Watumiaji wa Mitandao ya Simu Tudhihirishe Nguvu ya Wateja

Bams

JF-Expert Member
Oct 19, 2010
16,505
41,013
Tangu kesi dhidi ya Mbowe, inayojulikana kama kesi ya mchongo au kesi kubambikia ianze, imedhihirika wazi pasipo shaka namna baadhi ya makampuni ya simu za mkononi yanavyoshirikiana na Polisi waovu dhidi ya wateja.

Mwanasheria wa kampuni ya Tigo na Airtel, wote kwa nyakati tofauti walieleza jinsi wanavyotoa taarifa za wateja hovyo, alimradi tu wameona barua yenye nembo ya jeshi la Polisi huku wakiacha kujishughulisha kabisa kulinda haki za wateja wao wala kutaka kujua taarifa za mteja zinaombwa kutokana na kosa gani. Kwao Polisi ndiyo kila kitu, wateja ni takataka.

Kutokana na ukweli huu, wateja ni lazima tulipinge hili kwa vitendo. Tufanye yafuatayo,na mengine uatakayoonekana yanafaa:

1) Sisi wenye line za Airtel, kwa vile wengi tuna lines zaidi ya moja, tusitumie line ya Airtel angalao kwa mwezi mmoja. Kama unalazimika, basi tumia pale tu ambapo huna namna nyingine.

2) Kwa uhakika mitandao karibia yote ya simu, ukiondoa Halotel na Zantel (hakuna ushahidi), siyo salama. Itumie kwa tahadhari kubwa hata kama mawasiliano yako hayana uovu wowote. Hawa jamaa hutengeneza uovu kisha wanausukumiza kwako alimradi mazingira yaruhusu. Tumia sms na calls za kawaida kwa mambo ambayo ni ya kawaida sana na yaliyo wazi. Mambo ambayo unadhani ni serious au confidential tumia whatsap, viber au skype.

Mawasiliano hata huko kwenye nchi zilizoendelea, yanakuwa monitored kwa sababu za kiusalama, lakini kwetu yanakuwa monitored kwaajili ya kuwakomoa au kuwabambikia watu kesi.
 
Tujiridhishe kwanza wakati Airtel wanaomba kuoperate Tanzania Leseni yao ilikuwa na masharti yao.

Lakini pia, Je ni kweli ukiwa mhalifu na Serikali au vyombo vya usalama wanahitaji taarifa za uhalifu wako basi sheria haiwaruhusu kupewa?

Hebu tujadili kwanza nafasi yatunaowatuhumu kwa maana ya makampuni ya simu kabla ya sisi pia kutoa hukumu.

Ni mtazamo wangu tu.
 
tujiridhishe kwanza wakati Airtel wanaomba kuoperate Tanzania Leseni yao ilikuwa na masharti yao..

Lakini pia, Je ni kweli ukiwa mhalifu na Serikali au vyombo vya usalama wanahitaji taarifa za uhalifu wako basi sheria haiwaruhusu kupewa..?

Hebu tujadili kwanza nafasi yatunaowatuhumu kwa maana ya makampuni ya simu kabla ya sisi pia kutoa hukumu...

Ni mtazamo wangu tu...

Hakuna anayekataa taarifa za wahalifu kutolewa kwa mamlaka husika, ila sio kwa lengo la kumkomoa mteja. Kinachoendelea kwenye hiyo kesi ya Mbowe, makampuni yote yaliyopeleka ushahidi hadi sasa yanaonyesha yanatoa taarifa kwa shinikizo la kukomoana, na hayo makampuni yote yanajua fika yanatumika kutengeneza ushahidi wa kukomoana kisiasa. Mashahidi wote wawili wanatoa ushahidi wa wazi wa kutengeneza.
 
tujiridhishe kwanza wakati Airtel wanaomba kuoperate Tanzania Leseni yao ilikuwa na masharti yao..

Lakini pia, Je ni kweli ukiwa mhalifu na Serikali au vyombo vya usalama wanahitaji taarifa za uhalifu wako basi sheria haiwaruhusu kupewa..?

