Mjuni Lwambo
JF-Expert Member
- Apr 25, 2012
- 9,416
- 8,876
Mwalimu alisema mtu akionja nyama ya mtu hataacha, baada ya muungano kufa wazanzibar watatafunana wao kwa wao,GOD FORBID
Mgeni bin rasshid, karibu jamvini, nijaalie sheikh! naona umekuja na taharuki, taratibu mziwanda wangu, hili jamvi kubwa, baraza ya heshima. Karibu tena mwinyi.nafikir ulochanganyikiwa niwewe usojua asili wa mila na utamaduni wako hem unaelewa eleza japo kwa mukhasari kidogo wazanzibar sio wabamtu huu ndo ukweli wacheni kukaa kwenye vilab vyapomabe ndo kwanza mnaandaa vitambulisho vya kujuana leo eti vya taifa la tanzania mbona hamuutaki ukweli na mnakumabatia ulaghai na utape nivya tanganiyika au utanganyika ndo utaifa wenu kwanini hamilipendi hili jina au nyerere aliwalisha sumu juu ya kuukanusha utanganyika
Mgeni bin rasshid, karibu jamvini, nijaalie sheikh! naona umekuja na taharuki, taratibu mziwanda wangu, hili jamvi kubwa, baraza ya heshima. Karibu tena mwinyi.
Karume ana asili ya Unyasa, sijui kama si mbantu na kama si mzanzibar. Wazanzibar hasa wa unguja ni zao la utumwa kutoka unyamwezini, umakua umatumbini n.k. sijui kama hao hawana Ubantu na kama wanao siyo Wazanzibar?
Mwinyi, Nasor Moyo na Jumbe asili yao ni bara, je hao si wabantu na kama ni wabantu wanakuwa katika daraja gani Znz.
Bin Rasshid, kwani kuwa Mbantu ni tusi? Kuna punguza nini katika ubinadamu wako?
Wakati ukisema Znz si wabantu wenzako wanaandika makala na kule Mzalendo.net wanasema Znz ni Cosmopolitan. Sasa unakuwaje na Cosmopolitant kama Hukubali Wabantu ambao ni sehemu kubwa ya hiyo cosmo.
Psychologically kinachokukera ni jina, wewe unaitwa Bin Rasshid, sasa unapopewa uzalendo sawa na Natepe au Mwakanjuki, Kombo au Makame, unajisiikia dhalili. Ungependa watu waliokuzunguka wawe akina Kharrfim Bin Sayed, Alwatan Abdulkarim, Almaarufu Hussein Abdallah Haji bin Zuein n.k.
Jamani ehee, washirazi wanaidai nchi yao, kitambulisho ni rangi ya dhahabu na nywele za katani.
Ukiwa na rangi ya giza na nywele za kipili pili, jina la 'kishirikina' jiulize utakwepa minyororo?
siku hizi siyo minyororo ya chuma kama ile ya utumwa, ni ya sayansi na teknolojia. Unapewa kila kitu, na mnyororo ni electronic.
LET ZNZ GO!
Mzee Mwanakijiji,
Nafikiri biashara ya kuuza watu,
waliifanya kabla ya kuokoka sorry Kusilimu na kuwa Waislamu,
Sidhani Muislamu wa kweli mnyenyekevu wa moyo,
anaweza kamata mtu akamuuza kama tende.
Au pengine mtu kwao ni Muarabu tu.
hawa ni watumwa kutoka tanganyika wakipelekwa super market ya utumwa znz,
hakuna mtu wa znz aliefanywa mtumwa kwa sababu biashara ya utumwa ilipo anza zanzibar watu wake tayari walikua na serikali inayo jiendesha
tanganyika, malawi na kwengi neko hakukua na serikali yoyote, ma chief walikua wakiwauza watu wao kwa kupewa vioo!! ama wanawake !!!
hivyo hizi picha za kuchora hazia shirii kuwa hawa ni wa znz bali ni wa bara ambao wanapelekwa znz kuuzwa
hawana uhusiano na znz nz hawakuwa na haki ya kiraia huko,
tusichanganye mambo!!
hawa uta waona kule marekani ,na ulaya amabo pengine ndio kina Ophrah ama Tyson, na wengine wapo Kule salala Oman, ukienda kule utawaona 'waarabu' weusi kuliko mnyachusa
hawa hawakukuta znz haina watu bali walikuwapo,,,, na wao walikua wapita njia tu ..wakinunuliwa haya hawooo ulaya...
Gia ya kuingilia....
