Watu wasiojulikana waiba CCTV(camera) zilizokuwa zinazuia majangili Ruaha National Park

barafu

JF-Expert Member
Apr 28, 2013
6,726
32,818
Watu wasiojulikana wameiba na kutokomea na CCTV(camera) zilizowekwa kandokando ya mipaka ya vijiji na mbuga ya Hifadhi ya Ruaha(Ruaha National Park) katika Tarafa ya Pawaga na Idodi.

Kamera hizo ziliwekwa na mamlaka husika ili kuzuia vitendo vya ujangili vinavyofanywa na majangili wakubwa wanaofadhili wanakijiji wa vijiji vilivyochini ya MBOMIPA kuhujumu maliasili na wanyamapori katika hifadhi ya Ruaha.

Kuondolewa/kuibiwa kwa kamera hizi kunaongeza uwezekano wa kuendelea kwa ujangili na wizi wa mali katika mipaka na ndani ya mbuga ya Ruaha iliyoko kati ya mikoa ya Iringa na Mbeya.

Mamlaka husika zimeanza uchunguzi kubaini wote waliohusika na uwizi huo wa kamera maalumu za kufuatilia ujangili.

Siku kadhaa barafu wa JF nilileta uzi huu Mh. Kigwangalla, karibu Maliasili na Utalii. Anza na hawa majangili wa Ruaha National Park kumpa changamoto Waziri wa Maliasili Mh.Hamis Kigwangala kuanza na majangili wa Ruaha National Park,na siku kadhaa baadae,majangili hao wameshirikiana na wanakijiji wa vijiji vya MBOMIPA kwa kuwarubuni ili kuendeleza uwizi.

Hizi ni changamoto za sekta ya utalii na ujangili katika Wizara ya Mh.Kigwangala,tunamsihi tena na tena,hii ndio wizara ambayo wadau wana pesa kuliko waziri.Aingie kwa step...Kupotea kwa CCTV huko Ruaha National Park ni salamu kwa Mh.Kigwangala.
 
...
....dah sisalama kwa Tembo wetu

Mkuu Barafu nimepata taarifa Mtafiti wetu wa Tembo mashuhuri Tazania kafariki huko Arusha alifunga GPS tracking kwa Tembo huko Ruaha
 
...
....dah sisalama kwa Tembo wetu

Mkuu Barafu nimepata taarifa Mtafiti wetu wa Tembo mashuhuri Tazania kafariki huko Arusha alifunga GPS tracking kwa Tembo huko Ruaha
Ndio unanipa habari,sikuwa mtandaoni kwa muda kidogo!!Habari mbaya hii
 
kama inaumuhimu mkubwa recordings zake zingekaa hata wizarani.
na kuwe na task force mtu akitemper na hizo camera tu hata kwa kuiziba wanafika haraka kupatrol kuona kwa nini na ninani kama hakuonekana kwenye footage au kama alificha sura.

maoni tu japo hatujui mazingira na jiographia iKOJE HUKO.
au zinawekwa za siri bila hata wahusika kujua kama sheria inaruhusu hizo zinazoibika zinabaki kuwapoteza maboya.
hongera mkuu kwa taarifa.
 
Ndio unanipa habari,sikuwa mtandaoni kwa muda kidogo!!Habari mbaya hii
.....
.....sana Mkuu TUMEPOTEZA
Aliweza kufunga GPS kwa Tembo kujuwa movements zao huko Saadan West Kilimanjaro Ruaha etc na ni Mtanzania very Kujituma kwa kazi yake....
 
kama inaumuhimu mkubwa recordings zake zingekaa hata wizarani.
na kuwe na task force mtu akitemper na hizo camera tu hata kwa kuiziba wanafika haraka kupatrol kuona kwa nini na ninani kama hakuonekana kwenye footage au kama alificha sura.

maoni tu japo hatujui mazingira na jiographia iKOJE HUKO.
au zinawekwa za siri bila hata wahusika kujua kama sheria inaruhusu hizo zinazoibika zinabaki kuwapoteza maboya.
hongera mkuu kwa taarifa.
.....
...wakipekuwa vizuri kwenye vijiji watapata information. ..
 
Back
Top Bottom