Watoto wa vigogo waiteka UVCCM!

Watoto wa vigogo waiteka UVCCM!

nadhani hawana shughul nyingine za kufanya so wanaandaliwa kuridhi biashara za wazee wao,nimeamin kwenye miti hakuna wajenzi kuna vijana wako bright na creative ila wanakosa support na nyenzo za kubun miradi itakayonufaisha vijana wengi lakin wenye support na mitaji wote wanakimbilia siasa.hv hawana fani zingine za kufanya zaidi ya siasa??
 
CHADEMA ndiyo mkombozi wa sie walala hoi..Chama Cha Mafisadi mwisho wao Umekaribia...
 
[h=5]Nzi na nyuki hufa kwa kulazimisha kupenya kwenye kioo , ndivyo watakavyoangamia wasomi, wafanyakazi na wakulima wanaolazimisha kutimiza ndoto zao kupitia CCM, sasa tuko kwenye kampeni maalum dhidi ya ccm 2015, waliingia kwa mbinu watatoka kwa mbinu watenda hutendwa, tuisaport CHADEMA, Tanzania bila ccm Inawezekana! Tuma ujumbe huu kwa waliochoshwa na ccm hasa wakulima, walimu, NMB,TRL, Wazee Wa EAC na Wanafunzi Vyuoni.MUNGU ibariki CHADEMA DAIMA_xx2[/h]
 
Lord Have Mercy! hivi hawa watu dhamira zao ina maana ZIMEKUFA KABISA??
 
CCM ikishinda mwaka 2015 itakuwa hivi! Kwanza wengine wata chakachua wapate ubunge kupitia viti maalumu.
Wengine watalamba ubunge wa kuteuliwa na Mkulu-sijui Lowassa wakati huo!

1. DICKSON MEMBE -Naibu Waziri wa Mambo ya Nchi za Nje
2. FREDY LOWASA -Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu-Tamisemi
3. RIDHIWANI KIKWETE - Naibu Waziri wa Sheria
4. ASHURA HUSSEIN MWINYI - Naibu wa Wizara ya Afya
5. BEN SAMWEL SITTA -Waziri wa Afrika Mashariki
6. DEBORA MWANDOSYA -Naibu Waziri wa Kilimo na Umwagiliaji
7. IRENE PINDA -Waziri Ofisi ya Raisi-Utawala Bora
8. FELISTER NDUGAI - Naibu Waziri wa Habari na longolongo
9. CHRISTOPHER NDEJEMBI -Balozi wa Kenya
10. SHARIFA BILAL -Naibu Waziri wa Fedha
11. HAWA KIGODA -Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara
12. JUDITH MUKAMA -Naibu Katibu Mkuu nyinyiem
13. JALOME MSEKWA -Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu-Bunge

Ikitokea hivi ni kuingia msituni tu! Wazazi wameua makumi, watoto wataua makumi elfu! Ufisadi utakaokuwepo utazidi ule wa Seseseko Zabanga.....!
 
hatari!

Angalia, watoto wa vigogo waliopita uvccm ngazi ya taifa.

1. Dickson membe
2. Fredy lowasa
3. Ridhiwani kikwete
4. Ashura hussein mwinyi
5. Ben samwel sitta
6. Debora mwandosya
7. Irene pinda
8. Felister ndugai
9. Christopher ndejembi
10. Sharifa bilal
11. Hawa kigoda
12. Judith mukama
13. Jalome msekwa
n.k

hao wote unaowataja wamegombea na kushinda, tuambiwe sasa kuwa lucy owenya ambaye ni mtoto wa ndesamburo aliigiwa kura na nani kupata ubunge viti maalumu??, grace kiwelu mkwe wa ndesamburo alipigiwa kura na nani?? Rahya ibrahimu alipigiwa kura na nani?? Christina lissu alipigiwa kura na nani?? Na wengine kibao wa viti maalumu nani aliwapigia kura?
?
 
Sasa unataka tukae kimya kwa kuogopa machafuko na kuwaacha wahujumu demokrasia hawa wakitufanya watz wajinga?Unaakili ya kitumwa sana wewe kama unaogopa kifo kaa kimya sisi hatuogopi kifo wala kuua maana tumeshazoea kuuawa na itafika zamu yao siku moja utashuhudia au kusimuliwa haki itakavyokuwa ikitendeka
Katika kutoa maoni, epuka jazba, uwe huru na ujifunze kukubali kusikia maoni hata yale yanayotofautiana na maoni yako. Kama mnadai kuchukua nchi kwa maneno makali namna hiyo, je! kweli mtaweza kuongoza???????? Mungu akuhurumie.
 
