Wazee wa BANDARI: MWAKYEMBE na aje...

Maofisa mbalimbali wa Mamlaka ya Bandari Tanzania wamepania kumwonyesha Waziri Mteule wa Uchukuzi,Dr.(PhD) Harrison Mwakyembe,kilichowashinda watangulizi wake: Omari Nundu na Athuman Mfutakamba.Wakiongea nami jana katika nyakati tofauti juu ya vipi watampokea Waziri 'mpya',wazee hao wa Bndari walitamba kuwa hawataacha kilichozoeleka Bandarini hapo.'Tunajua Rais anatupima ubavu kwa kutuletea Mwakyembe.Na aje tumwonyeshe mfupa mgumu hapa Bandarini.Hatutaacha mazoea yetu'. alitamba mmoja wa wazee wa Bandari. Mwakyembe ataisafisha Bandari yetu?

Wee kweli huzijui soga za wakulu wa bandari, jamaa wanaongea haoo utaogopa...:hat:
 
...Habari za kupika na za uoga-oga utazijua tuu.

Ndo yale ya zamani...nishike ntaua jamani, ntaua kumbe mtu muoga na karibu anajinyea. Magangwe tulikuwa tukisikia mtu kama huyo, tunamuacha hakuna kumshika na mara zikianza anapigwa kichwa, na then kata funua unashangaa jamaa anakwenda chini kirahisi kama Maige na Ngeleja !! Hawa kama ni kweli na mabusha yao, Harrison atawakata buti mpaka wakimbilie kwa kijana wao wa kucheka-cheka ili awahutubie tena baada ya ubwabwa pale Diamond :)

Pale kuna mizizi ya akina Kondo, Idd Simba, Karamagi na wale wa kuishi kimjini-jini !!
 
Wanapima pasipo pimika. akiwashindwa MWAKYEMBE basi wajiandae kuondoka kwa nguvu ya umma baada ya uchaguzi wa 2015 ambapo CDM itaingia madarakani.
 
Wamesisitiza kulinda mazoea yao. Nilipowauliza ni yapi,mmoja wao akanijibu:'utamuuliza Mwakyembe'. Yaani...
 
Weeeee . Mwakyembe kashindikana .kikwete na ccm hawana hamu tena nae. Walijua wanemmaliza. Sasa wamewasakizia wazee wa bandari walioshindikana. Mwakyembe anamwamini yesu
 
Mamlaka ya bandari ya mkusanyiko wa wazee fulani waswahili swahili kiasi kwamba wamekuwa ni watu wa kuendekeza ushirikina tu na ndio maana wengi wao licha ya kufanya kazi bandarini miaka mingi na kipato kizuri lakini wako duni kabisa. So hilo la kumuonyesha Mwakyembe mfupa uliowashinda watangulizi wake ndio muendelezo wa ule ujinga wao...lakini tatizo ni kuwalea na kuwaogopa ndiko kunakowapata kiburi. Kuna jamaa yangu ndugu yake alipata kazi ya udereve pale temporary kwa muda wa miezi miwili tu jamaa aliambiwa kuwa kuendesha gari iliyokuwa ikiendeshwa na yule mzee inabidi awe mgumu jamaa hakujali lakini siku ya 5 tu akaomba kuacha kazi......:eek2:

Mkuu unayosema ni kweli, watu hao wanaweza kumchanganya sana Dr. Mwakyembe; mimi naona cha kufanya kwanza nikusafisha wizara nzima, makatibu wakuu wabadilishwe na watendaji wakuu, mkuu wa TPA apewe kazi nyingine nje ya Wizara ya uchukuzi-vile vile panapashwa kuwa na mabadiliko makubwa kwenye kitengo cha bandari zote. Akisha maliza zoezi hilo atafute taharifa zote ambazo ziliwahi kuandikwa na tume teule kama ziliwahi kuwepo azifanyie kazi mapendekezo yaliyo wahi kutolewa na TUME hizo, zoezi hili lifanywe kwenye shirika la ndege ATC na Reli hasa hasa ya TAZARA.
 
Hapa inawezekana kuna mtu mkubwa anaogopeka hapa..ni nani? na kuna kipindi mkulu alisema kuwa anawajua watu wote wa bandari pale na matendo yao...

Mkuu hakuna statement inayoudhi kama hiyo hasa toka kwa mkuu! Anawajua wauza unga wote, anawajua majambazi sugu, anawajua wezi wa halmashauri, anawajua walaji wa bandari, lakini hajui kwanini Tanzania ni maskini! Lol, Tanzania ina kila sababu ya kuingia ktk historia kwa kuwa na raisi wa kipekee
 
Mkuu hakuna statement inayoudhi kama hiyo hasa toka kwa mkuu! Anawajua wauza unga wote, anawajua majambazi sugu, anawajua wezi wa halmashauri, anawajua walaji wa bandari, lakini hajui kwanini Tanzania ni maskini! Lol, Tanzania ina kila sababu ya kuingia ktk historia kwa kuwa na raisi wa kipekee
Kweli tz tuna hali mbaya! Presidaa anaelewa kila kitu ila haelewi afanye nini! Thats why huwa anaenda abroad maana hawezi fanya lolote zaidi ya unafiki hilo ni pro yake
 
Hawa Wazee wote fukuza fasta.... Wanacheza na Mwakyembe kachungulia kifo karudi... ngoja awalipizie hasira zake waone moto...
 
hao watu wa bandari wajue mwakyembe yuko na Mungu..walimpa sumu na bado yuko mzima mwili ushakomaa sijui huko bandarini watamtosa kwenye maji??
 
Mwakyembe is unbeatable, he is going to trigger and unleash success in that part of our economy.
 
hivi bandari imeshindwa kuwa na ofisi moja tu unapeleka docs zako unapewa bei ya kulipa kiasi gani unalipa siku hiyo hiyo then wapangiwa siku ya kuchukua mzigo wako. Hii ingesaidia watu kutopoteza mua wa kufuatilia
 
Back
Top Bottom