Watu gani watatu mashuhuri unaweza ukatundika picha zao ukutani kwako?

ESCORT 1

JF-Expert Member
Dec 7, 2015
1,267
2,519
Kutokana na nafasi zao na michango yao katika jamii, mimi bila kupoteza muda picha za Bob Marley, Patrice Lumumba na Nelson Mandela zipo ukutani nyumbani kwangu. Hao watu ni vielelezo vya wanaharakati waliojitoa kwa ajili ya kupambania haki za wengine hasa mtu mweusi.

Je, kwa upande wako ni watu gani watatu mashuhuri unaweza ukabandika picha zao nyumbani kwako?

F482CFC7-20F4-47AE-A400-E989C67B8B20.jpeg
 
1. Mwalimu Julius Kambarage Nyerere.

2. Nelson Mandela.

3. Barack Obama.

Inspiration ya hao watu inazidi utamu wa 'Pira Biriani'.
Obama...???
Seriously.. after what happened to Libya still you got the gut to take the man as inspiration to you. Yemen, Iraq, Palestine na nchi nyingine nyingi zilifanywa vibaya na uongozi wa huyu bwana. Muamar Gaddafi the Icon of Africa aliondolewa na huyu bwana mwenye ngozi nyeusi lakini mweupe ndani. Hafai hata kutajwa na sisi wa Africa. Usiangalie tu rangi ya ngozi yake na ukubwa wa nafasi aliyowahi kuishika.
Hata tu hapa kwetu kuna mwanamke wa pekee kushika wadhifa wa juu lakini ona anachotufanya.
 
Kutokana na nafasi zao na michango yao katika jamii, mimi bila kupoteza muda picha za Bob Marley, Patrice Lumumba na Nelson Mandela zipo ukutani nyumbani kwangu. Hao watu ni vielelezo vya wanaharakati waliojitoa kwa ajili ya kupambania haki za wengine hasa mtu mweusi.

Je, kwa upande wako ni watu gani watatu mashuhuri unaweza ukabandika picha zao nyumbani kwako?

View attachment 2221681
2 pac , Pablo Escobar na Osama bin laden
 
Nyerere, Benjamin William Mkapa, Jaji Sinde Warioba ex PM!
Muda wowote nikipewa nafasi nitagonga nao cheers!

Nje ya nchi Put-in, Bob Marley, Fidel Castro, mbali na mabeberu

Katika mabeberu Margaret Thatcher, Angela Merkel, na Benjamin Netanyahu!

Netanyahu alikuwa akili kubwa. Kuwatawala sijui kuwaongoza wale waisrael wakaksi, kupangua shutuma na kesi zake yaani huwa namuona genius! Huku kukiwa na Hamas na PLO, Kwa vipindi tofauti, huwa namu admire! Ujasiri na uthubutu! Sifagilii uuaji wa wapalestina!
Mpalestina anatumia manati muisrael anatumia bunduki! World is not fair!

Ila kuna kwamba Silvio Berlusconi, kuna issue aliambiwa hii kesi huchomoi labda uwe prime minister, jamaa akasema ndoho taabu. Akawa prime minister! Haa haa!
 
Back
Top Bottom