Way forward 2018-2020

Way forward 2018-2020

Hapana tuwe wakweli ccm ya sasa ni imara kweli? Hapana kabisa, imeendelea kuwa majeruhi
Mshana una umri gani? labda umeanza kupiga kura mwaka 2015 maana huko nyuma ulikuyashule ya msingi. Mwaka 1995 CCM ilipigwa vijembe mpaka na mwanzilishi wake Mwalimu Nyerere. Msioijua CCM jaribuni kuacha maneno ya akiba kwaajili ya 2020.
 
Kweli mshana utawala umefitinika........kuna watanzania ambao hawawezi kumuazima mtu akili zao...........Kwani hela nani kasema ni kila kitu.,?!
 
Mshana una umri gani? labda umeanza kupiga kura mwaka 2015 maana huko nyuma ulikuyashule ya msingi. Mwaka 1995 CCM ilipigwa vijembe mpaka na mwanzilishi wake Mwalimu Nyerere. Msioijua CCM jaribuni kuacha maneno ya akiba kwaajili ya 2020.
Aisee naona uko mbali na ukweli.. Wakati Mchonga anaachia ngazi 1984 ulikuwa wapi? CCM ilitikiswa haswa uchaguzi uliopita kuliko wakati mwingine wowote... Na kama sio kutumia mbinu chafu kabisa leo hii ingekuwa haipo madarakani
 
Mshana una umri gani? labda umeanza kupiga kura mwaka 2015 maana huko nyuma ulikuyashule ya msingi. Mwaka 1995 CCM ilipigwa vijembe mpaka na mwanzilishi wake Mwalimu Nyerere. Msioijua CCM jaribuni kuacha maneno ya akiba kwaajili ya 2020.
Unawaza 1995? hamia digitali mkuu ccm wanapumulia mashine
 
Aisee naona uko mbali na ukweli.. Wakati Mchonga anaachia ngazi 1984 ulikuwa wapi? CCM ilitikiswa haswa uchaguzi uliopita kuliko wakati mwingine wowote... Na kama sio kutumia mbinu chafu kabisa leo hii ingekuwa haipo madarakani
Ni vizuri sana umejijibu mwenyewe. Kama ilishindikana huko nyuma kipi kinakupatia nafasi kudhani wataweza wakati huu? Ubaya wa upinzani ni kwamba hawapo wamoja na hakuna nidhamu lakini wenzao CCM pamoja na ubaya wao wapo kama mafia hawacheki na ujinga inapokuja kuki save chama chao. Lowasa alikua na watu wengi sana wakati wa mchujo mpaka waliimba Lowasa sema, walipokemewa walikaa kimya. nani alimfuata Lowasa CDM? Ningependa sana CCM isambaratike lakini moyo unaona bora hili jini tulijualo kuliko watu kama CDM wasiokua na msimamo leo wanamsema mtu ni fisadi kesho wanampakata.
 
Unawaza 1995? hamia digitali mkuu ccm wanapumulia mashine
Seriously anataka kuilinganisha ccm ya 1995 na ya sasa kwa hoja kwamba Mchonga aliisimanga? Zimwi likujualo halikuli likakwisha Mchonga asingekubali ccm ife
 
Mshana nakuelewa Sana lakini Kati ya vitu ambavyo vinanipa shida Ni pamoja na kuamini kuwa mwiguli kabanwa na atakimbilia upinzani..kati ya watu ambao najua nje ya ccm hawawezi Ku survive Ni mwigulu..na aitoka ccm atakua mnafiki kuliko polepole
Mwigulu atakimbia tuu ccm, hata kama hawezi kuja Chadema lakini anaweza kwenda chama kingine. Hali ya Mwigulu ndani ya kile chungu ni chungu, unaambiwa manyanyaso anayopata amebakia kubabuliwa vibao tuu na mzee. Hapendwi kabisa na yupo yupo tuu.
 
Unawaza 1995? hamia digitali mkuu ccm wanapumulia mashine
Mlisema hivyo mwaka 2020. Mimi na ndugu zangu wengine tuliacha kuongea sababu nilikua nawakumbusha sana kuhusu 1995 na wakasema 2015 haikua 1995. Nikawaambia wajifikirie sana siyo kupenda kwa jazba. 2020 CCM itashinda, Ujinga walioufanya Upinzani utawafuata miaka yote na kutousikiliza ushauri wa mchonga.

NCCR pekee ingewafanya washinde uchaguzi na hapa sizungumzii NCCR Mageuzi nazungumzia ile NCCR tuliyofanya mkutano wa kwanza Diamond Jubelee kudai katiba mpya. Ndoto za kuishinda CCM ziliishia mwaka 1995 tulipokubali kuingia uchaguzi kwa katiba ya CCM.....
 