Sijui kama alikuwa anamaanisha kuwa waliokuwa humu nao walikuwa wanajihisi hivyo hivyo kabla ya kuja Mwingereza!
Watumwa wakiwa na minyororo karne ya 19 visiwani Zanzibar ambako msomaji anatuambia kuwa watu wote waliishi kwa "mapenzi makubwa". NIna uhakika - nikiamini maneno ya mwandishi - hawa jamaa wenye minyororo walikuwa wanashukuru wanavyopendwa na kutendewa mambo mema na Wazanzibari "wenzao"!
Wazanzibari kwa kweli kabla ya Mwingereza walikuwa wanapendana sana!
Wazanzibari ni watu walio na asili zao nyingi na ustaarabu mchanganyiko ulizoanzia mbali. Asili za kiarabu, ki-pashia, kihindi, kitanganyika, kiganda, kikenya, kimsumbiji, kikomoro, kinyasa, kisumeri, kiassiri, kisomali, kiabisini, kifoniki, kidiba, kidebule, kireno, kibaluchi, kikurdi, kijojia, kichina, kisrilanka nk Wengi wao ni machotara, hakuna awezae kukaza mdomo akamtukana mbantu, akija akitanabahi kumbe kamtukana babu yake, au
Huu ndo upendo wa kweli wa Mtwana kumpenda Bwana wake.
Unakosea, siyo baadhi yao wapo, ukweli ni kuwa wale walioachwa baada ya biashara kupigwa marufuku hakuna aliyefanikiwa kurudi Unyamwezini, Umanyema au Uwemba. Tena basi kwa wale walioona hila za kutengwa wengine wapo south Africa na wanasehemu yao maalumu.Unaposema baadhi yao, unajaribu kujenga hoja kuwa weusi ni 'minority' kama ambavyo nitakuthibitishia mbele ya safari.Macos;4385528]Nguruvi3,hapana wa znz ni wa znz tu hawana uhusiano na watanganyika, wapo wahamiaji ambao walifika zanzibar kutokana na masalia ya biashara ya utumwa. itakumbukwa kuwa zanzibar ndio ilikua ndio soko lautumwa afrika mashariki , wafanya biashara wa utumwa wa kizungu, kiarabu na washirazi kwa kushirikiana na ma chifu wa tanganyika walifanya biashara hii na znz ndio ilikua ndio super market yao.hakuna mshirazi aliefanywa mtumwa, mara baada kupigwamarufuku biashara ya utumwa kutokana na uvumbuzi wa viwanda hivyo nguvu kazi hii haikutakiwa tena huko ulaya wale masalia ambao hawakupatwa kuuzwa ndio waafrika walio bakia zanzibar na ndio baadhi yao wapo
Hapa unasahau kuwa mwandishi wa makala alisema kuwa nchi ya Marekani imeundwa na wahamiaji bila kujali walitokea wapi. Kwahiyo kuwataja hao na kusema wamekuja karne ya 20 si kweli, ukweli ni kuwa wazazi wao walikuja kabla ya hapo. Hata hIvyo hiki ndicho Washirazi wanakitaka, kuonyesha kuwa Waafrika walifika Zanzibar na kuwakuta wao wakiwa na nchi.kundi la pili la watanganyika ni wale waliokuja znz katika karne ya 20, hawa kufata neema ya uchumi na kazi , hawa wamo kina Ali hassan mwinyi, Aboud Jumbe Mwinyi, Seif Bakari , Edington Kisasi, Sepetu, David WAKATI, Abeid Aman Karume(alitokea Malawi)hakuna mshirazi aliekubali ku olewa na mtanganyika ama mkenya ama mmalawi ila wachache sana, lakini washirazi,wapemba , na watumbatu walikuwepo znz miaka na miaka na ndio asili yao znz , watanganyika hawana historia yoyote kwamba waliingia znz kabla ya utumwa
Effect unayotarajia ni katika lugha na tamaduni. Umesahau kuwa Waarabu hawana ngoma ya Msewe! sina maana kuwa msewe unatoka bara lakini nataka nikuonyeshe kwa uchache tu kuwa athari za mwingiliano kati ya Tanganyika na Znz hazipo katika lugha ya kiarabu, ukristo au Uislam ni lazima ufungue macho na kuangalia kwa upana zaidi na mbali kuliko pale mwarabu alipokuonyesha! Msewe uwe umetoka msumbiji, Kenya n.k bado ni wa Mrima.inajulikana wazi hapa dar es salaam na tanga na bagamoyo miaka 300 iliyopita hapajakuwa na mhaya , myachusa,mchaga, ama mhaya aliyerfika maeneo ya pwani, seuze ku - venture safari ya bahari kwenda znz !!! huu ni ukweli, kabla ya kujengwa reli watanganyika wa kati ya tanzania hawakuwahi kuja huku pwani hata siku moja, sasa wa znz walikua ni wa znz na wa tanganyika walikua wa wabara tu, ambao walikua chini ya ma chief wao, na taratibu zao, za kiafrika , huu ndiio ukweli, hakuna historia yoyote inayosema amabyo ina mshiko kama kuna mhaya znz, ama mchaga, ama mhehe,ama mnyachuza, laiti ingekuwa kuna slight intergration ya watu wa bara na znz basi wangeacha atahari japo kidogo,kwenye tanaduni ama lugha
Nimekuuliza ngoma ya msewe asili yake ni Uarabuni?wareno walifika pemba na kutawala chini ya miaka 100 lakini walia cha athari ya lungha na mitaa. seuze leo iwe jamaii ya znz iwe ina asili ya bara ama tanganyika halafu kusiwe na athari yoyote ya kutoka mrima,!! ila ni ukweli kwamba znz ndio imeacha athari kubwa upande wa tanganyika , kwa dini, uislam. hata ukristo, wazungu walianzia znz, wame acha athari ya lugha ya kiswahili.
