Watu 20 wafa ajalini Busega

Watu 20 wafa ajalini Busega

Nipo ktk eneo la tukio, kiukweli hali ni mbaya sana watu waliofariki mpk sasa ni zaidi ya 40. Kuna maiti imeng'ang'ania chini ya tairi hata break down wilaya nzima hakuna! JAMANI AJALI NI MBAYA SANA KULIKO TUNAVYOFIKIRIA.
 
Kamanda Mpinga apeleke tochi wiki hii hii. Lakini wakati mwingine wananchi hao wanakuwa sehemu ya matatizo. Ukithubutu kumkemea dereva kwa mwendo kasi usiofaa, abiria watakugeuka na kukushurutisha ushuke katika basi. Matokeo yake basi likishapinduka na kuua, ndipo utasikia, ooh dereva alikuwa akiendesha kasi! Tanzanians, wake up!! Poleni sana ndugu zetu mliofikwa na dhahama hii.

Eti zile speed governor vipi? Miradi hii jamani, tunazidi kuteketea!!
 
Watu wapatao 20 wamefariki dunia na wengine kujeruhiwa vibaya sana baada ya basi la Nyehunge (au Luhuye) kutoka Musoma kwenda mwanza kuacha njia na kugonga nyumba kisha kupinduka katika kijiji cha itimila/Itumila A wilayani Busega mkoani simiyu

Chanzo: ITV breaking news

Ni katika kijiji cha Yitwimila "A" , Kata ya Kiloleli, Wilaya ya Busega. Basi hilo limepeasuka tyre kisha likaacha njia na kugonga nyuma ya Marehemu Mwalimu Mbofu (aliyekuwa mwenyekiti wa CWT Wilaya ya Magu) na kupinduka. Ni ajali mbaya sana.
 
Nipo ktk eneo la tukio, kiukweli hali ni mbaya sana watu waliofariki mpk sasa ni zaidi ya 40. Kuna maiti imeng'ang'ania chini ya tairi hata break down wilaya nzima hakuna! JAMANI AJALI NI MBAYA SANA KULIKO TUNAVYOFIKIRIA.

Jamani jamani jamani.... Mungu awarehemu!!
 
Barabara yote kuanzia sirari hadi mwanza hakuna tochi ya polisi. Magari, hasa mabasi yanaendeshwa kwa fujo sana. Kamanda mpinga aweke tochi pengine madereva wataogopa.

tochi siyo soln, maana madereva wengi wakijua point ya tochi tu wanapunguza mwendo na wakishapita wanalianzisha.Pita highway yote ya Mwanza-Dar point zote za tochi zinafahamika na madereva ni mchezo huohuo. Dawa kubwa ni kuwafungia madereva wazembe na wauaji kazi za kuendesha hata kama ni mkokoteni maisha yao yote. Kuna madereva wao ni kuua na kubadili mabasi na matajiri kama nguo.
 
Hiyo mizimu ya ccm haijashiba damu?? Yote hayo ni ili katiba ipitishwe tu wazidi kukaa madarakani mwanzo mwisho. Loh! Tambiko hizi zitawamaliza watz. Huko madreva hawana leseni mpya?? Ukiwa nayo tu hakuna ajali

Story ya Speed governor vipi? nipeni tender niwaletee original ajali zitakuwa historia!! Serikali sikivu ..........!!
 
Leseni mpya ilikua dili kwa maveiko.
Make sijaona ufanisi wowote.
 
Poleni wafiwa pia tunawaombea majeruhi wapone haraka, rai yangu kwa serikali hili suala la ajali si la kulizoea! Hatua stahiki zichukuliwe ili kuondosha majanga haya yanayogharimu maisha ya wananchi wasio na hatia! Ushauri madereva na kampuni znazosabisha ajali za mara kwa mara zifunguwe kutoa huduma! Pia rekebusheni hyo barabara ya mwanza musoma, imechoka njia nzima viraka!
 
dume kubwa,uti bila wa sheria bila shurti inatakiwa kwa watu wote
matokeo yake ndio hayo,huyu mwenzetu anasababisha vilema vya watu
 
Story ya Speed governor vipi? nipeni tender niwaletee original ajali zitakuwa historia!! Serikali sikivu ..........!!

dume kubwaaa;

Hilo dili limekaa poa saana hilo. Mwambie Wassira tu, akimwambia Lukuvi, tayari itaingia bungeni kesho kutwa kwani bunge la bajeti linaanza haraka kupisha muendelezo wa bunge la katiba. Lakini uwe tayari kwa 10%. Au vipi banaa. Kipindi hiki hao jamaa wameshiiba kweli kweli. Mwaka ulikuwa wa neema huu, mabunge mawili, vikao kibao na semina elekezi kedekede. Mlala hoi atazidi kuamkia hoi.
Mtanzania na vitendo tu Mtanganyika na usingizi tu
 
Nipo ktk eneo la tukio, kiukweli hali ni mbaya sana watu waliofariki mpk sasa ni zaidi ya 40. Kuna maiti imeng'ang'ania chini ya tairi hata break down wilaya nzima hakuna! JAMANI AJALI NI MBAYA SANA KULIKO TUNAVYOFIKIRIA.
...verybad news, but poleni sana aisee
 
Back
Top Bottom