Watu wa Dar mnazidi kutuangusha upinzani, sijategemea

Watu wa Dar mnazidi kutuangusha upinzani, sijategemea

Countrywide

JF-Expert Member
Joined
Mar 2, 2015
Posts
21,484
Reaction score
34,223
Habari wana JF,

Kama ilivyo kawaida yangu kuwaletea kila kinachojiri kuhusu chama chetu na upinzani kwa ujumla wake. Leo kulikuwa na tukio pale Kiluvya, ambapo mgombea wetu alizuiliwa. Yote kwa yote siungi mkono polisi kumzuia ila niseme tu watu wa Dar ilipaswa kuonyesha mshikamano kwa kuwa tunaamini nguvu ya umma haijawahi kushindwa.

Cha kushangaza kabisa, pamoja na taarifa kutolewa kila wakati juu ya kuzuiwa kwa mgombea wetu ila watu wa Dar ni kama waliweka pamba masikioni na kutoonekana kwa wingi kabisa kuwa pamoja na mgombea wetu.

Mimi nilikuwepo eneo la tukio na imeniwia vigumu sana kuamini kama kweli watu wa Dar wapo hivi.
Ni kwamba mpo busy sana? Au basi tu mmeamua kupuuzia? Ili iweje?

Pia niseme tu mgombea wetu anapaswa kupata washauri kwa kuwa anaonekana pia kutoa msimamo kwenye jambo ambalo haliwezekani.

Chini nimeweka picha za mchana na video ya usiku huu kabla ya kuamua kuondoka hapo.
IMG_20201006_195035.jpg
IMG_20201006_201151.jpg

 
We si ulikuwepo?? Mbona hujafanya kitu???.. watu wa Dar wamewadharau.
 
Wewe ulikuwepo eneo la tukio, vipi ulifanya nini mkuu? Au si miongoni mwa watu wa dar?


Let's meet at the top, cheers 🍻
 
Roho wa Mungu akuhurumie
Yaan huwa najiuliza hawa mashabiki wa CCM kwa nini wanajifanya vipofu na viziwi.

Huwa nakereka na ninaumia sana kila ninavyona comments za wafuasi wa Magufuli kwenye nyuzi humu.
 
Sisi watu wa Dar huwaga tunakula vichwa kimya kimya.

simba mwenda pole ndiye mla nyama.

2015 ilikuwa hivi hivi.... kushitukia kiutaniutani 70% ya majimbo ya ubunge yakaishia mikononi mwa UKAWA na pia wakaikamata halmashauri ya Jiji.

watu wa Dar usituchukulie poa hata kidogo ndugu!
 
So lengo la haya yote ni kujaza watu Kiluvya au?!
 
pamoja na kupongeza namna wenzetu wa sehemu zingine za nchi wanavyofanya siasa za upinzani kwa hamasa kubwa, nikuambie tu mleta-mada, Dar is there and ready. tarehe 28 utashangaa.

Segerea ✌
Ukonga ✌
Kawe ✌
Ubungo✌
Kibamba ✌

subiri uone.
 
pamoja na kupongeza namna wenzetu wa sehemu zingine za nchi wanavyofanya siasa za upinzani kwa hamasa kubwa, nikuambie tu mleta-mada, Dar is there and ready. tarehe 28 utashangaa.

Segerea [emoji111]
Ukonga [emoji111]
Kawe [emoji111]
Ubungo[emoji111]
Kibamba [emoji111]

subiri uone.
Mkuu jimbo pekee mlilobaki nalo hapa dar ni kawe pekee nayo mjiandae kisaikolojia.

Kama hiyo ukonga ndio kabisa
 
Mapolisi wamelegea! wamekimbia kutoka eneo la tukio.

Chuma kimesema kinaendelea na mikutano Mlandizi usiku huu huu.

Tundu Lissu kawashika MATAGA kunako dadeki!!
 
Back
Top Bottom