Ahsante kwa kueleza ukweli, kwamba akina Karume, Mwinyi, Jumbe, Nasor Moyo hao si Wazanzibar. Kama hakuna wenye asili ya kimasai, wangoni akina Moyo na Wanyasa akina Karume vipi.watu wa znz ni wa visiwani tu hawakua na asili ya bara tuache siasa za kuwadanganya watu.znz hakuna watu wenye asili ya kimasai
Unakosea, siyo baadhi yao wapo, ukweli ni kuwa wale walioachwa baada ya biashara kupigwa marufuku hakuna aliyefanikiwa kurudi Unyamwezini, Umanyema au Uwemba. Tena basi kwa wale walioona hila za kutengwa wengine wapo south Africa na wanasehemu yao maalumu.Unaposema baadhi yao, unajaribu kujenga hoja kuwa weusi ni 'minority' kama ambavyo nitakuthibitishia mbele ya safari.
Hapa unasahau kuwa mwandishi wa makala alisema kuwa nchi ya Marekani imeundwa na wahamiaji bila kujali walitokea wapi. Kwahiyo kuwataja hao na kusema wamekuja karne ya 20 si kweli, ukweli ni kuwa wazazi wao walikuja kabla ya hapo. Hata hIvyo hiki ndicho Washirazi wanakitaka, kuonyesha kuwa Waafrika walifika Zanzibar na kuwakuta wao wakiwa na nchi.
Inathibitika katika kauli yako kuwa Waafrika walipofika Znz Washirazi walikuwa na asili yao hapo.
Huu ni udanganyifu wa hali ya juu, kule Mzalendo watakuelewa, JF tutakwambia stop!
Hakuna Mshirazi aliyekuwepo Afrika. Wote wamekuja kwa masilahi ya biashara.
Hakuna Mwarabu mwenye asili ya Zanzibar wote wamekuja kutoka Uarabuni.
Inaleta mantiki kama kuna mwafrika amwenye asili ya Znz, kwasababu ni ujinga kuamini kuwa Tehran ni karibu na Znz kuliko Dar es salaam, big anachronism! serious black alienation. Effect unayotarajia ni katika lugha na tamaduni. Umesahau kuwa Waarabu hawana ngoma ya Msewe! sina maana kuwa msewe unatoka bara lakini nataka nikuonyeshe kwa uchache tu kuwa athari za mwingiliano kati ya Tanganyika na Znz hazipo katika lugha ya kiarabu, ukristo au Uislam ni lazima ufungue macho na kuangalia kwa upana zaidi na mbali kuliko pale mwarabu alipokuonyesha! Msewe uwe umetoka msumbiji, Kenya n.k bado ni wa Mrima.
Najua unachotaka kukwepa ni kujinasibisha na Tanganyika lakini ukweli unabaki kuwa Makame, Kombo, Mwanamtama, Karume, Natep, Mwakanjuki hayo si majina ya Kiarabu. Sasa kama wana qualify kuwa wazanzibar au hapana hilo ni jukumu la Wznz. Inatosha mimi kusema Mapuri si mzanzibar halisi kwasababu ya jina, nywele na rangi! yeye alikuja karne ya 20 na kuwakauta akina Sheikh Khalid, Muhusini, Babu zake Maalimu Seif, na wale wenye madevu na nywele za katani.