Moja ya dalili ya ulevi wa madaraka ndo hii kwamba watu wanadhani nchi ni ya kwao peke yao na wengine ni watumwa, na kwa sababu wazazi wana madaraka na pesa nani anawazuia? Lakini si wakati wote watafanikiwa kuna kizazi kitakataa mambo haya..nimesema.
 
Sioni tabu ya hawa watoto kugombea nafasi yeyote ndani na nje ya vyama vyao nao ni watanzania wenye haki sawa na mtanzania mwingine tusiwanyanyapae kwa sababu tu baba zao ni vigogo au mashuhuri au wanasiasa. Tuangalie je uchaguzi ulikuwa huru na haki. Je wazazi wao walilazimisha wao kushinda au walishinda kwenye mfumo huru??

Na sisi watoto wa akina pangu pakavu tusibweteke na kujiona wanyonge kwa kila kitu, jazeni form kwenye mifumo hii ya kisiasa serikali taasisi mbali mbali mshiriki badala ya kukaa pembeni na kupiga mayowe. Ninaushahidi wa kutosha kwamba watanzania wengi wanapenda kulalamika sana bila kushiriki. Sasa kama ninyi hamtaki kushiriki kwenye hizo chaguzi mnategemea nini?? Vigogo wanajitengenza na kazi ni kugombea tu. Ni vyema tukapigia kelele rushwa na kupendelea kuliko kuwawanyapapa hawa wototo kwa sababu tu baba zao wanamajina, wengine masikini zaidi ya majina ya baba zao choka mbaya.

Tushiriki kwenye mfumo wetu ili tuwe na kesi
Chief Mkwawa wa Karenga
No spinning
Chukua hatua madhubuti, tetea haki, wajibika, shiriki, kulalamika hakubadilishi nchi.

Ningependa nikujibu kama ifuatavyo mkuu; CCM ni chama kilichojitengenezea kamfua ka rushwa kutawala kipindi cha chaguzi zote kuanzia za chama hadi za jumuiya zao. Na viongozi wengi hapo ni wale ambao wamejirimbikizia mali kupitiliza, je mi mtoto wa kapuku nitaweza kushindana nao kwa dhana ya rushwa kutawala chaguzi zao? Kwanini wasijae wao walio na fedha za kuhonga?
 
Kuna tetesi kuwa majina mengi ya wajumbe wa UVCCM ni watoto wa vigogo! Kama habari yenyewe ni kweli basi tunakokwenda siko
TOA MAONI YAKO!
 
Hata chama chenyewe ni cha Vigogo au uliondoka nchini miaka mingi ndo uumerejea?Sema tukusaidie kukupa jinsi ilivyofikia leo tangu ilivyoanza...Hiki sio chama ila ni makundi ya Familia Marafiki...Wewe hujui kweli au unazuga
 
Hayo ni majungu yanakusumbua mbona Bush baba na Bush mtoto wote waliitawala USA? Sasa kuna ubaya gani kwa watoto wa wana siasa kugombea uongozi
 
Kuna tetesi kuwa majina mengi ya wajumbe wa UVCCM ni watoto wa vigogo! Kama habari yenyewe ni kweli basi tunakokwenda siko
TOA MAONI YAKO!

Mkuu haya hapa...., Dickson membe,Fredy lowasa, Ridhiwani Kikwete, Iren Pinda, Sharifa Bilaly, Ashura Hussein Mwinyi, Beny samweri Sita, Felister Ndugai, Deborah Mwandosya,Hawa kigoda, Judith mukama na Jalome msekwa......., wote wanaandaliwa kuwa viongozi wa nchi katika nyadhifa mbalimbali kulinda maslai ya wazee wao..mfano rahisi tuu waziri wa afya....,Sisi tutabaki humu humu tu JF tukiumiza vichwa vyetu watoto wa wakubwa wanachukua nchi na kututawala.. LIKE FATHER LIKE SON.!!!..Nchi ngumu sana hii.
 
Hiki chama kinaendeshwa kwa mfumo wa BMWV, Yaani Baba Mama, Watoto na Vimada.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom