Wazanzibar muungano tutaununua...

Wazanzibar muungano tutaununua...

Status
Not open for further replies.

Makamee

JF-Expert Member
Joined
Nov 29, 2013
Posts
2,029
Reaction score
1,201
Ndugu zangu wazanzibar,Ni muda mrefu sasa tumekua ktk manung'uniko kwamba serikali ya Muungano(Tanganyika) wanatunyonya.

Kumekua na rai nyingi sana za kutaka mamlaka kamili ya nchi Zanzibar ili tujiendeshe kama nchi nje ya Jamhuri ya Muungano.

Wapo wazanzibar walofika mbali zaidi na kusema sasa Muungano basi.

1.Napenda niwaulize ndugu zangu wazanzibar kabla hatujapaza yowe la kuukataa muungano huu je tumejiandaaje kujiendesha kama nchi kamili nje ya Muungano.

2.Niwajuze wazanzibar wenzangu kelele na manung'uniko yetu yamewaamsha watanganyika sasa wako mbioni kupata nchi yao nje ya muungano.wao wamejipanga tayari kwa hilo.

3.Ndugu zangu wazanzibar kama tulikua tunafanya utani wenzetu wapo serious,kiuchumi,kisiasa.
Wamejiimarisha ktk nyanja nyingi muhimu kama nchi.JE sisi tumejiandaaje!

Rai yangu kwenu mdundo huu wa kuvunja muungano usituleweshe naona mwisho wake tutakuja kuwapigia magoti watanganyika turudiane kuungana.

Upepo wa mabadiko
Upepo wa kisiasa
Lazima tuangalie tuna vyuo vikuu,vyanzo vya mapato zanzibar,ajira,n.k
Malalamiko na manung'uniko yasio na tija hayafai.
 
hawa kina makame hata siwaelewi wanachotaka
 
Ndugu zangu wazanzibar,Ni muda mrefu sasa tumekua ktk manung'uniko kwamba serikali ya Muungano(Tanganyika) wanatunyonya.

Kumekua na rai nyingi sana za kutaka mamlaka kamili ya nchi Zanzibar ili tujiendeshe kama nchi nje ya Jamhuri ya Muungano.

Wapo wazanzibar walofika mbali zaidi na kusema sasa Muungano basi.

1.Napenda niwaulize ndugu zangu wazanzibar kabla hatujapaza yowe la kuukataa muungano huu je tumejiandaaje kujiendesha kama nchi kamili nje ya Muungano.

2.Niwajuze wazanzibar wenzangu kelele na manung'uniko yetu yamewaamsha watanganyika sasa wako mbioni kupata nchi yao nje ya muungano.wao wamejipanga tayari kwa hilo.

3.Ndugu zangu wazanzibar kama tulikua tunafanya utani wenzetu wapo serious,kiuchumi,kisiasa.
Wamejiimarisha ktk nyanja nyingi muhimu kama nchi.JE sisi tumejiandaaje!

Rai yangu kwenu mdundo huu wa kuvunja muungano usituleweshe naona mwisho wake tutakuja kuwapigia magoti watanganyika turudiane kuungana.

Upepo wa mabadiko
Upepo wa kisiasa
Lazima tuangalie tuna vyuo vikuu,vyanzo vya mapato zanzibar,ajira,n.k
Malalamiko na manung'uniko yasio na tija hayafai.

"Haa! hivi kwani kabla ya huu muungano tulikuwa tukijiendeshaje? tumetimiza miaka 50 ya uhuru na mapinduzi, hivi lengo la yote hayo tuyasalimu mamlaka yetu kwa nchi nyengine atuendeshee?

Unavyoongea ni kam Mh Nahodha, kisha anaunyemelea Urais wa Zanzibar wakati tayari hajiamini kiulinzi wala kiuchumi. Wapo wanoweza na ndio tutowaweka madarakani 2015"
 
Kuna lugha inasema " You never know the importance of a thing until you loss it" Kiingereza changu kibovu lakini nadhani nimeeleweka.