Nimekuuliza ngoma ya msewe asili yake ni Uarabuni?Ahsante kwa kueleza ukweli, kwamba akina Karume, Mwinyi, Jumbe, Nasor Moyo hao si Wazanzibar. Kama hakuna wenye asili ya kimasai, wangoni akina Moyo na Wanyasa akina Karume vipi.
Tunachokiona hapa ni ukweli ulio wazi kuwa WASHIRAZI wanafanya maandalizi ya hali ya juu ya kuirudisha nchi yao iliyopotea baada ya MAPINDUZI YA 1964. Mwandishi wa makala amethibitisha kwa kauli ya 'neema kabla ya 1964' na bwana Macos anasema hakuna mzanzibar mwenye asili ya Tanganyika, hata wale watumwa wapo wapo tu, mwenye asili ni MSHIRAZI anayehitaji nchi yake kwa ushirika nna Wa Oman na Waarabu.
Nje ya Muungano, kama una ngozi nyeusi basi jiandae kuwa kijakazi. Hata hivyo mwafrika ameahidiwa neema iliyokuwepo kabla ya 'upuuzi wa Mapinduzi 1964'. Mzanzibar mkazi ni mwafrika, mzanzibar mzawa ni MSHIRAZI, sasa fitna inajitokeza.
WASHIRAZI wanadai nchi yao!
LET ZNZ GO!
Ndugu yangu Macos, sasa ndio unajichanganya kabisa.HiLI SOMO PEVU, Maana mabo mengi yamekorogwa na uongo..
akuna anaesema znz ni ya waarabu..hata siku moja...ila wapo waarabu wahamiaji .warabu walifika znz 1628 baada ya "WAZANZIBARI HALISI AMBAO HAWANA UUSIANO NA TANGANYIKA WALA WARABU" chini ya kiongozi wao Mwinyi mkuu wa unguja na pemba kupata dhiki ya utawala wa kishenzi wa wa Wareno, walipeleka ujumbe Oman kuomba msaada wa kijeshi kuja kuwasaidia kuwatoa wareno katika ardhi yao.
(wa oman wao waliwatoa wareno huko kwao)
hapa ndipo wa Oman kuja kwao Znz , lakini haikua rahisi kwani wareno walikuwa tayari wapo coast yote mpaka lamu mombasa kilwa hadi chini maputo.
wa oman hawa waliweza kuwatoa wareno katika pwani hizi na ikabaki kule msumbiji tu.
wengi walifariki na kuteswa na wareno lakini waliwatoa ndugu zao kutoka katika mateso ya wareno. vita hii ilichukua zaidi ya miaka 50 na hapa askari kwa askari wa ki oman walikua wakija huku na ndio mwnzo wa wao kuhamia pwni ya afrika mashariki.
sasa utaona ile jamii ya znz ya kina mwinyi mkuu walikua ni wa znz wa asili na asili yao ni visiwani.
warabu waliwakuta
watumwa watanganyika na kutoka kwengine nao walikuja wakawakuta
wahindi waliwakuta
na wazungu waliwakuta
visiwa hivi vilikuwa na wenyeji wake na ndio hao washirazi
hakuna anaesema kwamba waraabu ndio wenyeji , wao wanaajujua kwamba wao ni Muhajirun, sawa na wabongo, wote ni walowezi,
walipokuja wa oman znz tayari ni nchi ya kiislam, kulikuwa tayari kuna misikiti, mingi sana, nao hao wa oman walijenga yao ya madhehebu yao ya kiibadhi.
ndio maana znz wenyeji wote ni wa madheheb ya sunni mabyo si madhehebu ya watawala wa ki oman.
ukweli utabaki znz ina wenyewe tangu enzi na enzi...
kabla ya mwarabu wa oman
kabla ya kuja wa tanganyika kwa njia ya utumwa
na tanganyika ina wenyeji wake
kila nchi ina wenyeji wake
watumwa walioplekwa marekani ni zaidi ya 20,000,0000 na hawa hawafanyi kuwa wao ndio asili yao ni marekani asili yao ni afrika, wenyeji ni red indians hata kama wazungu wahamiaji wa huko wali wachinja chinja
kule Burma kuna issue sasa hivi wenyeji MA BUDA wanawatoa kwa nguvu wahamiaji waislam, asili ya Rongyia, na hawa walihamia Burma miaka zaidi ya 200.
