Watu wengi au watu bora

Watu wengi au watu bora

ShesRise_1

JF-Expert Member
Joined
Aug 21, 2025
Posts
16,776
Reaction score
39,743
Maana unaweza kusema, "Ninakubalika." Sawa, lakini unakubalika na akina nani?

Ni watu wa aina gani wanaokukubali?

Kwa sababu si kila anayekukubali anaelewa hata maana ya kukukubali.


Wengine wanakufuata kwa mazoea, wengine kwa mihemko, na wengine kwa sababu hawajui hata lipi ni sahihi na lipi si sahihi

Unaweza ukawa na kundi kubwa sana la watu, lakini likiwa halina uwezo wa kuhoji wala kuchambua, kweli huo ni mtaji au ni idadi tu?

Watu ambao kazi yao ni kusema, "Ndiyo mzee. (Pr J song ) Ukisema kushoto ni kulia, watasema ni kweli. Ukibadili kesho, nao watabadilika bila hata kukuuliza kwa nini

Binafsi, bora niwe na watu wachache wanaoweza kunichana makavu kuliko kuwa na maelfu wanaoniambia kila siku kuwa niko sahihi

Bora niwe na watu wanaoweza kunisifia hadharani lakini wakinikosoa hata kwa siri

Bora niwe na watu wasioniogope bali waniheshimu(tuheshimiane sio kuogopana)

Watu ambao wakiona nimepotoka, wana ujasiri wa kuniambia
Hapana, hapo umekosea

Kwa sababu watu wanaoshindwa kukukosoa si wote wanakupenda
wengine wanaogopa, wengine wananufaika na makosa yako, na wengine hawana hoja kabisa

Sasa jiulize, unataka watu wanaojenga fikra zako au wanaojenga ego yako?

Wewe mdau, unapendelea kuwa na kundi kubwa lisiloweza kukuchallenge, au watu wachache wenye akili wanaoweza kukubadilisha kwa hoja, kwa maneno na kwa vitendo?
 
Maana unaweza kusema, "Ninakubalika." Sawa, lakini unakubalika na akina nani?

Ni watu wa aina gani wanaokukubali?

Kwa sababu si kila anayekukubali anaelewa hata maana ya kukukubali.


Wengine wanakufuata kwa mazoea, wengine kwa mihemko, na wengine kwa sababu hawajui hata lipi ni sahihi na lipi si sahihi

Unaweza ukawa na kundi kubwa sana la watu, lakini likiwa halina uwezo wa kuhoji wala kuchambua, kweli huo ni mtaji au ni idadi tu?

Watu ambao kazi yao ni kusema, "Ndiyo mzee. (Pr J song ) Ukisema kushoto ni kulia, watasema ni kweli. Ukibadili kesho, nao watabadilika bila hata kukuuliza kwa nini

Binafsi, bora niwe na watu wachache wanaoweza kunichana makavu kuliko kuwa na maelfu wanaoniambia kila siku kuwa niko sahihi

Bora niwe na watu wanaoweza kunisifia hadharani lakini wakinikosoa hata kwa siri

Bora niwe na watu wasioniogope bali waniheshimu(tuheshimiane sio kuogopana)

Watu ambao wakiona nimepotoka, wana ujasiri wa kuniambia
Hapana, hapo umekosea

Kwa sababu watu wanaoshindwa kukukosoa si wote wanakupenda
wengine wanaogopa, wengine wananufaika na makosa yako, na wengine hawana hoja kabisa

Sasa jiulize, unataka watu wanaojenga fikra zako au wanaojenga ego yako?

Wewe mdau, unapendelea kuwa na kundi kubwa lisiloweza kukuchallenge, au watu wachache wenye akili wanaoweza kukubadilisha kwa hoja, kwa maneno na kwa vitendo?
Kwenye siasa, watu wengi tena wapiga kura ndio mtaji. Wawe vyovyote utakavyowaona wewe, ili mradi wanapiga kura na ni wengi, basi hao ni muhimi sana.

Kwenye academic arena, idadi ya watu sio hoja kabisa. Hata mkiwa wawili ili mradi mnaweza kujenga hoja pamoja mkaelewana, sawa kabisa. Karl Marx na rafiki yake Friedrick Angels walielewana sana hadi wakaandika kitabu chao cha "Das Kapital" ( The Capitalism). Tena inasemekana walikuwa wakikiandika baada ya kutoka Baa kupiga mvinyo pamoja! Ahahahahaha!!
 
Bora uwe na high self esteem.

Uwe na watu wengi ama uwe na watu bora, u wont care.

You will feel self sufficient regardless of whatever situation.
Upo sahihi kua na high self esteem
Na huu ni ndio msingi wa mtu mwenye maarifa

Lakini pia watu wanaweza kukubadili au mazingira yanayokuzunguka

Mi nadhani watu wako wa karibu wana mchango kwa kiasi fulani kwenye maisha yako matendo nk....
 
Upo sahihi kua na high self esteem
Na huu ni ndio msingi wa mtu mwenye maarifa

Lakini pia watu wanaweza kukubadili au mazingira yanayokuzunguka

Mi nadhani watu wako wa karibu wana mchango kwa kiasi fulani kwenye maisha yako matendo nk....
Ukishakuww na high self esteem plus uko positive, basi automatic una attract watu bora maishani mwako.
 
Back
Top Bottom