"kama tunavyoona thamani ya uhuru wetu na kujitawala wenyewe sasa. tunalazimishwa tu lakini hatupikiki chungu kimoja"
 
"Haa! hivi kwani kabla ya huu muungano tulikuwa tukijiendeshaje? tumetimiza miaka 50 ya uhuru na mapinduzi, hivi lengo la yote hayo tuyasalimu mamlaka yetu kwa nchi nyengine atuendeshee?

Unavyoongea ni kam Mh Nahodha, kisha anaunyemelea Urais wa Zanzibar wakati tayari hajiamini kiulinzi wala kiuchumi. Wapo wanoweza na ndio tutowaweka madarakani 2015"


Hapo kwenye bluu; let's be serious, Muungano ulizaliwa not more than three months baada ya Mapinduzi. Hii inamaanisha kwamba Zanzibar iliwahi kusimama yenyewe kama taifa huru (nje ya Muungano) kwa kipindi kisichozidi miezi mitatu tu! Kabla ya hapo Mamlaka ya Zanzibar yalikuwa chini ya Mkoloni (mwarabu) tangu 1840 - 12th Jan. 1964 yaani kwa miaka 124.

Hivyo, kusema kwamba "kabla ya muungano" Zanzibar iliishije; jibu ni rahisi; YALIKUWA MAISHA YA UKOLONI WA KIARABU, labda ndio aina ya maisha wengine mnayotamani kuishi. Vinginevyo nakubaliana na mleta mada kwamba nje ya Muungano Zanzibar inatakiwa "kuanza upya" kwani kabla ya hapo Zanzibar kama taifa huru "haikuwahi kuwa na chochote" na sio kutuletea majibu mepesi na ya kijinga eti "kabla ya muungano ilikuwaje" kana kwamba Muungano ulikuja muda mrefu baada ya Zanzibar kuwa taifa huru!
 
Ndugu zangu wazanzibar,Ni muda mrefu sasa tumekua ktk manung'uniko kwamba serikali ya Muungano(Tanganyika) wanatunyonya.

Kumekua na rai nyingi sana za kutaka mamlaka kamili ya nchi Zanzibar ili tujiendeshe kama nchi nje ya Jamhuri ya Muungano.

Wapo wazanzibar walofika mbali zaidi na kusema sasa Muungano basi.

1.Napenda niwaulize ndugu zangu wazanzibar kabla hatujapaza yowe la kuukataa muungano huu je tumejiandaaje kujiendesha kama nchi kamili nje ya Muungano.

2.Niwajuze wazanzibar wenzangu kelele na manung'uniko yetu yamewaamsha watanganyika sasa wako mbioni kupata nchi yao nje ya muungano.wao wamejipanga tayari kwa hilo.

3.Ndugu zangu wazanzibar kama tulikua tunafanya utani wenzetu wapo serious,kiuchumi,kisiasa.
Wamejiimarisha ktk nyanja nyingi muhimu kama nchi.JE sisi tumejiandaaje!

Rai yangu kwenu mdundo huu wa kuvunja muungano usituleweshe naona mwisho wake tutakuja kuwapigia magoti watanganyika turudiane kuungana.

Upepo wa mabadiko
Upepo wa kisiasa
Lazima tuangalie tuna vyuo vikuu,vyanzo vya mapato zanzibar,ajira,n.k
Malalamiko na manung'uniko yasio na tija hayafai.
Zanzibar na hali yake huku Tanganyika inafahamika na kueleweka fika, zadi ya hilo kelele zenu na manung'uniko yasio isha, amayo hata CCM haikuyakemea yamewaamsha wenzenu hisia ya uTanganyika.

Mtikila alikuwa akionekana msema ovyo sasa ameeleweka.

Naona umekuwa makini kuonyesha ukweli kuwa matatizo ya muungano wazanzibari wengi wakifikiri ni kutokana na Tanganyika, kumbe ni dhana potofu.