siasa za uongo ambazo ndio hizo zinazowataka kuwafanya wazanzibar waamini kuwa asili yao ni bara ili kuhalalisha muungano , lakini wao wenyewe sasa wamengamua kuwa wao ni wazanzibar na waislam na wana asili yao ambayo haina uhisiano na uwarabu wala utanganyika sasa kuna wanaosappurt dhana hii na wanaopinga...wana pinga kuoogopa aumoja wa znz
ustaarabu huo ni kuwafanya weusi watumwa na weupe ni watwana, sawa leta hadithiWAZANZIBARI NI JAMII YENYE ASILI NA USTAARABU MSETO (COSMOPOLITAN SOCIETY) NA SIO JAMII YA KIBANTU (KIAFRIKA)
Written by Ahmed Omar Khamis| 04/08/2012
Kabla ya kuja mkoloni wa kiingereza Zanzibar, wazanzibari wa asili mbali mbali kama walivyo hivi sasa walikuwa wakiishi kwa mapenzi makubwa bila ya chuki za ukabila na urangi, au kwa lugha nyengine, waliishi bila ya mimi ni nani na wewe na nani.
Muingereza alikuja kuwaundia wazanzibari vyama vya kikabila na urangi. Vyama hivyo yaani jumuiya za kikabila ni kamavile Arab association, Shirazi association, African association, Indian association na jumuiya nyengine.
Wazanzibari nao wakavishabikia vyama hivi vya kikabila na kila mmoja akawacha kupigania maslahi ya uzanzibari na akapigania maslahi ya kabila lake. Lakini hayo yalikuwa ni mafanikio makubwa kwa Muengereza, kwani ni sera yake muhimu ya ukoloni ya wagawe uwatawale (divide and rule).
Kuanzia harakati za kutafuta uhuru chama cha ASP na viongozi wake akiwemo kiongozi mkuu Karume waliukejeli na kuupiga vita ukweli kwamba wazanzibari ni watu wa asili na ustaarabu mseto na kujaribu kuyatenga makundi yote ya kizanzibari yalio na asili zake kutoka nje ya bara la Afrika kama vile waarabu, wahindi, magoa nk. Jambo la kushangaza zaidi ni kwamba hata washirazi wenye asili zao kutokeaIranambao ndio wanaofanya asilimia kubwa ya wazanzibari nao walipigwa vita.
Kama hilo halitoshi hata wakomoro wenye ngozi nyeupe lakini wenye asili zao kutokea katika bara la Afrika nao walikejeliwa na kukataliwa. Kwa viongozi wa ASP mzanzibari namba moja au mzanzibari asilia na mwenye hadhi kubwa ni lazima awe mwafrika mwenye ngozi nyeusi. ASP iliupigia kelele, kuunadi na kuutukuza uafrika pamoja na ngozi nyeusi na kuzidharau jamii zote za kizanzibari zilizobaki.
Kabla ya mapinduzi ASP na viongozi wake walijaribu kuwaheshimu washirazi wakifahamu bila ya wao na wingi wao ushindi kwa ASP ingelikuwa ndoto. Mara tu baada ya mapinduzi na ASP kushika hatamu chuki dhidi ya ushirazi na washirazi zikadhihirika.
Serikali ya Karume ilipambwa na viongozi wenye asili zao kutokea bara hususanTanganyika. Hii inajionyesha hata kwa majemedari wa mapinduzi na wajumbe wa baraza la mapinduzi la mwanzo lilikuwa na watu wengi zaidi wenye asili zao kutokea bara. Hii iliwafanya wafikirie kwamba serikali ya mapinduzi ni ya wazanzibari wa asili za bara na waliobaki ni watu wa daraja la pili. Baada ya mapinduzi Karume aliwataka watu wote wenye asili ya kikomoro kuomba uzanzibari (Burgess 2009:204). Kwa kuwa Karume mwenyewe alikuwa na asili yake kutokeaMalawialiwaogopasanawashirazi. Katika akili yake Karume aliwaona washirazi ni watu wanaoringa na kujidaikamawazanzibari halisi. Hivyo basi aliwalazimisha washirazi nao kubadilisha makabilayao.
Washirazi wengi walilikataa agizohilola Karume hususan wapemba. Wengi wa washiraziPembawalisema wao hawana kabila jengine mbadala mpaka Karume atakapowapatia baba wengine. Hivyo basi hali halisi ya ugozi na ukabila ilipamba moto zaidi baada ya mapinduzi kuliko kabla.
Wapigaji na wachezaji wa ngoma hiyo chafu ya ukabila baada ya mapinduzi walikuwa viongozi wa serikali ya mapinduzi na wajumbe wa baraza la mapinduzi la mwanzokamavile Karume mwenyewe, Seif Bakari na Abdalla Said Natepe, Mungu awarehemu.
