Hata oparesheni haikuwa shangwe ila Matokeo yake leo tunayafurahia. Baba yangu alinyang'anywa mashamba bila fidia. Tulilalamika sana. Fidia tuliyopata ni kufutwa tabu ya watoto kutembea km 8 asubuhi na 8 jioni kwenda shule ya Msingi. Wadogo zangu na wanangu hawaamini kuwa tulitembea km 16 kila siku ya shule,suluhu ilikuwa oparesheni vijiji. Naungana na wanaowahurumia wajane,wagane,wazee vikongwe na wagonjwa badala ya kulaumu tujitolee kuwasaidia. Tunachangia harusi kwenda kula sahani moja ya chakula na bia 2 au 3 kwa kutoa laki moja bibi na bwana. Tuwachangie walioathirika kupata viwanja vilivyopimwa. Tujitokeze kuchangia ,lkn ubomoaji uendelee.