ngoshwe
JF-Expert Member
- Mar 31, 2009
- 4,131
- 931
Kuna kale ka sheria ka kulinda haki za watoto (The Childrens 2009)sijui utekelezaji wake umeishia wapi. Nipo hapa Arusha City Park (Rest in Peace) ni karibu kabisa na kituo kikuu cha polisi cha Arusha. Yapata saa mbili kasoro usiku sasa watoto wadogo wapo kibao wanabembea wakati wazazi wanakata kilevi. Hili ni eneo ambalo ma changu wa Arusha wanavinjari hovyo hovyo, sijui mamlaka za serikali hapa Arusha zinafikiriaje jambo hili la kuweka sehemu ya kucheza watoto kwenye baa?! Mungu tusaidie.