Hebu tujadili kwanza nafasi yatunaowatuhumu kwa maana ya makampuni ya simu kabla ya sisi pia kutoa hukumu...

Ni mtazamo wangu tu...
Inashamgaza kuona huna uelewa hata ule wa msingi:

1) Makampuni yote yanalazimishwa na sheria kulinda siri za mteja

2) Vyombo vya usalama vinapohitaji taarifa kutoka kwenye makampuni haya kwa sababu za kiusalama, makampuni haya yamepewa haki ya kukubali au kukataa kutegemeana udhahiri wa sababu ambazo kwazo taarifa za kteja zinaombwa. Vyombo vya ulinzi na usalama vikikataliwa, vinalazimika kuomba order ya mahakama. Lakini pia hawa service providers wana uwezo wa kukataa na kuomba kinga ya mahakama.

3) Mtandao wa simu ukigundua mteja wao anataka kuingiliwa haki zake za msingi bila sababu zenye msingi wa kisheria,, wanatakiwa kumtaarifu mteja juu ya hatari zinazomzunguka.

4) Kama kuna namna yoyote ile mitandao ya simu ikagundua kupitia mitandao yao, kuna uhalifu unapangwa, umepangwa au umetendwa, wanalazimika kuvitaarifu vyombo vya ulinzi na usalama.

Lakini kwa yaliyotokea, ni mtu anapokea barua yenye nembo ya polisi, hapo hapo anaprint taarifa za mteja. Sasa huo siyo uwendawazimu?

Line yangu ya Airtel itapumzika kabatini kwa miezi 2.
 
Hakuna anayekataa taarifa za wahalifu kutolewa kwa mamlaka husika, ila sio kwa lengo la kumkomoa mteja. Kinachoendelea kwenye hiyo kesi ya Mbowe, makampuni yote yaliyopeleka ushahidi hadi sasa yanaonyesha yanatoa taarifa kwa shinikizo la kukomoana, na hayo makampuni yote yanajua fika yanatumika kutengeneza ushahidi wa kukomoana kisiasa. Mashahidi wote wawili wanatoa ushahidi wa wazi wa kutengeneza.
Unayoyasema ni wazi kabisa.
 
Inashamgaza kuona huna uelewa hata ule wa msingi:

1) Makampuni yote yanalazimishwa na sheria kulinda siri za mteja

2) Vyombo vya usalama vinapohitaji taarifa kutoka kwenye makampuni haya kwa sababu za kiusalama, makampuni haya yamepewa haki ya kukubali au kukataa kutegemeana udhahiri wa sababu ambazo kwazo taarifa za kteja zinaombwa. Vyombo vya ulinzi na usalama vikikataliwa, vinalazimika kuomba order ya mahakama. Lakini pia hawa service providers wana uwezo wa kukataa na kuomba kinga ya mahakama.

3) Mtandao wa simu ukigundua mteja wao anataka kuingiliwa haki zake za msingi bila sababu zenye msingi wa kisheria,, wanatakiwa kumtaarifu mteja juu ya hatari zinazomzunguka.

4) Kama kuna namna yoyote ile mitandao ya simu ikagundua kupitia mitandao yao, kuna uhalifu unapangwa, umepangwa au umetendwa, wanalazimika kuvitaarifu vyombo vya ulinzi na usalama.

Lakini kwa yaliyotokea, ni mtu anapokea barua yenye nembo ya polisi, hapo hapo anaprint taarifa za mteja. Sasa huo siyo uwendawazimu?

Line yangu ya Airtel itapumzika kabatini kwa miezi 2.

Kabisa mkuu, ni kama kuna uhusiano wa kihalifu baina ya serikali na haya makampuni ya mawasiliano. Taarifa zinatakiwa kinyume na sheria, na zinatolewa kwa kisingizio cha mamlaka husika. Kwa mtiririko wa ushahidi uliotolewa na hawa mashahidi wawili wa makampuni ya mawasiliano, unatoa viashiria vyote kuwa wanashirikiana na serikali kufanikisha lengo hili chafu la ushahidi wa kupanga
 
Nape na January wako kwenye baraza la Mawaziri labda watakuja na muswaada imara wa kulinda faragha za watumiaji simu.
 
