaf tunaona mabadiliko mitaani kwetu mbona poa. Nani atagoma kukatwa hela ihali anaona barabara safi kila mtaa.
 
Kweli shida iko hapo, wangekuwa wanakata hela alaf tunaona mabadiliko mitaani kwetu mbona poa. Nani atagoma kukatwa hela ihali anaona barabara safi kila mtaa.
Shida inaanzia pale kodi imelipwa, halafu wao huko juu wanashindwa kuisimamia inagawanwa na wasiowaadirifu, halafu, hakuna anayewajibishwa na kuwajibika, matokeo yake walipa kodi wanapewa mzigo mzito
 
Hii kodi ya kukatana hela kwenye line za simu kila siku hii, itakuja kufutwa tu kabla ya 2025! CCM ni mabingwa wa kutengeneza matatizo halafu mwisho wa siku, wao wenyewe wanakuja kujigeuza kuwa wakombozi!...
Kwani wabunge wawakilishi wa wananchi wanasemaje?
 
Zamu ya wanyonge kuishi kishetani.Waziri kipato chake ni kikubwa akichukuliwa watz wote vipato sawa na yeye
 
Back
Top Bottom