GY
JF-Expert Member
- Nov 2, 2009
- 1,279
- 126
Ufisadi umejikita zaidi kwenye matumizi mabaya ya rasilimali za umma, na kila mwananchi anajua ubaya wa jambo hili na hatari yake kwa taifa. Tumeshasema sana na tuendelee kubanana ili mapambano haya yasiwe ni nguvu za soda.
Lakini pia tuanze kungalia muelekeo wa uchumi wetu ukoje, focus ikiwa hasa kuhusu sera na mipango mbalimbali ya kitaifa.
Jana waziri wa viwanda na biashara Bi Mary Nagu amekiri kuwa nyuzi zinazotumika katika kiwanda cha nguo cha URAFIKI zinatoka nchini China..(TBC 1)
Najaribu kuitazama hii issue katika mapana yake kidogo, mfano
Misaada ya wachina inavyoambatana na makampuni toka kwao, wakiwemo mpaka vibarua wa ujenzi wanaobaka dada zetu na kuzaa nao bila serikali kuwa na uwezo wa kufanya lolote
Misaada toka china inavyoambatana na sera za kuruhusu raia wa nchi iyo waje watakavyo hata kama wanakuja kuwa wamachinga kariakoo, au kufungua vimigahawa vya mama ntilie. Sijasema hapo kuhusu kuruhusiwa kwa bidhaa sub-standard kutoka nchi hiyo
Misaada kutoka Japan inavyoambatana na sera ya ununuzi wa magari ya kifahari na magari chakavu toka nchini humo
Mifano iko mingi sana, lakini kila rafiki na mwekezaje ajae hapa nchini anaonekana kuwa anayo ajenda yake
Uwekezaji usio tija toka Afrika kusini na namna nchi iyo inavyoleta malighafi ambazo kimsingi hata hapa zinapatikana kirahisi mno. Ebu tazama shairi, madawa, na items mbalimbali zinazotumika katika kiwanda cha bia cha TBL zinatoka hapa nchini au South Africa
Ushirikiano na India na namna tunavyoletewa vitu vya hovyo kama bajaji ambazo si tu kuwa zinadhoofisha sekta ya umma ya usafiri (public transport system), lakini pia ni janga litakalokuja kuturipukia muda si mrefu
Kama alivyouliza Makwaia wa Kuhenga jana katika kipindi chake "Je tutafika" Iko wapi focus ya uchumi ya nchi hii??
Sijasema athari za ushiriano wetu na mataifa makubwa ya ulaya na marekani, maana hao tumewakaribisha mpaka chumbani, wanatujua kuliko wandani wetu
Swali langu ni kuwa ivi bado kuna nchi kweli hapa, au mkusanyiko wa viumbe fulani mahali fulani, vikiwa havina mbele wala nyuma
AM JUST CURIOUS!
Lakini pia tuanze kungalia muelekeo wa uchumi wetu ukoje, focus ikiwa hasa kuhusu sera na mipango mbalimbali ya kitaifa.
Jana waziri wa viwanda na biashara Bi Mary Nagu amekiri kuwa nyuzi zinazotumika katika kiwanda cha nguo cha URAFIKI zinatoka nchini China..(TBC 1)
Najaribu kuitazama hii issue katika mapana yake kidogo, mfano
Misaada ya wachina inavyoambatana na makampuni toka kwao, wakiwemo mpaka vibarua wa ujenzi wanaobaka dada zetu na kuzaa nao bila serikali kuwa na uwezo wa kufanya lolote
Misaada toka china inavyoambatana na sera za kuruhusu raia wa nchi iyo waje watakavyo hata kama wanakuja kuwa wamachinga kariakoo, au kufungua vimigahawa vya mama ntilie. Sijasema hapo kuhusu kuruhusiwa kwa bidhaa sub-standard kutoka nchi hiyo
Misaada kutoka Japan inavyoambatana na sera ya ununuzi wa magari ya kifahari na magari chakavu toka nchini humo
Mifano iko mingi sana, lakini kila rafiki na mwekezaje ajae hapa nchini anaonekana kuwa anayo ajenda yake
Uwekezaji usio tija toka Afrika kusini na namna nchi iyo inavyoleta malighafi ambazo kimsingi hata hapa zinapatikana kirahisi mno. Ebu tazama shairi, madawa, na items mbalimbali zinazotumika katika kiwanda cha bia cha TBL zinatoka hapa nchini au South Africa
Ushirikiano na India na namna tunavyoletewa vitu vya hovyo kama bajaji ambazo si tu kuwa zinadhoofisha sekta ya umma ya usafiri (public transport system), lakini pia ni janga litakalokuja kuturipukia muda si mrefu
Kama alivyouliza Makwaia wa Kuhenga jana katika kipindi chake "Je tutafika" Iko wapi focus ya uchumi ya nchi hii??
Sijasema athari za ushiriano wetu na mataifa makubwa ya ulaya na marekani, maana hao tumewakaribisha mpaka chumbani, wanatujua kuliko wandani wetu
Swali langu ni kuwa ivi bado kuna nchi kweli hapa, au mkusanyiko wa viumbe fulani mahali fulani, vikiwa havina mbele wala nyuma
AM JUST CURIOUS!