Kuna watu wawili ambao kesho wakienda kwenye TV au watoke na wasema maneno haya nchi hii tutakuwa na chaguzi huru na demokrasia. Watu hawa sio wanasiasa au wazee je wa hao ni nani na watasema nini
1. Mkuu wa majeshi atoke na aseme tena kwa upole sana. Aseme nchi yetu inapenda haki, nchi yetu na katiba yetu ni ya kidemokrasia jeshi la wananchi hakitakubaki chaguzi zisizo za huru na haki
2. Kadinali wa katoliki Protase Rugambwa. Huyu ni mkuu wa kanisa katoliki ambalo pamoja na waumini wengi ndilo kanisa lenye wekezaji mkubwa kuliko shirika lolote Tanzania la binafsi au la umma. Atoke aseme hivi
kanisa kitatoa tamko kwa wakatoliki wote na wapenda imani kwamba wasishiriki chaguzi zozote kabla ya sheria kurekebishwa na kanisa litasimamisha shughuli zote nchini ambazo ni pamoja na mashule, mojospitali na mambo yote ya kanisa mpaka pale chaguzi ziwe za huru na haki
Kati ya hawa wawili wakitoka na kusema hivyo kesho hii nchi itabadilika. Hivyo tushinikize hawa wawili kufanya hivyo kwa maslahi ya taifa kabla nchi hii haijawa ya familia tatu
Cardinal Protase Rugambwa sio mkuu wa kanisa hapa Tanzania, hana cheo Cha kiongozi kwenye kanisa la Tanzania kwenye level ya Kitaifa,zaidi ya kuwa Askofu Mkuu wa metropolitan ya Tabora na majimbo kadhaa yanayomzunguka ikiwemo jimbo la kigoma.
Askofu mwenye mamlaka na bossy wa kanisa Katoliki Tanzania,ni Rais wa Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania,kwa sasa ni ASKOFU WOLFGANG PISSA WA JIMBO LA LINDI, chini yake ni Askofu Eusebius Mzigirwa Makamu wa Rais.
Hao wawili ndiyo wakuu kwa sasa, ndio wasemaji kwa niaba ya Kanisa Katoliki Tanzania,wakitoa tamko kanisa Katoliki linafuata, Maaskofu wanafuata akiwemo Askofu Mkuu wa Tabora ambaye pia ni Cardinal.
Watu wengi wanachanganya wanadhani kardinali ni mkuu wa kanisa Katoliki,hata waandishi wengi hupenda kwenda kumuhoji kardinali panapokuwa na jambo kwa niaba ya Kanisa badala ya Rais wa Baraza la Maaskofu.
Kardinali ni cheo tu Cha kuwa mshauri wa Papa,na kazi nyingine ni kupiga kura wakati wa uchaguzi wa Papa,anapewa pia Parokia huko Vatican.
Kwa hapa Tanzania ni mjumbe tu kwenye Baraza la Maaskofu, ni Askofu tu kama maaskofu wengine.
Hilo tamko unalotamani atoe kardinali,hana uwezo wala mamlaka hayo ya kulitoa,mwenye uwezo na mamlaka hayo ni Rais wa Baraza la Maaskofu Tanzania, unless ikitokea kardinali Rugambwa amechaguliwa pia kuwa Rais wa Baraza la Maaskofu.
Wakati wa pengo waandishi wengi VILAZA walikuwa wanaenda kumuhoji pengo kuhusu Kanisa la Tanzania,mosi kwa kutokujua nani Mkubwa na msemaji kwa Kanisa la Tanzania.
Kwahiyo Hilo tamko unalotamani mwenye mamlaka ni Rais wa Baraza la Maaskofu TEC Askofu WOLFGANG PISSA.
Aksante sana 🙏🙏