Waziri aagiza mzee wa miaka 98 kulipwa mil 500 na waliompora ardhi

elivina shambuni

JF-Expert Member
May 31, 2018
461
295
1567082981796.png



WAZIRI wa Ardhi William Lukuvi ameagiza Wakazi wa Sinoni mkoani Arusha kumlipa Bibi Nasi Muruo (98) kiasi cha Sh. milioni 519 kwa kosa la kuvamia eneo lake na kujenga baada ya kushinda kesi ya kudhulumiwa ardhi yake tangu mwaka 1979 na kuzungushwa.

atimaye kaya 109 zimetakiwa kumlipa fidia jumla ya Sh519.3 milioni kikongwe Nasi Muruo(98) mkazi wa eneo la Sinoni, katika jiji la Arusha, baada ya kurejeshwa ardhi yake aliyokuwa anaidai kwa miaka 42 .Waziri Lukuvi ametangaza uamuzi huo wakati akizungumza na kaya 109 zilizovamia eneo la bibi huyo katika viwanja vya shule ya msingi Sinoni.

Amesema kila kaya italipa kiasi cha Sh20,000 kwa mita moja ya mraba katika eneo la bibi huyo, lakini italipia pia fedha za kupimwa ardhi ili kupewa hati ndani ya miezi mitatu "Kila manachi aliyopo hapa ili zoezi la uvamizi na majina yenu ya uvamizi yaweze kubadilika na muitwe wamiliki ni lazima utaratibu ufuatwe ili nikija siku nyingine hapa nizungumze na wamiliki wa ardhi sio wavamizi wa ardhi kwa sababu mtakuwa na hati zenu," amesema Lukuvi na kuongeza kuwa; "Sasa hili zoezi la kubadilisha majina yenu kutoka wavamizi kuwa wamiliki ni lazima utaratibu ufanyike na muwe wazalendo mlipe kodi ya kila mwaka lakini lazima huyu mama alipwe na kiwango atakacholipwa mtamchangia wote nyinyi, haipungui milioni 500 kwa uchache kwa sababu tumepunguza tumewapaneni kiwango cha chini kabisa cha shilingi elfu 20,000 mtachanga na kuingiza kwenye akaunti yake," amesema Kikongwe huyu alirejeshewa ardhi yake, Julai 8, 2019 na Waziri Lukuvi, kutokana na maelekezo ya Rais John Magufuli wa Tanzania, alipomtaka kushughulikia mgogoro huo, hasa baada ya kuripotiwa malalamiko ya Kikongwe huyo, kunayanyang’anywa ardhi yake tangu mwaka 1977 na ndugu wa ukoo wao, Edward Lenjeshi
 
..mama alishinda kesi MAHAKAMANI.

..pia alitetewa na wanasheria toka kituo cha kutetea haki za binadamu.

..kwa hiyo uamuzi wa waziri ni wa kukazia tu hukumu ya mahakama.
 
Mangapi yameamuliwa na mahakama hayajatekelezwa?
Sifa na pongezi ni uthubutu wa waziri,ni makini na muwajibikaji
..mama alishinda kesi MAHAKAMANI.

..pia alitetewa na wanasheria toka kituo cha kutetea haki za binadamu.

..kwa hiyo uamuzi wa waziri ni wa kukazia tu hukumu ya mahakama.
 
Kwa Umri wa huyo Mama, Shida alizopitia na Mazingira aliyomo kama hatopatiwa Kwanza Msaada wa Kisaikolojia Siku akipewa rasmi hizo Hela au akaambiwa kuwa ameshaingiziwa katika Akaunti yake anaweza Akafa na wala asizifaidi na zikaishia tu Kuliwa na wale ambao hawana Uchungu nae wowote ule.
 
Mangapi yameamuliwa na mahakama hayajatekelezwa?
Sifa na pongezi ni uthubutu wa waziri,ni makini na muwajibikaji

..Tumpongeze Bibi aliyefuatilia bila kuchoka.

..Tuwapongeze mawakili wanasheria kwa utetezi wao.

..Tuipongeze mahakama kwa kutenda haki.

..Tumpongeze waziri kwa kutekeleza maamuzi ya mahakama.
 
Habari nzuri
Huyo ndugu aliyetajwa.. pesa alizokuwa anaonga zimeenda bureeeeeee
 
Kwenye sheria kuna msemo "justice delayed is justice denied".
Hata mbowe atalipwa fidia kubomolewa bilcan na Shamba lake lililoharibiwa na byakana Kwa maagizo waliobomolewa Nyumba zao Kwa uonevu nao wawe na subiria mbeleni watalipwa serikali iyayo ni sikivu
 
..Tumpongeze Bibi aliyefuatilia bila kuchoka.

..Tuwapongeze mawakili wanasheria kwa utetezi wao.

..Tuipongeze mahakama kwa kutenda haki.

..Tumpongeze waziri kwa kutekeleza maamuzi ya mahakama.
Tatizo ni kwamba huenda huyo bibi akaondoka bila kuiona hata senti moja!
 
Back
Top Bottom