Watu 5 mbaroni wakihusishwa na kifo cha muuguzi wa KCMC

Nyendo

JF-Expert Member
Jun 4, 2017
1,194
4,115
Jeshi la Polisi mkoa wa Kilimanjaro linawashikilia watu watano kwa tuhuma za mauaji ya Khudheifa Changa, ambaye alikuwa ni Muuguzi wa Hospitali ya KCMC Moshi mkoani humo.

Inadaiwa Khudheifa Changa aliuawa usiku wa kuamkia Julai 2, mwaka huu wakati akipita katika uchochoro wa Mtaa wa Marindi mjini Moshi, katika purukushani alijeruhiwa kwa kuchomwa na kitu chenye ncha kali kwenye mbavu ya kushoto usawa wa moyo.

Kamanda wa Polisi mkoa wa Kilimanjaro ACP Simon Maigwa, amesema kuwa watuhumiwa hao ambao watatu ni wanaume na wanawake wawili walikuwa na nia ya kumpora mali alizonazo, na kwamba watafikishwa mahakamani upelelezi utakapokamilika.

Pia soma: Muuguzi KCMC auawa kwa kuchomwa na kitu chenye ncha kali uchochoroni
 
Source EATV.
Jeshi la Polisi mkoa wa Kilimanjaro linawashikilia watu watano kwa tuhuma za mauaji ya Khudheifa Changa, ambaye alikuwa ni Muuguzi wa Hospitali ya KCMC Moshi mkoani humo.

Inadaiwa Khudheifa Changa aliuawa usiku wa kuamkia Julai 2, mwaka huu wakati akipita katika uchochoro wa Mtaa wa Malindi mjini Moshi, katika purukushani alijeruhiwa kwa kuchomwa na kitu chenye ncha kali kwenye mbavu ya kushoto usawa wa moyo.

Kamanda wa Polisi mkoa wa Kilimanjaro ACP Simon Maigwa, amesema kuwa watuhumiwa hao ambao watatu ni wanaume na wanawake wawili walikuwa na nia ya kumpora mali alizonazo, na kwamba watafikishwa mahakamani upelelezi utakapokamilika.
20230705_184610.jpg



My take..
Kwahiyo vibaka Hapo Maeneo ya Malindi mpaka redstone, hugoz wameshindwa kuthibithiwa?
Mwaka Jana nilikua nahama kiwanja natoka Hapo hugoz naenda redstone ni mwendo wa sekunde chache then unavuka road. Pikipiki ilipita mbele yangu imebeba watu wanne wakashuka na mapanga na sime isingekua mbinu zangu za Usain bolt zisingefanya kazi sasahivi ningekua Marehemu, nilitoka nduki vibaya mno hao vibaka wanakaona Vumbi tu.


Hapo vichochoroni Malindi kama unaenda maktaba Kuna mateja (sio Malaya) ni mateja kabisa hata Ukiwa na buku unawainamisha Hapo Lakini ukitoka salama basi wewe unae Mungu maana wanakupiga search huku vibaka wakiwa wamejificha nyuma ya uzio wa maktaba ya mkoa pale.

Basi inaonekana ndugu yetu alikua anapita kufanya doria tu hao vibaka wakaunga nae pole yake sana.

Ukiwa mgeni Moshi saa mbili au tatu usitembee kwa mguu Maeneo hayo vibaka wa pikipiki ni wengi mno.
 
Back
Top Bottom