Baada ya mapinduzi vitabu vyote vya historia vilivyofundisha ukweli kuhusuZanzibar, maisha ya masultani, na urithi wa ustaarabu mseto vilichomwa moto (Burgess 2009). Tukio moja la uchomaji huo lilifanyika eneo la Lumumba Unguja mbele ya macho ya maelfu ya watu. Badala yake mwenyekiti wa Youth league, Seif Bakari aliandika kitabu kipya kilichokua kikisomeshewa watoto mashuleni. Katika kitabu chake hicho, Seif Bakari anadai kuwa yote yaliopita kabla ya mapinduzi yalikuwa si chochote bali ni dhiki na dhuluma.
Katika kuzidi kuchonga chuki miongoni mwa wazanzibari weusi dhidi ya wenye ngozi nyeupe, Abdalla Said Natepe ambae ni mjumbe wa mwanzo wa baraza la mapinduzi na mjumbe wa kamati ya watu 14 alikuwa akifanya mikutano ya hadhara kuwaaambia watu hadithi za uzushi. Miongoni mwa hadiuthi hizo ni kuwa waarabu waliwalazimisha waafrika kupanda minazi kisha wakawa wanajifundishia shabaha kwa kuwatungua kwa risasi.
Hadithi nyingine ni kuwa waarabu waliwalazimisha wanawake wa kiafrika kufyagia barabara kwa maziwayaona waja wazito wa kiafrika walip[asuliwa ili bibi wa kiarabu ajue mtoto amekaaje tumboni. Mafundisho haya yamekuwa yakitolewa mashuleni kwa muda mrefu ili kutia sumu katika akili za watoto wakishirazi na kifrika dhidi ya waarabu.
Nyimbo za uafrika dhidi ya asili nyengine zote ziliendelea kuimbwa ndani serikali ya mapinduzi kupitia warithi wake wenye misimamo mikali ya uhafidhina wa ugozi na umapinduzi kwa lengo la kulinda malengo na uhalali wa mapinduzi hayo.
Kuthibitisha kasi na nguvu za uhafidhina huu na chuki dhidi ya watu wasiokuwa na asili ya kiafrika ndani ya Zanzibarni maneno ya Omar Ramadhani Mapuri, ambae yeye mwenyewe ana asili yake kutoka Tanzaniabara, aliyekuwa Waziri wa elimu na Naibu waziri kiongozi katika awamu ya nne ya Rais Salmin Amour. Kupitia kitabu chake, Zanzibar Revolution, Achievements and Prospects, kitabu ambacho kinazungumzia kiwango cha juu cha ukabila katika enzi za ustaarabu duniani, Mapuri ameweka wazi hisia zake kali dhidi ya watu wasiokua waafrika ndani yaZanzibar.
Lengo kuu la Mapuri katika kitabu chake ni kuwataka wazanzibari wenye asili za kiafrika kuungana dhidi ya kile anachokiita chokochoko na uchokozi wa nchi za magharibi na waarabu ambao chini kwa chini kwa mujibu wa Mapuri wanataka kurudisha tena ushawishi waoZanzibarkama ilivyokuwa kabla ya mapinduzi. Umoja huu ambao Mapuri anawaasa wazanzibari ndio ule ule uliotumika katika harakati za uhuru na mapinduizi ya 1964.
Katika kitabu chake pia Mapuri anakana kwa nguvu zote mauwaji yaliyofanywa na mapinduzi ya 1964 na kwa mujibu wa mawazo yake yale yanayoripotiwa kuwa ni upotezaji wa roho za watu kwa mgongo wa mapinduzi ya 1964 ni uongo mtupu na kusisitiza kwamba watu waliokufa kutokana na mapinduzi hayo ni wachache mno. Hata hivyo katika kitabu chake anadai kuwepo kwa nyaraka zinazobainisha azma ya serikali ya Shamte na Sultani iliyopinduliwa ya kutaka kuuwa raia wengi wa kiafrikakamani kulipiza kisasi kwa mauwaji ya waarabu waliouliwa kufuatia uchaguzi wa juni 1961 ijapokuwa hakubainisha katika kitabu chake nyaraka hizo zilipo.
Mapuri anadai nyaraka hizo zinathibitisha kwamba serikali ilipanga kuuwa waafrika sitini (60) kwa kila mwarabu mmoja aliyeuliwa Juni 1961. Mapuri pia anadai nyaraka hizo zinathitisha azma ya serikali ya Shamte na Sultani kuzitaifishamalizote za waafrika wasio na asili za kizanzibari. Hakumalizia hapo Mapuri pia ameandika kwamba Serikali ya Shamte ilikuwa na lengo la kuwafanya watumwa wazanzibari wote wenye asili ya kiafrika na hatimae Zanzibar kutangazwa kama ardhi ya waarabu.