Inashamgaza kuona huna uelewa hata ule wa msingi:

1) Makampuni yote yanalazimishwa na sheria kulinda siri za mteja

2) Vyombo vya usalama vinapohitaji taarifa kutoka kwenye makampuni haya kwa sababu za kiusalama, makampuni haya yamepewa haki ya kukubali au kukataa kutegemeana udhahiri wa sababu ambazo kwazo taarifa za kteja zinaombwa. Vyombo vya ulinzi na usalama vikikataliwa, vinalazimika kuomba order ya mahakama. Lakini pia hawa service providers wana uwezo wa kukataa na kuomba kinga ya mahakama.

3) Mtandao wa simu ukigundua mteja wao anataka kuingiliwa haki zake za msingi bila sababu zenye msingi wa kisheria,, wanatakiwa kumtaarifu mteja juu ya hatari zinazomzunguka.

4) Kama kuna namna yoyote ile mitandao ya simu ikagundua kupitia mitandao yao, kuna uhalifu unapangwa, umepangwa au umetendwa, wanalazimika kuvitaarifu vyombo vya ulinzi na usalama.

Lakini kwa yaliyotokea, ni mtu anapokea barua yenye nembo ya polisi, hapo hapo anaprint taarifa za mteja. Sasa huo siyo uwendawazimu?

Line yangu ya Airtel itapumzika kabatini kwa miezi 2.


Mteja yupi na siri zipi?..
Hizo siri zilindwe baina ya nani na nani..

Makampuni yamepewa haki ya kukubali au kukataa...sasa tunaanzaje kuilaumu Airtel ambayo imepewa haki ya kukubali au kukataa?..

Kuna haja ya kuzichimba sana hizi sheria na kupata ufafanuzi wa kitaalam usio na chembe ya siasa..
 
Hakuna anayekataa taarifa za wahalifu kutolewa kwa mamlaka husika, ila sio kwa lengo la kumkomoa mteja. Kinachoendelea kwenye hiyo kesi ya Mbowe, makampuni yote yaliyopeleka ushahidi hadi sasa yanaonyesha yanatoa taarifa kwa shinikizo la kukomoana, na hayo makampuni yote yanajua fika yanatumika kutengeneza ushahidi wa kukomoana kisiasa. Mashahidi wote wawili wanatoa ushahidi wa wazi wa kutengeneza.

Kukomoa kwa maana ya taarifa wanazotoa ni za uongo hakuna hizo communications au kutoa taarifa kwa vyombo vya dola ndio kukomoa?..

Nataka kuelewa hapo..
 
Kukomoa kwa maana ya taarifa wanazotoa ni za uongo hakuna hizo communications au kutoa taarifa kwa vyombo vya dola ndio kukomoa?..

Nataka kuelewa hapo..

Namna ya utoaji ni wenye nia ovu ya wazi. Isitoshe anatoa ushahidi kwa kuficha baadhi ya mambo kwa lengo la kufikia hitimisho lenye nia ovu.
 
Tangu kesi dhidi ya Mbowe, inayojulikana kama kesi ya mchongo au kesi kubambikia ianze, imedhihirika wazi pasipo shaka namna baadhi ya makampuni ya simu za mkononi yanavyoshirikiana na Polisi waovu dhidi ya wateja.

Mwanasheria wa kampuni ya Tigo na Airtel, wote kwa nyakati tofauti walieleza jinsi wanavyotoa taarifa za wateja hovyo, alimradi tu wameona barua yenye nembo ya jeshi la Polisi huku wakiacha kujishughulisha kabisa kulinda haki za wateja wao wala kutaka kujua taarifa za mteja zinaombwa kutokana na kosa gani. Kwao Polisi ndiyo kila kitu, wateja ni takataka.

Kutokana na ukweli huu, wateja ni lazima tulipinge hili kwa vitendo. Tufanye yafuatayo,na mengine uatakayoonekana yanafaa:

1) Sisi wenye line za Airtel, kwa vile wengi tuna lines zaidi ya moja, tusitumie line ya Airtel angalao kwa mwezi mmoja. Kama unalazimika, basi tumia pale tu ambapo huna namna nyingine.

