Watu 20 wafa ajalini Busega

Watu 20 wafa ajalini Busega

Barabara hii ina viraka juu ya viraka. Halafu mabasi full kujiachia speed.
 
Dah Habari mbaya hii kusikia kwa siku hii ya ufufuko wa Masiah..Ila hilo basi mwendo wake unajulikana na kuna siku muungwana mmoja alisema hili basi likipiga mzinga utakuwa ni balaa. Dereva wake wananyosha sana goti na kuinunia lami.
Zipumzike mahala pema roho za marehemu wasionahatia.
 
Kamanda Mpinga apeleke tochi wiki hii hii. Lakini wakati mwingine wananchi hao wanakuwa sehemu ya matatizo. Ukithubutu kumkemea dereva kwa mwendo kasi usiofaa, abiria watakugeuka na kukushurutisha ushuke katika basi. Matokeo yake basi likishapinduka na kuua, ndipo utasikia, ooh dereva alikuwa akiendesha kasi! Tanzanians, wake up!! Poleni sana ndugu zetu mliofikwa na dhahama hii.
 
Habari tulizopata ni kwamba kuna ajali ya basi la Luhuye liendalo Sirari na Mwanza limepata ajali leo. Taktiban watu ishirini wamefariki papo hapo. Ajali hiyo imetokea maeneo ya Mwamanyiri. Taarifa zaidi Na picha zitawajia nitalapofika eneo la tukio.

Maafa makubwa ya ajali za barabarani Tanzania hayataisha mpaka pale tutakapoacha kuziona kuwa ni 'AJALI TU'. Serikali wanatakiwa kuchunguza kisayansi kila ajali ili kujua kwa nini zilitokea na ni nani awajibishwe.

Kwenda kuwapa pole wafiwa/walioumia peke yake sio kazi ya serikali, bali kuchunguza kwa kina vhanzo vha ajali inatakiwa iwe ndio jukumu lake kubwa. Mola awafariji wote walioguswa na ajali hii.
 
pole sana wahanga wa tukio, na marehemu wapumzike kwa amani
 
Poleni sasa jamani wafiwa wote na waliojeruhiwa wote ajali hizi zimezidi.
 
So sad! RIP. Kuna jamaa yangu hapa anadai eti Gamboshi iko Busega!?
 
Hiyo mizimu ya ccm haijashiba damu?? Yote hayo ni ili katiba ipitishwe tu wazidi kukaa madarakani mwanzo mwisho. Loh! Tambiko hizi zitawamaliza watz. Huko madreva hawana leseni mpya?? Ukiwa nayo tu hakuna ajali
 
kuna mabasi ya ZAKARIA huku mwanza sirari huo mwendo wake ni zaidi ya hatari na matrafiki wapo tu barabarani wanacheka nao
 
Barabara yote kuanzia sirari hadi mwanza hakuna tochi ya polisi. Magari, hasa mabasi yanaendeshwa kwa fujo sana. Kamanda mpinga aweke tochi pengine madereva wataogopa.

Tochi ipo Magu na Nyashimo. Lakini kuna hofu ya ushirikina baada ya askari mmoja aliyekuwa na tochi kufariki ghafla akiwa kazini huko Busega.
 
Mkuu Wilayani Busega Mkoani Simiyu na si Mwanza maeneo ya Magu... Usichanganye tafadhali
simiyu ilimega baadhi ya sehemu za magu ndo maana wengine bado wanayaita maeneo hayo kuwa ni ya magu.mazoea tu.
 
Back
Top Bottom