Wauguzi wawili hospitali ya Mpwapwa wasimamishwa kazi kwa kusababisha kifo cha kichanga

Chachu Ombara

JF-Expert Member
Dec 11, 2012
5,897
10,358
Wauguzi wawili wa hosipitali ya wilaya ya Mpwapwa wamesimamishwa kazi kwa tuhuma za uzembe uliosababisha kifo cha kichanga tumboni kwa mama aliyefahamika kwa jina la Rehema Amos kutokana na kucheleweshewa huduma alipofika hospitalini hapo kujifungua.

Mkuu wa Wilaya ya Mpwapwa Mohammed Utaly ametoa agizo kwa watumishi hao kusimamishwa alipotembelea hospitali hiyo kufuatia tukio hilo ambapo inadaiwa wakiwa zamu kwenye wodi ya wajawazito kwa makusudi walifanya uzembe kwa kuchelewesha huduma hali iliyochangia kichanga cha mama huyo kufia tumboni huku akiunda tume ya watu watano kwa ajili ya kuchunguza tuhuma hizo.

Kwa upande wao wauguzi walipokutwa na tuhuma hizo Adam Mwampashi na Pendo chibutu wakizungumza na jopo lililoongozana na mkuu wa wilaya wakekiri kumuhudumia mama huyo wakati wa kijifungua huku wakikanusha madai ya kuhusika na kifo cha kichanga hicho.

Mganga Mkuu wa hosipitali hiyo Dk. Said Mauji amesema uongozi utashirikiana na tume hiyo bega kwa bega ili hatua zaidi kwa watumishi hao zichukuliwe endapo watabainika kuwa na hatia
 
Nashauri serikali ijitahidi kuajiri wauguzi na wakunga wa kiume wengi kuliko wa kike maana wanawake ni wakatili na wenye roho mbaya sana kwa wanawake wenzao.
 
mie mke wangu akienda kujifungua halafu muuguzi kwa uzembe wake akasababisha mambo yakaenda hovyo kwakeli nahisi nitapelekwa segerea....

Eeeeh Mungu pitisha hii mbali
 
Weka identity yako tukufuatilie tuone utafanya nini if at it happens to your wife! though we do not pray for that anyway
 
Adhabu iwe ni kifungo cha maisha kwa kusababisha vifo kwa watoto wasio na hatia

Yan mtu ubebe mimba miez tisa halafu kwa uzembe WA muuguz mtoto afe... Aisee inauma sana
 
Kusimamishwa peke ake haitoshi.

Hao ni wauaji.

Sijui kwanini baadhi ya wauguzi wanakuwa na roho mbaya, utafikiri wao hawana watoto!

Mpaka unaingia mkataba kazi ya uuguzi, ni pamoja na kuwa mvumilivu, mnenyekevu kwa mgonjwa.

Au hawa wajinga wajinga wetu hawapewi elimu hiyo?

Au ni dharau, na kujisikia baada ya kupata kibarua!

Utu ni kitu muhimu sana, acheni dharau
 
Wauguzi si wote wanarohombaya ila kunawengine wanawaalibia wenzao ila wengi wana roho mbaya ,kuna mmoja pale mwananyamara nilienda kujifungua miaka 6 iliyopita nilikuwa tayali kujifungua nilimwambia anipeleke chumba cha kuzalia akakataa akang'ang'ani kunipima anasema bado, uchungu ulinizidia Nilikuwa sioni macho yalipofuka ghafla kilanikijaribu kufumbua macho jicho linazunguka ata sijui mahusiano ya macho na uzazi.nilijikaza nikashuka kitandani na kumuaidi nesi naenda mwenyewe nilienda naisia huku nikipapacha mpaka chumba cha kuzalia peke yangu na niumbali kidogo kutoka chumba nilichokuwepo ,kule manesi wa kule wakanishangaa kuja peke yangu bila nesi na kunisaidia kupanda kitandani Mara yule nesi nae kwa aibu alikuja na vifaa vyangu wakaangalia likodi yangu ya uchungu wakaona nilikuwa tayali yule nesi wa chumba cha pili alimsema yule nesi mpaka nikagundua kumbe kuna manesi wengine wana roho nzuri, nilivyojifungua nilirudi kuchukua nguo zangu nilipewa pole na wagonjwa wenzangu kumbe nao walikuwa wanauona uzembe unavyo fanyika waliogopa kumkosoa nesi nae nilimkuta aliinamia kichwa chini .lakini nimemsamehe alikuwa anafanya Nazi kwa mazoea ikiwa kwenye ubao liliandikwa jina langu mgonjwa serious. Lakini alizembea.kunabaadhi ya manesi wanaroho mbaya .
 
Naomba wafukuzwe kabisa hao manesi, kwa sisi tulio wahi kuwa wahanga katika hili tunaelewa ni jinsi gani hili jambo linauma katika maisha ya binadamu
 
Hao manesi wawezakuta hata hawajausika na kifo hicho,ngoja tume italeta majibu sahihi tusubiri,tuache siasa ktk matibabu jamani.
 
Back
Top Bottom