2) Kwa uhakika mitandao karibia yote ya simu, ukiondoa Halotel na Zantel (hakuna ushahidi), siyo salama. Itumie kwa tahadhari kubwa hata kama mawasiliano yako hayana uovu wowote. Hawa jamaa hutengeneza uovu kisha wanausukumiza kwako alimradi mazingira yaruhusu. Tumia sms na calls za kawaida kwa mambo ambayo ni ya kawaida sana na yaliyo wazi. Mambo ambayo unadhani ni serious au confidential tumia whatsap, viber au skype.

Mawasiliano hata huko kwenye nchi zilizoendelea, yanakuwa monitored kwa sababu za kiusalama, lakini kwetu yanakuwa monitored kwaajili ya kuwakomoa au kuwabambikia watu kesi.
Unataka kufanya mgomo wa kijinga huku ukishawishi wafuate ujinga huo. Hakuna taasisi yoyote iliyopewa leseni ya nchi husika kuendesha shughuli zake za kibiashara, huduma na wajibu ambayo ina watu wakafanya uharifu kama wenyewe kisha wakajificha kwenye kivuli cha kutetewa na sheria ya faragha vinginevyo nchi nyingi zinge kuwa zimeshapinduliwa kirahisi na kizembe sana.

Hao uliowataja Halotel na Zantel unafahamu wamiliki wake ni akina nani?

Kwa ushauri tu jisomee hapa: https://journals.sas.ac.uk/deeslr/article/download/2302/2255/
 

Attachments

  • THE ACCESS TO INFORMATION ACT.pdf
    2.6 MB · Views: 6
  • THE CYBERCRIMES ACT, NO.14-2015.pdf
    7.5 MB · Views: 4
Hapo kwenye kukomoa hujaeleweka!

Fafanua vizuri.

Polisi walitaka kupewa taarifa ya miamala ya mteja husika, polisi walitaka pia kujiridhisha na mtiririko wa mawasiliano kati ya watuhumiwa, ambao pia ni wateja wa Airtel.

Huu ni utaratibu wa kawaida katika nyanja ya upelelezi wa makosa ya jinai Duniani kote.

Nini kosa la Airtel hapo?

Kumbuka kwamba kwao Airtel, wateja wote ni fair treated, hakuna mwenyekiti au katibu. Kwao wanafuata vigezo na masharti yaliyoko kwenye mikataba na leseni zao.

Mleta mada nakuomba utafute Documentary za "Discover ID's" zinapatikana kwenye king'amuzi cha Azam bundle la 35,000/=.

Huko utajifunza mengi kuhusu namna wenzetu hao tunaowaiga wanavyoshirikiana na makampuni ya mawasiliano kuwa trace watuhumiwa kwa kutumia mitandao ya simu na minara ya mawasiliano.

Tena wao wanakwenda mbali zaidi,saa ingine wanarekodi mawasiliano yoote ya mfuatiliwaji na kwa muda mrefu, mpaka wanapojiridhisha.

Chadema mnataka kila kila kitu muwe wajuaji.sheria nyinyi,siasa nyinyi,akifariki mwandishi habari Polisi,tayari mmerukia.

Yaani hamna agenda rasmi ambayo mnaitumia kama dira. Bali mnabaki kudandia matukio na kuongoza kamati za fitna na visasi.
Yaani team ^roho mbaya "

Mmeweka wanasheria nguli kwenye hiyo kesi ya Mwenyekiti Mbowe.
Vema muwaache wafanye kazi yao kwa uhuru mpaka mwisho wa kesi.

Hizi harakati zenu za kujifanya kupambana na huduma za kijamii huwa mnafeli kila wakati, ila sababu hamtunzi kumbukumbu ndio maana mnarudia mihemko yenu kila mara.

Nchi inao wananchi milioni sitini, chadema mnao wanachama wangapi nchi nzima ambao wako radhi kuitikia wito huu wa kijinga?

Hata kama wakiitikia kwa 15% au 100%,still haitaweza kubadili mwenendo wa kesi iliyoko mahakamani.

