Kiukweli baada ya uvumilivu wa Muda mrefu nimeona bora kusema tu kweli kuhusu hawa waturuki wanaojenga SGR, sitaki kubase sana kwenye efficiency yao ya kazi ila nataka niweke wazi kwenye swala la socialization na sisi watanzania.
Wamekua ni watu wakatili na wakorofi sana inapokuja kwenye swala la haki ya mfanyakazi wanawapiga ndugu zetu site bila sababu na endapo ukajaribu kujibu mashambulizi wanakufukuza kazi.
Hivi majuzi nimeshuhudia mtu amefukuzwa kisa tu amekutwa amemsaidia dereva gari baada ya dereva kuumwa ghafla wakiwa site .