Wauza sura Mlimani City

Wauza sura Mlimani City

Wazungu wanaita window shopping, kuingia dukani sio lazima uwe na hela ya kununua kuna kitu kinaitwa customer behaviour unafanya research kabla hujafanya maamuzi sio kila mtu muuza sura wengine wanafanya tafiti zao

Inamaana wewe ni mdhungu maana umekoti sana.!
 
Tanzani sijaona sehemu ya kupumzisha akili watakuja watu hapa watakuambia bar, sijui hotel tembeeni kwa wenzenu ulaya huko kuna sehemu zimetengwa kwa ajili ya kuipa akili afya unakutana na maua mazuri miti ya kijani, ukoka uliokatwa madadi, kiyoyozi cha Mungu, muziki wa ndege sio huku magomeni, eti mnazi mmoja ndio garden za kupumzikia, hizo beech zetu ndio majanga .

karibu mombasa mkuu,mi nimeamua kujiongeza kuja huku kenya.nauli 40000tsh au 2000ksh kwa tahmeed au ratco luxury
 
Umeanza! Nakwambia umeanza uchokozi. Kama unataka uhamishwe jiji la DSM, gusa maisha ya 'watu wa Mlimani city'!
 
Ulikua unataka watu waende Mlimani city kufanya nini Labda?! Tuanzie hapo
 
Mkuu mambo ya Mall hayo labda wakati wanazunguka zunguka wanasubiri kuingia movie si unajua kuna kumbi za cinema.
 
karibu mombasa mkuu,mi nimeamua kujiongeza kuja huku kenya.nauli 40000tsh au 2000ksh kwa tahmeed au ratco luxury
Mkuu al shabaab si ndio gumzo huko. Nisalimie wale wadada wa kutoa hudma ya massage pale florida
 
Siku zote humu watu wanaleta nyuzi kuhusu maisha kwamba kabla ya kufanya kitu unatakiwa ujipange usikurupuke, kwahiyo ukiwa huna hela haina maana usipite kwenye maduka hata kushangaa tu maana kwa kupita kwao hapo maana yake tayari ameshaona vitu flani flani na endapo anapata hela tu anafanya maamuzi tofauti na mleta uzi ambae unajiona una issue ukiingia pale lazima kuna kubambikwa.
 
huo sasa wivu
afu hujui wengi wa unao waona pale wanakuwa wanasubiria kuingia movie na hii mtu akifika mapema anasubiria muda wa muvi anayotakia ufike aingie. Kula ice cream ni jambo la kawaida sana wakti mtu anasubiria muvie time.

afu wewe jali yako ulokwena na fuko la kazi maalum huko, wenzio ata tu kutizama wanaopita kwao ni sehem ya mapumziko.

afu nakushangaa ivi kama ndo unakazi nyingi kama unavyojitanabahisha apa unapata wapi muda wa kutizama wengine?

simple mind hii, na wee ni mmojawapo wa wauza sura hao
Wengine wanajua ku-relax mpaka ukae sehemu utumie hela kumbe hata kupanda gari tu ukaamua kwenda Gongolamboto na kurudi bila issue ya kufanya kule nayo ni ku-relax au kwenda Mliman City na kuangalia hiki na kile hata kama mfukoni una mia tano.
 
Wengine wana job hapo mall then ww unadai wazururaji.
 
Jamani nimegundua watu wengi wanaoenda Mlimani City wanakuwa hawana issue ya maana zaidi ya kwenda kuuza sura.

Iko hivi, ukifika Mlimani City utawakuta mabrazamen na masista duu kibao wanatembeatembea tu bila mpango wowote atashangaa hiki mara kile atakaa chini anapiga miayo ya njaa mara atajifanya yupo bize na kismart phone cha mchina kumbe hakina salio lolote,baada ya muda watanunua ice cream za watoto watalambalamba.

Wakimaliza kuuza sura wataondoka zao.

Wakuu mkitaka kuamini nendeni Mlimani City mtawaona .

Jamani nendeni Mlimani City mkiwa na issue za maana na sio kuuza sura tu.

Ipo siku watakuja kuuza jicho.
 
Back
Top Bottom