Lakini pia haitawadhuru Airtel kwa lolote.hii kampuni ina operate almost Afrika kote.na mmoja wa wana hisa wake ndie huwa anatoa tuzo ya mwanasiasa bora Afrika kila baada ya kipindi fulani.
Huyo ni Mo Ibrahim.

Watu mnaweza kuwa na imani ya itikadi moja ya kisiasa ndio.
Lakini hamuwezi kulingana linapokuja suala la mahitaji binafsi.

Kila mmoja anazo mbinu na shughuli zake mahsusi za kujitafutia kipato kwa kuendesha familia yake.
Hata Mbowe ni mwanasisa lakini pia ni mfanyabiashara.na kuna namna amekuwa mnufaika wa huduma za Airtel kwa kipindi kirefu.
Ndio maana alikuwa mteja wao.

Wengine mawasiliano ndio kila kitu, ukizingatia maendeleo ya teknolojia ya sasa.
Ikiwemo suala la miamala ya simu pia.

Halafu wewe mkereketwa wa siasa umwambie afunge ujasiliamali wake .
Kisa mawasiliano ya mwenyekiti yametolewa na kampuni kwa serkali kama sehemu ya kielelezo cha ushahidi?

Je baadae chadema itamsaidiaje huyu mnayemshauri kususia huduma kwa maslahi ya chama chenu,kwa maslahi ya mwenyekiti Mbowe?

Mtamsaidia kujikimu kimaisha wakati akiwa ameitikia wito wenu na amesitisha uwakala wa miamala ya Airtel?

Mlifeli huko nyuma, kampeni kama hii kwa Vodacom.

Pia mkafeli kwa kampeni kama hii kwa kampuni ya kuzalisha maji ya kunywa, mkiihusisha na mheshimiwa Aeshi,kama sikosei.

Hamjifunzi kuanzia hapo?

Acheni kamati za Roho Mbaya!

#Hatutakiwahuni
 
Tangu kesi dhidi ya Mbowe, inayojulikana kama kesi ya mchongo au kesi kubambikia ianze, imedhihirika wazi pasipo shaka namna baadhi ya makampuni ya simu za mkononi yanavyoshirikiana na Polisi waovu dhidi ya wateja.

Mwanasheria wa kampuni ya Tigo na Airtel, wote kwa nyakati tofauti walieleza jinsi wanavyotoa taarifa za wateja hovyo, alimradi tu wameona barua yenye nembo ya jeshi la Polisi huku wakiacha kujishughulisha kabisa kulinda haki za wateja wao wala kutaka kujua taarifa za mteja zinaombwa kutokana na kosa gani. Kwao Polisi ndiyo kila kitu, wateja ni takataka.

Kutokana na ukweli huu, wateja ni lazima tulipinge hili kwa vitendo. Tufanye yafuatayo,na mengine uatakayoonekana yanafaa:

1) Sisi wenye line za Airtel, kwa vile wengi tuna lines zaidi ya moja, tusitumie line ya Airtel angalao kwa mwezi mmoja. Kama unalazimika, basi tumia pale tu ambapo huna namna nyingine.

2) Kwa uhakika mitandao karibia yote ya simu, ukiondoa Halotel na Zantel (hakuna ushahidi), siyo salama. Itumie kwa tahadhari kubwa hata kama mawasiliano yako hayana uovu wowote. Hawa jamaa hutengeneza uovu kisha wanausukumiza kwako alimradi mazingira yaruhusu. Tumia sms na calls za kawaida kwa mambo ambayo ni ya kawaida sana na yaliyo wazi. Mambo ambayo unadhani ni serious au confidential tumia whatsap, viber au skype.

Mawasiliano hata huko kwenye nchi zilizoendelea, yanakuwa monitored kwa sababu za kiusalama, lakini kwetu yanakuwa monitored kwaajili ya kuwakomoa au kuwabambikia watu kesi.
Hakuna lisilo na mwisho. Haya hao makampuni hawana raha na kesi za kubambikiza.
 