Kikubwa zaidi ambacho pia Mapuri amewatanabahisha wazanzibari katika kitabu chake ni azma ya Serikali ya Shamte iliyopinduliwa kuwauwa watoto wote wa asili ya kiafrika na wanawake wenye asili ya kiafrika kulazimishwa kuolewa na waarabu kwa malengo ya kutokomeza ngozi nyeusiZanzibar.
Alichokifanya Mapuri bila shaka lilikuwa si jambo geni katika historia yaZanzibar. Ni marudio tu ya yale yalioanzia miaka ya 1960 ya mapambano ya makabila katika kugombania kumezwa, kufunikwa au kutokomezwa na makabila mengine.
Ni jambo la kushangaza mno kwa enzi ambayo vuguvugu la kihistoria la ukabila na uasili tayari limeshasahaulika, kiongozi wa ngazi za juu katika serikali ya Mapinduzi ya Zanzibaranapika upya migawanyiko ya wazanzibari kwa misingi ya rangi, ngozi na wanakotokea mababu zao.
Kiongozi kama huyu bila shaka ana dhima kubwa ya kuwaunganisha wazanzibari walio na asili na utamaduni wa kila namna karibu kutoka pembe zote za dunia lakini badala yake anashajihisha na kuhimiza umoja na muungano wa baadhi ya wazanzibari dhidi ya wenzao. Hata hivyo sio Mapuri peke yake katika viongozi wa leo wanaopiga kelele za ukabila na uasili ndani ya Zanzibarya kisasa.
Wapo wenzake Mapuri ambao wao wamefika mbali zaidi kwa kudai kwamba vijukuu na vinyinginya vya waarabu hawapaswi kupewa madaraka ya Zanzibarkwa kunasibika kwao na kabila la wapinga mapinduzi ya 1964. Katika kitabu chake, Kwaheri ukoloni kwaheri uhuru, Harith Ghassany analizungumzia hivi suala hili.
Fikra ya uzalendo ya Pan-Africanism ambayo ilikuwa ikipigiwa kelele na hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere ilikuwa na misingi kwamba kila asiye Muafrika ni mgeni (wakuja) Afrika na kwa maana hiyo pia ni mgeni Zanzibar hata kama alizaliwa na alikuwa na mizizi mirefu na mipana ndani ya Zanzibar.
Kinyume chake kila aliyekuwa ana asili ya Kiafrika (kibantu) na hata kama hakuzaliwa na wala hana mizizi mirefu ndani ya Zanzibar basi ana haki zaidi juu ya kuweza kutawala kwa sababu tu ni Muafrika. Hapa sharti ifahamike kwanza kuwa neno Afrika linatokana na neno Ifriqiya, ambayo wanahistoria wanathibitisha ilikuwa ni jimbo la Kaskazini ya Afrika katika nchi ambayo kwa sasa inajulikana kwa jina la Tunisia.
Ibn Khaldun, mwanafalsafa wa historia maarufu duniani na baba wa sayansi ya jamii (sociologist) aliyeishi miaka 676 nyuma, amemzungumza katika kitabu chake Mfalme wa zamani wa Yemen Afriqus Bin Qays Bin Sayfi. Kwa mujibu wa Ibn Khaldum Mfalme huyu aliishi wakati wa Nabii Musa au labda kidogo kabla yake. Ibn Khaldum anathibitisha kuwepo kwa mfalme huyo kutoka Yemen ambaye jina lake hilo inawezekana sana likawa moja wapo wa asili ya jina Afrika.
Mawazo yaliyoenezwa kila upande ni kwamba Zanzibar ni ya Muafrika mweusi mwenye asili ya bara peke yake kuliko Muafrika mwingine yeyote hata kama amezalika huko Zanzibar kwa dahari nyingi. Mawazo haya yanatokana na fikra kuwa Bara la Waafrika ni Bara la watu weusi tu. Watu weusi hao tena ni wale wanaotokana na asili ya Kibantu na Wabantu hao bila shaka wawe hawana kabisa asili au uhusiano wowote na Waarabu.