Ni vizuri sana umejijibu mwenyewe. Kama ilishindikana huko nyuma kipi kinakupatia nafasi kudhani wataweza wakati huu? Ubaya wa upinzani ni kwamba hawapo wamoja na hakuna nidhamu lakini wenzao CCM pamoja na ubaya wao wapo kama mafia hawacheki na ujinga inapokuja kuki save chama chao. Lowasa alikua na watu wengi sana wakati wa mchujo mpaka waliimba Lowasa sema, walipokemewa walikaa kimya. nani alimfuata Lowasa CDM? Ningependa sana CCM isambaratike lakini moyo unaona bora hili jini tulijualo kuliko watu kama CDM wasiokua na msimamo leo wanamsema mtu ni fisadi kesho wanampakata.
Hapana sijajijibu ila wewe ndio umeshindwa kunijibu.... Na woga wako huo ndio unakufanya ushindwe kuchukua maamuzi sahihi kwa wakati sahihi
 
Seriously anataka kuilinganisha ccm ya 1995 na ya sasa kwa hoja kwamba Mchonga aliisimanga? Zimwi likujualo halikuli likakwisha Mchonga asingekubali ccm ife
Lakini kwa hali ya sasa Mkwere na Kipipa wanaweza iacha ccm ijifie kwani ni mawili. Eitha kumuondoa mwenyekigoda ili kuponya chama au kuacha chama kianguke ili kumhimili mwenye kigoda.
Hiyo ya kwanza itakuwa hatari sana kwa Mkwere & co kwani mwenye kigoda hawezi kukubali wamuondoe la sivyo Nissan patrol zaweza kutumika
 
Mwigulu atakimbia tuu ccm, hata kama hawezi kuja Chadema lakini anaweza kwenda chama kingine. Hali ya Mwigulu ndani ya kile chungu ni chungu, unaambiwa manyanyaso anayopata amebakia kubabuliwa vibao tuu na mzee. Hapendwi kabisa na yupo yupo tuu.
Aliambiwa hivi na Bob.... Tena wee kaa kimya kabisa.. Unadhani sikujui?! Loh jamaa akawa mpole kama maiti kumbe wanajuana huko kwenye ulingo wa hujuma na kuhujumiana
 
Seasonal migration kwenye ulingo wa siasa imeanza... Moja inafanyika kwa hiari na uamuzi binafsi nyingine ni nguvu ya shekeli na ahadi ya kazi na madaraka

Hongera Nyalandu Kwa kumchapa kofi yule mjamaa.. It was a very calculated timing....! Umefanya kusudi ili upime ubavu kati ya tukio lake na lako lipi litafunika... Lipi litapata kiki... siasa bhana.....!!!

CCM imepata pigo lingine jana.. Pigo kubwa... Ile hotuba imewasononesha wengi, kwamba wale wakazi 3000 waliovamia maeneo sensitive ya jeshi la polisi na jeshi la ulinzi pamoja uwanja wa ndege wasibomolewe nyumba zao kwakuwa MWANZA ndio walimpa kura..
Kuna watu wamepata kinga ya kutochukuliwa hatua za kisheria kwakuwa tu walimpa mkulu kura... Poleni ccm... Kiza kimetanda ndani ya chama... Na hakuna mwenye nyongo ya kuongea tena! Mwigulu na Kinana wanajua vema
Mchoko na kukata tamaa sasa ni dhahiri shahiri ndani ya chama dume na wenye kujitambua wameanza kuchukua hatua mapema.... Kujitenga na giza
Ukiachana na kizungumkuti cha uchaguzi 2020 kama utakuwepo ama la., lakini ccm itapukutika wanachama wake mahiri kuelekea 2020 na hawatakuwa na kimbilio lingine zaidi ya CHADEMA japo na mapandikizi yatakuwepo
Kuna tofauti kubwa ya mapenzi ya kweli hata kama mtu alikuwa changu na mapenzi ya pesa hata kama mtu alikuwa mlokole... CHADEMA itashutumiwa sana kupokea mafisadi, kupokea watuhumiwa wa kashfa mbalimbali, kupokea wachafu wa ccm... Lakini najua hawatayumba kwakuwa ufalme umefitinika....
Wadanganyika walikosea pale walipokataa kufuata ushauri wa hayati baba wa Taifa. Alishauri siku nyingi zilizopita tusije kuchagua raisi anayetoka makabila fulanifulani kwani wana matatizo ya asili ya kuzaliwa ni - lazima watatuletea matatizo sasa mwayaona vumilieni. Wa Dsm wabomolewe tu wameingia rizevu ya barabara, wa Mwanza hapana msiwabomolee walinipa kura. 'hata mkirifunga ribarabara wakafanya biashara kuna tatizo gani, ribarabara linatakiwa liwasaidie wananch'i.Mchome (Dr. anayefanya kazi mkoani Dsm) afukuzwe kazii ana cheti feki, Makonda anafanya kazi vizuri sana endelea sisikii wala sioni vyeo vya siasa havihitaji cheti cha fomu fo.
 
