Wazee: Dr. Magufuli ni chaguo la Mungu

Wazee: Dr. Magufuli ni chaguo la Mungu

Status
Not open for further replies.
Watu waache kuchezea jina la Mungu kienyeji.
 
Hao watakuwa wazee Wa ccm ambao wametoka mbinguni ndiko walikoambiwa Na Mungu kuwa magufuni ni chaguo lake Jamani Mungu hana mtu mwizi Mwuuza Mali za watanzania mpaka kwa wahindi
 
Tanzania ni nchi pekee ambapo watu wanaotegemewa wawe mwanga na viongozi wa jamii wamegeuka kuwa wapotoshaji wakubwa na hii yote ni kulinda matumbo yao

Nimewapuuza sana hao wazee!!
 
DSC00038.jpg

Kuna miungu wengi labda mungu wa jua lakini si huyu ninaemwamini mimi Muumba wa Mbingu na Dunia na vyote vilivyomo.
 
Hawa wazee ni wanafiki sana siyo wa kuamini tena hata JK tuliambiwa chaguo la Mungu lakini tumeona tulipofikia kwa sasa .
maisha bora kwa kila mwana ccm na maisha magumu kwa kila mtanzania asiyekuwa mwana ccm.
 
Watu wazima wafikiapo uzeeni huwa wengi wao huwa wanazeeka vibaya. Mungu si mjomba wenu enyi wazee!
 
Neno mgombea wa ccm ni chaguo la Mungu tuliambiwa mwaka 1995 wakati Kikwete anagombea. Matokeo yake kaiacha nchi katika hali isiyokubalika. Mungu anapenda watanzania wawe maskini? Haikubaliki hii dhana, tunapaswa kuhoji. Mgombea nani ni chaguo la shetani? Kikwete muogope Mungu.
 
Magufuli siyo chaguo la Mungu. Ni chaguo la mfumo wa chama cha kijani
 
Labda mungu wa mlima kolelo au mkundi au Mungy wa JF
Neno mgombea wa ccm ni chaguo la Mungu tuliambiwa mwaka 1995 wakati Kikwete anagombea. Matokeo yake kaiacha nchi katika hali isiyokubalika. Mungu anapenda watanzania wawe maskini? Haikubaliki hii dhana, tunapaswa kuhoji. Mgombea nani ni chaguo la shetani? Kikwete muogope Mungu.
 
Kitendo cha Chadema kupigwa upofu kumuondoa Dr Slaa na kumuweka fisadi mkuu ni wazi kabisa kuwa Magufuli ni chaguo la mbingu
 
Kuna kipindi shetani anajigeuza na kuwa kama Mungu, huyo ndo anawazuga
 
Hivi ndio vile vichekesho tulivyoambiwa...eti Magufuli ni chaguo la mungu, Hao wazee vipi, walikutana na mungu lini akawaambia? Si tuliambiwa pia Kikwete ni chaguo la mungu? Matokeo yake si ndio haya, tabu tupu, MAISHA BORA KWA VIONGOZI WA CCM NA FAMILIA ZAO.
 
Hivi huyu 'Mungu' aliyemuongelea ndio pia aliyesemwa na Father Kilaini!?
Sasa kama ndiye huyo huyo basi Dr. Magu atakuwa na wakati mgumu kuwashawishi wananchi wamkubali kwa sababu 'chaguo' la kwanza hawajalipenda kivile!
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom