figganigga
JF-Expert Member
- Oct 17, 2010
- 25,492
- 54,895
Kahama. Siku chache baada ya mbunge wa zamani wa Kahama, James Lembeli kuteuliwa kuwa mwenyekiti mwenza wa Taasisi ya Kimataifa ya Uhifadhi na Mazingira, wazee wamempongeza, wakisema ni heshima kwa Taifa.
Hivi karibuni, Lembeli aliteuliwa kuwa mwenyekiti wa taasisi ya Jane Goodall yenye makao yake makuu katika Jimbo la Virginia nchini Marekani. Taasisi hiyo hufanya kazi zake katika nchi 140 duniani.
Lembeli pia ni mjumbe wa bodi ya shirika jingine la hifadhi la African Parks Network lenye makao yake makuu jijini Johanessburg, Afrika Kusini.
Katika hafla ya kumpongeza Lembeli juzi, mwenyekiti wa Umoja wa Wazee wa Kahama (Uwaka), Nathan Homgan alisema wameamua kutumia fursa hiyo kutambua heshima yake kimataifa.
Umaarufu wa Lembeli uliongezeka wakati alipopinga Operesheni Tokomeza iliyotekelezwa vibaya kwa kukiuka haki za binadamu.
Chanzo: Mwananchi
Hivi karibuni, Lembeli aliteuliwa kuwa mwenyekiti wa taasisi ya Jane Goodall yenye makao yake makuu katika Jimbo la Virginia nchini Marekani. Taasisi hiyo hufanya kazi zake katika nchi 140 duniani.
Lembeli pia ni mjumbe wa bodi ya shirika jingine la hifadhi la African Parks Network lenye makao yake makuu jijini Johanessburg, Afrika Kusini.
Katika hafla ya kumpongeza Lembeli juzi, mwenyekiti wa Umoja wa Wazee wa Kahama (Uwaka), Nathan Homgan alisema wameamua kutumia fursa hiyo kutambua heshima yake kimataifa.
Umaarufu wa Lembeli uliongezeka wakati alipopinga Operesheni Tokomeza iliyotekelezwa vibaya kwa kukiuka haki za binadamu.
Chanzo: Mwananchi