Wadanganyika walikosea pale walipokataa kufuata ushauri wa hayati baba wa Taifa. Alishauri siku nyingi zilizopita tusije kuchagua raisi anayetoka makabila fulanifulani kwani wana matatizo ya asili ya kuzaliwa ni - lazima watatuletea matatizo sasa mwayaona vumilieni. Wa Dsm wabomolewe tu wameingia rizevu ya barabara, wa Mwanza hapana msiwabomolee walinipa kura. 'hata mkirifunga ribarabara wakafanya biashara kuna tatizo gani, ribarabara linatakiwa liwasaidie wananch'i.Mchome (Dr. anayefanya kazi mkoani Dsm) afukuzwe kazii ana cheti feki, Makonda anafanya kazi vizuri sana endelea sisikii wala sioni vyeo vya siasa havihitaji cheti cha fomu fo.
Rest in piece Mchonga meno na maono yanayotimia.. Ni unabii wa ajabu yule Mzee alikuwa kiona mbali
 
But you sense the trending

Bro, How I wish I could agree with your prophesy! I see the trend but trending to where???

Kwa hizi akili za waTanzania ninaowajua.....Aisee bado sana. Bado sana.

Ndo maana ukikaa ukiwaza..bado ukweli ni kwamba kuanzia nyumba kumi mpaka WMK....survival yao wanaitegemea kwa bwana yuleeeee! wachache watadiriki kuuma mkono unaowalisha.

Ndo maana mtu kama Lazarus I believe ameshajiandaa vilivyo kupambana na watu wasiojulikana. Mkuu wenye roho ya TL na wenzake ni wachache mnoooo! Mageuzi Africa yana safari ndefu mno!

Ukiwasikia majukwaani wakimuongelea Mwalimu JKN..unajiuliza hivi Nyerere ange-behave kama wao TZ ingekuwa wapi? au wao ndo wangetuongoza kipindi cha Mwalimu tungekuwa wapi?

Tanzania imebaki na wanasiasa wachache sana kama wapo. Majority waliobaki ni wachumia tumbo tuu ambao wala hata siasa hawaijui. They have no principles to stand for.

So many uncertainties bro!
 
Bro, How I wish I could agree with your prophesy! I see the trend but trending to where???

Kwa hizi akili za waTanzania ninaowajua.....Aisee bado sana. Bado sana.

Ndo maana ukikaa ukiwaza..bado ukweli ni kwamba kuanzia nyumba kumi mpaka WMK....survival yao wanaitegemea kwa bwana yuleeeee! wachache watadiriki kuuma mkono unaowalisha.

Ndo maana mtu kama Lazarus I believe ameshajiandaa vilivyo kupambana na watu wasiojulikana. Mkuu wenye roho ya TL na wenzake ni wachache mnoooo! Mageuzi Africa yana safari ndefu mno!

Ukiwasikia majukwaani wakimuongelea Mwalimu JKN..unajiuliza hivi Nyerere ange-behave kama wao TZ ingekuwa wapi? au wao ndo wangetuongoza kipindi cha Mwalimu tungekuwa wapi?

Tanzania imebaki na wanasiasa wachache sana kama wapo. Majority waliobaki ni wachumia tumbo tuu ambao wala hata siasa hawaijui. They have no principles to stand for.

So many uncertainties bro!
b400d0d1e30299e798a30ad54a685dc6.jpg
I can see your point Masanja
 
Seasonal migration yatakuwepo

Kuna tofauti kubwa ya mapenzi ya kweli hata kama mtu alikuwa changu na mapenzi ya pesa hata kama mtu alikuwa mlokole... CHADEMA itashutumiwa sana kupokea mafisadi, kupokea watuhumiwa wa kashfa mbalimbali, kupokea wachafu wa ccm... Lakini najua hawatayumba kwakuwa ufalme umefitinika....
mkuu mimi naamini kupitia haya makosa ya mkuu wao, Nchi inaenda kupata ukombozi wa kweli, upinzani wa kweli utatoka SISIEMU, aliwahi kusema Nyerere.
 
Back
Top Bottom