Hakuna anayekataa taarifa za wahalifu kutolewa kwa mamlaka husika, ila sio kwa lengo la kumkomoa mteja. Kinachoendelea kwenye hiyo kesi ya Mbowe, makampuni yote yaliyopeleka ushahidi hadi sasa yanaonyesha yanatoa taarifa kwa shinikizo la kukomoana, na hayo makampuni yote yanajua fika yanatumika kutengeneza ushahidi wa kukomoana kisiasa. Mashahidi wote wawili wanatoa ushahidi wa wazi wa kutengeneza.
Na kwa nn ktk statement yao ya miamala walijaribu kuficha jina la mzanzibar yule
 
Hakuna utawala wa sheria nchini hivyo wawekezaji wamekuwa waoga kwa serikali otherwise wangelinda faragha ya mteja mpaka polisi waje na order ya mahakama kama sheria inavyotaka. Unaletewa barua leo ya kuomba taarifa ya mteja wako, siku hiyohiyo unatoa taarifa za mteja pasipo kichunguza uhalali wa barua mradi tu ina nembo ya jeshi la polisi na muhuri. What if ikiwa barua ni ya kufoji?

Watuhumiwa wameshitakiwa kwa kosa la ugaidi lakini taarifa za mtuhumiwa zinaombwa kwa vifungu vya sheria ya mtandao, mwanasheria mzima unatoa taarifa haraka kwa uoga ama kuwepo sehemu ya michongo.
 
Hao mashahidi wote ni maafisa vipenyo waliomwagwa kila eneo enzi za mwendazake kwa ajenda maalum ya kuua upinzani,ni Sawa na wale waliofyatuliwa risasi na Mfanyabiashara wa Mabasi ya Zakaria yule jamaa angekua Hana Silaha wangeshamuua,hao dawa yao wakiingia ndani ya 18 zako nikuwafyeka tu,awamu hii Kama unauwezo wa kumiliki Liberty revolver,Taurus G2C au Glock G19 hakikisha unamiliki ka kwako Mambo yamechange now tunaishi Kama Nguruwe ndani ya shamba la mahindi.
 
Tangu kesi dhidi ya Mbowe, inayojulikana kama kesi ya mchongo au kesi kubambikia ianze, imedhihirika wazi pasipo shaka namna baadhi ya makampuni ya simu za mkononi yanavyoshirikiana na Polisi waovu dhidi ya wateja.

Mwanasheria wa kampuni ya Tigo na Airtel, wote kwa nyakati tofauti walieleza jinsi wanavyotoa taarifa za wateja hovyo, alimradi tu wameona barua yenye nembo ya jeshi la Polisi huku wakiacha kujishughulisha kabisa kulinda haki za wateja wao wala kutaka kujua taarifa za mteja zinaombwa kutokana na kosa gani. Kwao Polisi ndiyo kila kitu, wateja ni takataka.

Kutokana na ukweli huu, wateja ni lazima tulipinge hili kwa vitendo. Tufanye yafuatayo,na mengine uatakayoonekana yanafaa:

1) Sisi wenye line za Airtel, kwa vile wengi tuna lines zaidi ya moja, tusitumie line ya Airtel angalao kwa mwezi mmoja. Kama unalazimika, basi tumia pale tu ambapo huna namna nyingine.

2) Kwa uhakika mitandao karibia yote ya simu, ukiondoa Halotel na Zantel (hakuna ushahidi), siyo salama. Itumie kwa tahadhari kubwa hata kama mawasiliano yako hayana uovu wowote. Hawa jamaa hutengeneza uovu kisha wanausukumiza kwako alimradi mazingira yaruhusu. Tumia sms na calls za kawaida kwa mambo ambayo ni ya kawaida sana na yaliyo wazi. Mambo ambayo unadhani ni serious au confidential tumia whatsap, viber au skype.

Mawasiliano hata huko kwenye nchi zilizoendelea, yanakuwa monitored kwa sababu za kiusalama, lakini kwetu yanakuwa monitored kwaajili ya kuwakomoa au kuwabambikia watu kesi.
Tatizo watumiaji hatuna umoja wa namna hiyo
 
Back
Top Bottom