Leo nataka tukumbushane mji wetu mkongwe,mji maarufu wenye historia kubwa ndani ya nchi hii lakini inayoelekea kupotea.Mko wapi watoto wa kariakoo wa ukweli mtueleze tuijue kariakoo iko vipi,ilikua vipi,raha na karaha za mitaa ya kariakoo,na je kariakoo ya zamani na ya sasa zinalingana?karibu sana maskani mnaoijua kariakoo kiundani mtujuze sie wakuja maana ndo kwanza tunaishi kwenye maghorofa mapya baada ya wenye mji kuukimbia mji wao,maana tumekuwa tukiyasikia mengi kuhusu mitaa hii ilivyokua zamani.