ngoshwe
JF-Expert Member
- Mar 31, 2009
- 4,131
- 931
Pengine watanzania tulio wengi huwa hatupo makini sana na mambo ambayo yanaweza kutujenga au kutuathiri sana maishani.
Kwa sasa imekuwa ni desturi kama si kawaida kwa wengi wetu kuwatumia watumishi wa ndani (House Girls, au House Boy) kutusaidia majukumu yetu. Hata hivyo, japo kuwa watumishi hawa huwa tunawaajiri ili waishi majumbani mwetu kama sehemu ya familia yetu na ndio ambapo kwa familia nyingi sana tunawapa majukumu makubwa sana ya kuzilea familia zetu (watoto), lakini cha kusikitisha pengine tunawaajiri pasipo hata kujua asili zao au walikotokea na matatizo ambayo pengine yanawahusu, (backgrounds) wala hatutaki kuajiri ambao angalau wana elimu ili tuweze kuwa minya mishahara nk.
Zipo familia ambazo muda wote baba na mama wapo "busy" kila kitu anafanya house girl hata kujua kama mtoto anaumwa au hajaenda shule ni jukumu la "dada".
Kuna familia ambazo "u-buzy" wa staili hii umezigharimu maishani,
Jirani yangu ananieleza binti yake wa miaka minne na kidogo amezoea kuwa muda wote na "dada", binti anakuja kuwaeleza baba na ***** haya:
"Eti da Gire tulivyoenda dukani kwa Mangi siku ile,....yule kaka pale akaja akakuwa ana mshika tu da Gire tumboni na nyonyo zae , eti...yee Da Gire eti amekaa tu wala amgombelezi wala nini...!!"
Ni mangapi mtoto ameweza kujifuza kwa "dada" akiwa muda wote na "dada".
Vipo familia ambazo "House Boy", Bw. Ng'ombe/shamba au dereva wa nyumbani anatumika kufanya kila kitu cha familia. Baada ya muda anakuja kuwa kuwadi kwa watoto wa tajiri kama si mwenyewe kuhusika moja kwa moja kuwavuruga mabinti wa tajiri..wengine ndio wanaotoa michoro kwa wakora ili waweze kuingia nyimbani...
Tuwe makini tunapoajiri hawa watu majumbani mwetu.
Kwa sasa imekuwa ni desturi kama si kawaida kwa wengi wetu kuwatumia watumishi wa ndani (House Girls, au House Boy) kutusaidia majukumu yetu. Hata hivyo, japo kuwa watumishi hawa huwa tunawaajiri ili waishi majumbani mwetu kama sehemu ya familia yetu na ndio ambapo kwa familia nyingi sana tunawapa majukumu makubwa sana ya kuzilea familia zetu (watoto), lakini cha kusikitisha pengine tunawaajiri pasipo hata kujua asili zao au walikotokea na matatizo ambayo pengine yanawahusu, (backgrounds) wala hatutaki kuajiri ambao angalau wana elimu ili tuweze kuwa minya mishahara nk.
Zipo familia ambazo muda wote baba na mama wapo "busy" kila kitu anafanya house girl hata kujua kama mtoto anaumwa au hajaenda shule ni jukumu la "dada".
Kuna familia ambazo "u-buzy" wa staili hii umezigharimu maishani,
Jirani yangu ananieleza binti yake wa miaka minne na kidogo amezoea kuwa muda wote na "dada", binti anakuja kuwaeleza baba na ***** haya:
"Eti da Gire tulivyoenda dukani kwa Mangi siku ile,....yule kaka pale akaja akakuwa ana mshika tu da Gire tumboni na nyonyo zae , eti...yee Da Gire eti amekaa tu wala amgombelezi wala nini...!!"
Ni mangapi mtoto ameweza kujifuza kwa "dada" akiwa muda wote na "dada".
Vipo familia ambazo "House Boy", Bw. Ng'ombe/shamba au dereva wa nyumbani anatumika kufanya kila kitu cha familia. Baada ya muda anakuja kuwa kuwadi kwa watoto wa tajiri kama si mwenyewe kuhusika moja kwa moja kuwavuruga mabinti wa tajiri..wengine ndio wanaotoa michoro kwa wakora ili waweze kuingia nyimbani...
Tuwe makini tunapoajiri hawa watu majumbani mwetu.