Just Pray
JF-Expert Member
- Nov 7, 2023
- 2,142
- 4,779
Mwenyekiti wa Wazee wa Mkoa wa Dar Es Salaam, Salum Matimbwa amesema Wazee wa mkoa huo wanaungana na Watanzania lkumpongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa ushindi wa kishindo alioupata katika uchaguzi wa Oktoba 29, 2025.
Mzee Matimbwa akizungumza katika Mkutano wa Wazee hao na Rais Samia amesema ushindi huo ni ishara ya imani kubwa ya Watanzania kwa Dkt. Samia, kwamba ni kiongozi mahiri na makini
Hata hivyo, Mzee Matimbwa ameeleza kuwa wanatambua kampeni zilifanyika kwa utulivu mkubwa na hata uchaguzi mkuu mpaka pale vurugu zilipojitokeza.
Ameongeza kuwa kadhia hiyo imewafadhaisha kwa sababu vifo vimetokea, mali zimeharibiwa, miundombinu imeathiriwa n.k.
Mzee Matimbwa akizungumza katika Mkutano wa Wazee hao na Rais Samia amesema ushindi huo ni ishara ya imani kubwa ya Watanzania kwa Dkt. Samia, kwamba ni kiongozi mahiri na makini
Hata hivyo, Mzee Matimbwa ameeleza kuwa wanatambua kampeni zilifanyika kwa utulivu mkubwa na hata uchaguzi mkuu mpaka pale vurugu zilipojitokeza.
Ameongeza kuwa kadhia hiyo imewafadhaisha kwa sababu vifo vimetokea, mali zimeharibiwa, miundombinu imeathiriwa n.k.