Wenye mawazo haya bila shaka walisahau kuwa wanalitenga kundi kubwa la Waafrika wa Kaskazani katika nchi za Ethiopia, Somalia, Djibouti, Eritrea na Mauritius. Halkadhalika mawazo hayo yamewatenga wazungu wa Afrika Kusini, Zimbabwe na Kenya. Pia mawazo hayo yamewatenga Mayahudi na Wahindi wazalendo wa Afrika, na makabila yote ya watu ambayo yana chimbuko lake katika bara hili (Gassany 2010).
Wazanzibari ni watu walio na asili zao nyingi na ustaarabu mchanganyiko ulizoanzia mbali. Asili za kiarabu, ki-pashia, kihindi, kitanganyika, kiganda, kikenya, kimsumbiji, kikomoro, kinyasa, kisumeri, kiassiri, kisomali, kiabisini, kifoniki, kidiba, kidebule, kireno, kibaluchi, kikurdi, kijojia, kichina, kisrilanka nk Wengi wao ni machotara, hakuna awezae kukaza mdomo akamtukana mbantu, akija akitanabahi kumbe kamtukana babu yake, au akakaza mdomo akamtukana mwarabu, akitanabahi kamtukana mama yake.
Uarabu, ubantu, uhindi, na asili nyengine zote za wazanzibari zilizopo kamwe hazibandukani na uzanzibari na bila ya kundi moja tu katika hayo ni sawa na mwanadamu asivyokamilika akikosa baadhi ya viungo vyake.
Tunaishukuru sana serikali ya ya Dr Shein ya Umoja wa kitaifa kwani imefanikiwa kufuta madoadoa ya kibaguzi baina ya wazanzibari wenyewe kwa wenyewe na kuusimika ule ustaarabu mseto (cosmopolitanism) unaomtambua kila mzanzibari kua ni mzanzibari bila ya kuangalia rangi yake, nywele zake pua yake.
Wazanzibari tusurudi nyuma haya ya kufunzwa kubaguana ndio yaliyotufikisha hapa na kuipoteza nchi yetu na hatimae kuingia mikononi mwa Tanganyika. Tuungane kwa umoja wetu turudishe heshma ya Zanzibar yetu yenye mamlaka kamili kama ilivyowahi kutamalaki hapo kabla ya 1964.
Jamhuri ya watu wa Zanzibar kwanza
London1,E bwana we! Jukwaa limewaka moto! Te ! Te! Ngoja nami nichangie kidogo. Ninavyojua history ya zanzibar neno 'shiraz' lina husiana na persia (iran) ndio maana afro shiraz party kiliitwa hivyo sababu ya wanachama walikuwa ni mchanganyiko wa wa persia(iran) na watu wenye asili ya kiafrika(wa bantu).kwa hiyo sielewi mwandishi ana maana gani anaposema wenyeji wa zanzibar ni washiraz! Hilo haliwezekani ikiwa hao washiraz (persians) ni waamiaji, asili yao itakuwa ni iran. Pia kusema uislamu ulikuwapo na misikiti ilikuwapo kabla ya waarabu sielewi data hizi kazitoa wapi, sababu ni common knowledge kuwa waarabu hasa wa Ndio waliosambaza uislamu east afrika.Ingawa wengi walikaa zanzibar lakini pia walifika miji kama kirwa,kigoma mpaka burundi na kujenga miji mikubwa, kueneza dini na kufanya biashara ikiwapo ya utumwa.na ukichunguza utaona sehemu hizo ndizo zina watu wanaoitwa waswahili kutokana na ku share culture hasa pwani ya bara na visiwa vya zanzibar.
Suala la nani mwenyeji Zanzibar siku zote litawaumiza vichwa watu!sababu ni kweli watu wengi wameamia zNz na history ya afrika haikuandikwa vizuri tunasoma tulichoandikiwa na ndio maana mpaka leo bara zima lina migogoro ya kila aina!.Lakini tujaribu kutumia 'common sense' turudi nyuma kabla mgeni yeyote hajafika znz ,si mmPersia wala mwaarabu sababu hawa ndio waamiaji wa mwanzo na vizazi vyao bado vipo'imagine hawajafika na mitumbwi yao, imagine kisiwani zanzibar unamwona mtu wa aina gani pale pwani?? Au humwoni mtu yeyote?.Hizi ni possibility mbili pekee.either zanzibar kulikuwa hakuna mtu wakati hao washiraz wanakuja au kulikuwa na watu weusi wenye asili ya kibantu.nasema hivi sababu zanzibar ni kisiwa kicho afrika na lazima wenyeji ni wenye asili ya ki afrika.peace! Am out!
Yaani kuna wazenji wanaamini kuwa wakazi asilia wa Zanzibar ni washirazi?
Inasikitisha sana!