Hata hivyo kwa sasa hivi ni almost too late, Watanganyika wengi wameuchoka meengano, na wako wengi hata ikipigwa kura leo watautosa!

Kitu cha maana ni Zanzibar kubeba na kuzitata kero zao wenyewe, wakipata mjomba wa kuzibeba kero hizo alhamdulilahi!
 
Ni kweli, miezi miwili na nusu ya uhuru ilikuwa ngumu sana kwa marehemu Karume kushikilia dola ya visiwa viwili kama nchi moja - alishalemewa sana na hatari ya vita vya wenyewe kwa wenyewe - kama historia inavyoonesha. Lakini kwa sasa mazingira ni tofauti na wakati ule tulipohitaji msaada wa Watanganyika ili kuepuka balaa baada ya Mapinduzi matukufu. Sasa tunaweza kabisa kujisimamia kama nchi. Historia imebadilika, watu wamebadilika, mazingira ya ki-dunia yamebadilika. Tunawashukuru Wabara kwa kupita nasi kipindi kile kigumu, lakini shukrani na heshima hii itapungua na kubadilika iwapo mtaendelea kufikiri mtoto akishakua anahitaji tena kutunzwa na kusimamiwa na mzazi. Mzazi mwenye busara humpa mtoto heshima na uhuru wa kujitawala muda unapofika kufanya hivyo!
 
Mada nzuri, ila kwa upande wangu naona zanzibar bado haijakamilika kuwa dola huru kwa sasa, nahisi umuhimu wa muungano hawawezi kuuona mpaka hapo watakapojitoa ndo watabaini mapungufu makubwa ya zanzibar iliyo kamili, angalizo sipo upande wa kulazimisha muungano uendelee ila ni maono binafsi na muda ambao wazenji wanalalama wangetumia kuandaa na kujipanga kikamilifu na maisha nje ya muungano. Nawasilisha.
 
ka nchi kenyewe sawa na wilaya ya chunya aache waende wanajiona waarab zaid,idad yao sawa 2% ya watanganyka lakn wana kelele
 
ka nchi kenyewe sawa na wilaya ya chunya aache waende wanajiona waarab zaid,idad yao sawa 2% ya watanganyka lakn wana kelele

Ndugu ukubwa wa eneo ktk nchi ama wingi wananchi si hoja madhubuti ya kuiona nchi haiwezi kujitawala.
Zipo nchi zenye wakazi chini ya milion 1 na zina utawala kamili kama nchi.
Hoja hapa Wazanzibar huu si muda wa malalamiko tu, ni wakati pia ma kuweka mikakati tunajipangaje kama nchi kua nje ya muungano?
Naamini huu moto tuliouwasha sisi kwa makele wenzetu watanganyika wanajiandaa kimyakimya.
 
Ni kweli, miezi miwili na nusu ya uhuru ilikuwa ngumu sana kwa marehemu Karume kushikilia dola ya visiwa viwili kama nchi moja - alishalemewa sana na hatari ya vita vya wenyewe kwa wenyewe - kama historia inavyoonesha. Lakini kwa sasa mazingira ni tofauti na wakati ule tulipohitaji msaada wa Watanganyika ili kuepuka balaa baada ya Mapinduzi matukufu. Sasa tunaweza kabisa kujisimamia kama nchi. Historia imebadilika, watu wamebadilika, mazingira ya ki-dunia yamebadilika. Tunawashukuru Wabara kwa kupita nasi kipindi kile kigumu, lakini shukrani na heshima hii itapungua na kubadilika iwapo mtaendelea kufikiri mtoto akishakua anahitaji tena kutunzwa na kusimamiwa na mzazi. Mzazi mwenye busara humpa mtoto heshima na uhuru wa kujitawala muda unapofika kufanya hivyo!


