Wazazi adhabu hizi hazifai kwa watoto.

tremendous

JF-Expert Member
Aug 12, 2016
3,237
5,307
Habari wana JF
Kama tujuavyo mtoto huzaliwa akiwa hajui chochote ila anajifunza kadri anavyo interact ktk mazingira yake.
Katika kujifunza mtoto huchukua mazuri na mabaya kutoka ktk jamii inayomzunguka kwahiyo ni kazi kwa mzazi kuhakikisha mtoto anakuwa na maadili yenye kukubalika ktk jamii.

Ktk kuwaadhibu watoto wao baadhi ya wazazi hutoa adhabu ambazo hazilengi kuwafunza watoto bali kukomoa kama hizi hapa:

Kumfukuza mtoto nyumbani baada ya kutenda kosa. Wewe ndio mzazi wake unataka aende kwa nani sasa, tena wengine hufukuza hata iwe usiku mwishowe mtoto abakwe utamlaumu nani,!!

Kumpiga mtoto hadi unamdhuru. Kuna watoto wanapigwa hadi wanavunjwa, kupigwa ngeo. Mtoto anakuwa na vidonda mwili mzima hadi huruma.

Kunyimwa chakula. Hivi mzazi utamnyimaje mtoto chakula eti adhabu hiyo dah! Mtoto anahitaji chakula ili akuwe na kujengeka mwili ( growth & development).

Kuchomwa moto. Baadhi ya wazazi huwachoma watoto viganjani hasa wale wadokozi iliwakome. Kwanza hii tabia ni indication kuwa mtoto hashibi sasa badala ya kumpa chakula cha kutosha mtu anaishia kumchoma moto mtoto.

Ewe mzazi/mlezi mpe mtoto adhabu inayolenga kumfunza sio kukomoa.
Adhabu za kikatili humfanya mtu kuwa na tabia za ajabu ukubwani.

Mostly tulivyo leo ni reflection ya malezi tuliopewa na wazazi/walezi wetu.
 
Kuna wazazi wana mitabia ya ajabu sana kama mashetani vile.
 
kati ya wazazi wapumbavu ni wanaotoa vipigo vikali kwa watoto wao!

hivi unaanzaje kumburuza mtoto.


very stupid.

wamama wa kambo ndo balaa tu, wanapiga watoto kama nyoka!

katoto kadogo kananyukwa kama mwizi..

ukienda mashuleni walimu nao wanapiga watoto kama kitu gani.

hawa wanaotoa vipigo kwa watoto hasa wadogo Wanatakiwa wakamatwe na waadabishwe kwelikweli.

ningekuwa na hayo mamlaka ningewakomesha haswaaa haswaaa!

kwanini upige watoto??????

sipendi kabisa uonevu na mambo ya kikoloni.
 
kati ya wazazi wapumbavu ni wanaotoa vipigo vikali kwa watoto wao!

hivi unaanzaje kumburuza mtoto.


very stupid.

wamama wa kambo ndo balaa tu, wanapiga watoto kama nyoka!

katoto kadogo kananyukwa kama mwizi..

ukienda mashuleni walimu nao wanapiga watoto kama kitu gani.

hawa wanaotoa vipigo kwa watoto hasa wadogo Wanatakiwa wakamatwe na waadabishwe kwelikweli.

ningekuwa na hayo mamlaka ningewakomesha haswaaa haswaaa!

kwanini upige watoto??????

sipendi kabisa uonevu na mambo ya kikoloni.
Mkuu we acha tu, wengine mitusi utakuta mtoto anatukanwa kwa laana zote ulimwenguni
 
Kuna wazazi wana mitabia ya ajabu sana kama mashetani vile.
kuna mama mmoja aliokota mtoto chokoraa akaanza kuishi nae.

katoto kadogo kana miaka nane hivi..

kanatumikishwa, kanabebeshwa maji, kanadeki nyumba, kanafagia uwanja, kanapigwa vipigo vikali vya mbwa mwizi..

yani hawa watu ningekuwa na mamlaka ningewatia adabu ya uhakika.

watoto wanaelekezwa, watoto wanahitaji upendo!!

mamlaka zinazohusika na watoto waangalie hili swala, watoto wanapigwa sana!!

kamata hayo majitu peleka mahakamani.

kwanini upige watoto wadogo???
 
Hakuna watu waelewa kwa vitendo kama watoto hata hakuna haja ya kutumia nguvu nyingi kabisa wanaopiga watoto kama jambazi nawashangaa sana
 
Mkuu we acha tu, wengine mitusi utakuta mtoto anatukanwa kwa laana zote ulimwenguni
hao wazazi / walezi wa hivyo ni wapumbavu tu.

huwezi kumtupia mtoto maneno makali yanamuingia na yanamuharibu saikoloji.

mtoto analishwa maneno machafu kweli.

very stupid!
 
nawahurumia sana watoto wa zama hizi, maana wazazi wengi siku hizi ni mwendokasi upstairs.
 
Kumchoma moto mtoto???!!...kumfukuza ndani, kumnyima chakula??!
Asee huu sasa uonevu.
 
Hakuna watu waelewa kwa vitendo kama watoto hata hakuna haja ya kutumia nguvu nyingi kabisa wanaopiga watoto kama jambazi nawashangaa sana
nilifika mahali nikakakuta katoto ka kiume kalichookotwa kanalelewa hapo na huyo mama.

nilivyofika kakawa karibu sana na mimi, kila kakiniona kananikumbatia kanafurahi kweli.

akija mama kanapoaaa!!

nikaa kaa nacho nikawa naongea nacho taratibu, kalikuwa kana mengi sana moyoni, ni kadogo lakin kanaongea mpaka kanalia.

he was very honest na hana tatizo.
 
Kumchoma moto mtoto???!!...kumfukuza ndani, kumnyima chakula??!
Asee huu sasa uonevu.
kati ya watu wanaohitaji kulindwa kwa nguvu zote ni watoto!

wanaumizwa akili, na miili.

siku zote nakataa kabisa vipigo kwa watoto au wanafunzi wa sekondari.

hizi tabia za kikoloni za kupiga watu marungu zinatengeneza taifa la watu wenye matatizo ya akili.


viboko vinaharibu kabisa afya ya akili.

watoto wanakuwa mazezeta na watu wa kuogopa ogopa tu.

kuna njia nyingi sana za kuelekeza.


hasa hawa watoto wadogo wa miaka moja mpaka kumi...

nashangaa kweli nikiona mtoto anapigwa.
 
daaah hiyo ya kumchoma moto mtoto mikononi niliona dada yangu alimchoma mtoto wake mikono kisa mtundu, hadi leo mtoto anamakovu ukimuuliza anakwambia mama alinichoma,
 
Kuna wazazi wana mitabia ya ajabu sana kama mashetani vile.
Kuna baba mmoja alikuwa anakaanga vitumbua na kumpa bintiye akauze siku moja wajanja wakachukua vitumbua kadhaa na kutokomea bila kumlipa yule mtoto, asee alivyorudi home babake akamfukuza. Yule binti alirudi home kwao after six yrs akiwa na watoto wawili.
 
kati ya wazazi wapumbavu ni wanaotoa vipigo vikali kwa watoto wao!

hivi unaanzaje kumburuza mtoto.


very stupid.

wamama wa kambo ndo balaa tu, wanapiga watoto kama nyoka!

katoto kadogo kananyukwa kama mwizi..

ukienda mashuleni walimu nao wanapiga watoto kama kitu gani.

hawa wanaotoa vipigo kwa watoto hasa wadogo Wanatakiwa wakamatwe na waadabishwe kwelikweli.

ningekuwa na hayo mamlaka ningewakomesha haswaaa haswaaa!

kwanini upige watoto??????

sipendi kabisa uonevu na mambo ya kikoloni.
Kuna mama mmoja wa kambo aliwahi kumfunga mtoto wa mumewe kamba kwenye uume eti asikojoe, mwanaume mtoto wako akilelewa na mama wa kambo uwe makini.
 
kuna mama mmoja aliokota mtoto chokoraa akaanza kuishi nae.

katoto kadogo kana miaka nane hivi..

kanatumikishwa, kanabebeshwa maji, kanadeki nyumba, kanafagia uwanja, kanapigwa vipigo vikali vya mbwa mwizi..

yani hawa watu ningekuwa na mamlaka ningewatia adabu ya uhakika.

watoto wanaelekezwa, watoto wanahitaji upendo!!

mamlaka zinazohusika na watoto waangalie hili swala, watoto wanapigwa sana!!

kamata hayo majitu peleka mahakamani.

kwanini upige watoto wadogo???
Aisee inakera sana.
 
Hakuna watu waelewa kwa vitendo kama watoto hata hakuna haja ya kutumia nguvu nyingi kabisa wanaopiga watoto kama jambazi nawashangaa sana
Yawezekana na wao walilelewa hivyo basi wanajua mwendo ndio huo huo!
 
2 Reactions
Reply
Back
Top Bottom