Angalau umekiri "kipindi kile" hamkuweza kujisimamia kama nchi na hilo halina ubishi. Lakini tatizo linakuja pale ambapo baadhi yenu hamuishi kuitukana Tanganyika kila uchao pamoja na fadhila zote mlizotendewa. Chini ya mbingu ni mahali gani ambapo mZanzibari anaishi kwa uhuru tena bila nyaraka zozote za uraia kama Tanganyika? Ni wapi anapoweza kumili rasilimali zikiwamo ardhi, biashara, na nafasi nyingine za ajira kama Tanganyika?

Ni wapi pengine mZanzibari anaweza kuwa hadi Rais wa nchi, Makamu wa Rais, Waziri Mkuu, Waziri, mbunge, na nafasi nyingine lukuki za uongozi kama Tanganyika? Ni Uarabuni? Ulaya? Marekani? Uchina? Ushelisheli? Labda Mzee Barubaru atatuhadithia huko Oman aliko ana nafasi gani ya uongozi wa nchi ile ya kufikia. Au ni wapi Afrika ambako hilo linaweza kutokea? Hiyo nchi haipo na haitakaa iwepo baada ya Muungano huu ambao kimsingi umefikia "point of no return".

Nakubaliana na wewe kwamba mtoto akikua anastahili kuachwa ajitegemee; sawa, ila kinachokera ni jinsi mtoto huyu mpu.mba.vu tena wa kufikia asivyo na adabu kwa mzazi wake aliyemlea kwa jasho na damu. Kama wewe una dini naamini unajua dini zinasemaje kuhusu mtoto wa aina hii! Laana i miguuni pake!
 
Last edited by a moderator:
Ndugu ukubwa wa eneo ktk nchi ama wingi wananchi si hoja madhubuti ya kuiona nchi haiwezi kujitawala.
Zipo nchi zenye wakazi chini ya milion 1 na zina utawala kamili kama nchi.
Hoja hapa Wazanzibar huu si muda wa malalamiko tu, ni wakati pia ma kuweka mikakati tunajipangaje kama nchi kua nje ya muungano?
Naamini huu moto tuliouwasha sisi kwa makele wenzetu watanganyika wanajiandaa kimyakimya.


Tena Mkuu mjipange kwelikweli vinginevyo msijetoa machozi mtakaposikia "Amri ya Masaa 48". Ni ushauri tu.
 
Hapo kwenye bluu; let's be serious, Muungano ulizaliwa not more than three months baada ya Mapinduzi. Hii inamaanisha kwamba Zanzibar iliwahi kusimama yenyewe kama taifa huru (nje ya Muungano) kwa kipindi kisichozidi miezi mitatu tu! Kabla ya hapo Mamlaka ya Zanzibar yalikuwa chini ya Mkoloni (mwarabu) tangu 1840 - 12th Jan. 1964 yaani kwa miaka 124.

Hivyo, kusema kwamba "kabla ya muungano" Zanzibar iliishije; jibu ni rahisi; YALIKUWA MAISHA YA UKOLONI WA KIARABU, labda ndio aina ya maisha wengine mnayotamani kuishi. Vinginevyo nakubaliana na mleta mada kwamba nje ya Muungano Zanzibar inatakiwa "kuanza upya" kwani kabla ya hapo Zanzibar kama taifa huru "haikuwahi kuwa na chochote" na sio kutuletea majibu mepesi na ya kijinga eti "kabla ya muungano ilikuwaje" kana kwamba Muungano ulikuja muda mrefu baada ya Zanzibar kuwa taifa huru!

"na iwe hivyo, kwani hayakuwa maisha wakati wa huo wa ukoloni?, ndio wakati huo hata kina Ali Hassan Mwinyi, Aboud Jumbe, Salmin Amour, wazee wangu walisoma, wakitibiwa bure na kijujumla maisha yao yakienda vizuri tu kuliko tulivyo sasa chini ya huu ukoloni wa Tanganyika (mkoloni mwafrika). Na tupo tayari kuanza upya kwa hivyo uonavyo wewe."
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom