Wateja wa Taifa Gas tuwe makini

Wateja wa Taifa Gas tuwe makini

Mimi ni miongoni mwa watumiaji wa gesi ya Taifa Gas kwa ajili ya matumizi ya nyumbani. Wiki 4 zilizopita nilienda dukani kununua gesi [kubadilisha mtungi]. Wakati nauinua nikasikia kimiminika [gesi] ikicheza ndani kwa ombwe kubwa.

Kwa kuwa mwenye duka anao mzani [nilimshauri hivyo kufuatia agizo la serikali kuwa wauzaji wa gesib lazima waweke mizani ili wateja wahakiki ujazo] ilibidi niupime pale pale. Huwezi kuamini, kulikuwa na upungufu wa gm 950, yaani karibu kilo nzima! Akanipa mtungi mwingine, nao ukawa umepungua pia! Mtungi wa tatu ndio ukawa sawa.

Wiki iliyopita gesi ikawa imeisha, kwa kuwa sikuwa na pesa ya kutosha ikabidi nichuikue mtungi mdogo kabisa, na kwa kuwa imani yangu kwa Taifa Gas ilikuwa imepungua nikaamua kuupima. Amini usiamimini, nao ukawa umepungua! Nikachukua mtungi mwingine, nao ukawa umepungua vilevile hadi nilipopata mtungi wenye uzito sahihi.

Kwa uzoefu huu nawafahamisha wateja wenzangu wa Taifa Gas kuwa makini wanapobadilisha mitungi hiyo. Wito wangu kwa Taifa Gas ni kuwa watutendee haki wateja wao, mwenye duka aliniambia Oryx ndio mitungi ya uhakika, Oryx sio kampuni ka kizalendo, faida yao kwa sehemu kubwa inaenda kwa Wazungu, sasa huyu Mtanzania mwenzetu wa Taifa Gas anavyotufanyia uzalendo unaanza kunishinda.

Vv
Hii kampuni inamilikiwa na fisadi papa na dokozi lililokubuhu bw. Ristam Abdulrasul Aziz.... we endelea kujilengesha mdomoni mwa mamba!
 
Nitaanza kupima pia mkuu.

M binafsi natumia Taifa Gas simply kwa sababu ni ya mbongo, ila sasa kama mwenzetu anaamua kutufanyia uhuni tutaenda lake gas na kwingine sasa.
Rostam kaanza kuwafanyia uhuni leo nchi hii? Hivi watanzania mtaamka lini kutoka kwenye usingizi wa pono?
 
Itakua ni kweli kuna siku wife kamtuma mtu akachue gas ila akamwambia kwamba usinunue kwa " muha nunua kwa mangi sio majina halisi ya wahusika.

Nikamuliza kwann akasema hapo kwa muha inaisha haraka nikambishia na kumwambia una sababu zingine binafs kumbe kweli mambo haya yapo!!

Xmcha ajabu ni kwamba hawa wanauza huku mtaan hawana hiyo mizani unayosema
 
Hiyo ni kweli mm ni muuzaj WA ges nimekaa kwenye Hii industry miaka kama 6 sasa unachoongoea NI sahihi , na hilo tumewaambia mara nyingi lakini hawalifanyii Kazi kabisa,
Oryx na lake ni kampun Bora Sana zinazingatia ujazo

Sent from my SHG03 using JamiiForums mobile app
 
Hauna conflict of interest kweli mleta mada kwenye Biashara hii?
===
Hii ni tuhuma nzito, na unampaka kazi nzito Meneja masomo wa Taifa gesi. Kubwa kabisa, hii tuhuma ilitakiwa iambatane na ushahidi usiotiliwa shaka.kwa kueleza, ulinunua mitungi hiyo kwa duka la nani, mtaa gani, wilayagani. Pia ungeweka na ushindi wa picha ama video wakati unafanyia matukio yote haya.

Tujiepushe kutoa taarifa bila ushahidi. Na tuache kugombanisha makampuni. Suala la kuitaja Oryx gas moja kwa moja kwa mlengo huu katika uzi huu inaonyesha Nia ovu uliyonayo dhidi ya makampuni haya.
Mimi nipo tayar kutoa ushahidi ni muuza gesi WA muda mrefu hilo Jambo tumeongea Sana , , tena ushahidi ni simple Tu tunaenda kwa superdealer wao mmoja tunapima gesi , katika mitungi 10 , mitatu ndo itakuwa imejaa vizur

Sent from my SHG03 using JamiiForums mobile app
 
Hauna conflict of interest kweli mleta mada kwenye Biashara hii?
===
Hii ni tuhuma nzito, na unampaka kazi nzito Meneja masomo wa Taifa gesi. Kubwa kabisa, hii tuhuma ilitakiwa iambatane na ushahidi usiotiliwa shaka.kwa kueleza, ulinunua mitungi hiyo kwa duka la nani, mtaa gani, wilayagani. Pia ungeweka na ushindi wa picha ama video wakati unafanyia matukio yote haya.

Tujiepushe kutoa taarifa bila ushahidi. Na tuache kugombanisha makampuni. Suala la kuitaja Oryx gas moja kwa moja kwa mlengo huu katika uzi huu inaonyesha Nia ovu uliyonayo dhidi ya makampuni haya.
Kinachotakiwa sasa, wewe uondoke na uende kwenye maduka hayo ya taifa gas ili uthibitishe kuwa kilichosemwa na mhusika siyo KWELI. Badala ya kupinga wazo bila USHAHIDI.
 
Mimi nipo tayar kutoa ushahidi ni muuza gesi WA muda mrefu hilo Jambo tumeongea Sana , , tena ushahidi ni simple Tu tunaenda kwa superdealer wao mmoja tunapima gesi , katika mitungi 10 , mitatu ndo itakuwa imejaa vizur

Sent from my SHG03 using JamiiForums mobile app
Watakuwa wanajua mchezo wote hao wanajikausha

Ila in the longrun kibiashara kwenye biashara yenye ushindani kampuni itakufa

Uongo kwenye huwa hauna maisha marefu sana
 
Mimi ni miongoni mwa watumiaji wa gesi ya Taifa Gas kwa ajili ya matumizi ya nyumbani. Wiki 4 zilizopita nilienda dukani kununua gesi [kubadilisha mtungi]. Wakati nauinua nikasikia kimiminika [gesi] ikicheza ndani kwa ombwe kubwa.

Kwa kuwa mwenye duka anao mzani [nilimshauri hivyo kufuatia agizo la serikali kuwa wauzaji wa gesib lazima waweke mizani ili wateja wahakiki ujazo] ilibidi niupime pale pale. Huwezi kuamini, kulikuwa na upungufu wa gm 950, yaani karibu kilo nzima! Akanipa mtungi mwingine, nao ukawa umepungua pia! Mtungi wa tatu ndio ukawa sawa.

Wiki iliyopita gesi ikawa imeisha, kwa kuwa sikuwa na pesa ya kutosha ikabidi nichukue mtungi mdogo kabisa, na kwa kuwa imani yangu kwa Taifa Gas ilikuwa imepungua nikaamua kuupima. Amini usiamimini, nao ukawa umepungua! Nikachukua mtungi mwingine, nao ukawa umepungua vilevile hadi nilipopata mtungi wenye uzito sahihi.

Kwa uzoefu huu nawafahamisha wateja wenzangu wa Taifa Gas kuwa makini wanapobadilisha mitungi hiyo. Wito wangu kwa Taifa Gas ni kuwa watutendee haki wateja wao, mwenye duka aliniambia Oryx ndio mitungi ya uhakika, Oryx sio kampuni ka kizalendo, faida yao kwa sehemu kubwa inaenda kwa Wazungu, sasa huyu Mtanzania mwenzetu wa Taifa Gas anavyotufanyia uzalendo unaanza kunishinda.

Vv
Ndio nchi yenu hiyo....imejaa janja janja tupu.
 
Hii ni kweli, mihan inaisha haraka kuliko oryx.
TBS na Watu wa taasisi ya vipimo na mizani waingie kazini haraka

Waende na mizani yao kila kona ya nchi kwa kuvamia maduka ghafla wapime
 
Rostam kaanza kuwafanyia uhuni leo nchi hii? Hivi watanzania mtaamka lini kutoka kwenye usingizi wa pono?
Kwa hio unashaurije 🤔
Kampuni gani hii nchi haifanyi uhuni ? Tunaenda nao hivo hivo ila hata wew

Am sure ulikoajiriwa/jiajiri unafanyia watu uhuni,

Nchi hii kila mtu muhuni sema tunaenda hivo hivo, hakuna malaika kabisa, tumpe nafasi Rostam, licha ya uhuni ila anasaidia, Voda ipo nchi nzima inapata mawasiliano kwa ajiili ya kazi yake kubwa, saizi tigo pia kwa ajiili yake, uhuni upo ila tunavumiliana na kukosoana tupatapo nafasi
 
Kinachotakiwa sasa, wewe uondoke na uende kwenye maduka hayo ya taifa gas ili uthibitishe kuwa kilichosemwa na mhusika siyo KWELI. Badala ya kupinga wazo bila USHAHIDI.
Mkuu sijapinga wazo, bali nimekataa packaging ya wazo kwa namna lilivyoletwa hapa jukwaani. Yaani wazo limetetwa likiwa na mapungufu ya ushahidi. Na ushahidi ni jambo muhimu Sana katika kutafuta suluhisho la changamoto inayojitokeza popote!

Binafsi naona ni jambo jema sana kuleta tuhuma hizi zikiwa na ushahidi timilifu ili tuhuma hii ifanyiwe kazi na wahusika au Mamlaka husika (Weight and Measures Authority).
 
Ni kweli Taifa gas Wana hii shida me mwenyew nilienda kuchange mtungi nikamwambia yule muuzaji apime, aise alikuwa na mitungi imebaki minne na yote haikutimia ujazo ulio andikwa pale juu ya mtungi, kila mtungi ulikuwa na kilo pungufu,,nikamuuliza muuzaji mbona hivi shida ni nn akaaza kujitetea kwamba yye mwenyew hajui ila nikawaida tu coz ni point chache tu zimepungua ikabidi nichukue hivohivo,,

Ila hii nchi janja janja hazijaaza Leo hasahasa Kwa wafanya biashara wakubwa serikali inawabana wafanyabiashara wadogo lakn Hawa vibopa hawaguswi so hili jambo litabakia kama kilio Cha samaki.
 
Kwa hio unashaurije 🤔
Kampuni gani hii nchi haifanyi uhuni ? Tunaenda nao hivo hivo ila hata wew

Am sure ulikoajiriwa/jiajiri unafanyia watu uhuni,

Nchi hii kila mtu muhuni sema tunaenda hivo hivo, hakuna malaika kabisa, tumpe nafasi Rostam, licha ya uhuni ila anasaidia, Voda ipo nchi nzima inapata mawasiliano kwa ajiili ya kazi yake kubwa, saizi tigo pia kwa ajiili yake, uhuni upo ila tunavumiliana na kukosoana tupatapo nafasi
Sasa unalalamika nini we kima?
 
Hauna conflict of interest kweli mleta mada kwenye Biashara hii?
===
Hii ni tuhuma nzito, na unampaka kazi nzito Meneja masomo wa Taifa gesi. Kubwa kabisa, hii tuhuma ilitakiwa iambatane na ushahidi usiotiliwa shaka.kwa kueleza, ulinunua mitungi hiyo kwa duka la nani, mtaa gani, wilayagani. Pia ungeweka na ushindi wa picha ama video wakati unafanyia matukio yote haya.

Tujiepushe kutoa taarifa bila ushahidi. Na tuache kugombanisha makampuni. Suala la kuitaja Oryx gas moja kwa moja kwa mlengo huu katika uzi huu inaonyesha Nia ovu uliyonayo dhidi ya makampuni haya.
Whaaat? Kweli nchi hii tumefika kubaya. Ukisema kuna ufisadi sehemu fulani unaambiwa nenda mahakamani. Hili la mteja kulalamika nalo mpaka atumie process ndefu namna hii? Utaula wa chuya na huyu mwizi muuza gas. Jamani watu wenye nyodo kama hawa mnawaachia biashara yao mnahamia kwingine. ORYX NDIYO HABARI YA MJINI. KATAA UTAPELI WA TAIFA GAS.
 
Ili kuwasaidia wengine.
  • Mtungi mdogo unatakiwa uwe kg ngapi?
  • Mtungi wa kati unatakiwa uwe kg ngapi?
  • Mtungi mkubwa unatakiwa uwe na kg ngapi?
Kila mtungi una uzito tofauti, nadhani inategemea umetengenezwa lini. Mtungi mwingine unaweza kusoma kilo 20, mwingine 18. Muhimu ni kuhakikisha kuwa uzito wa mtungi una uzito ulioandikwa.

Vv
 
Kwa hio unashaurije 🤔
Kampuni gani hii nchi haifanyi uhuni ? Tunaenda nao hivo hivo ila hata wew

Am sure ulikoajiriwa/jiajiri unafanyia watu uhuni,

Nchi hii kila mtu muhuni sema tunaenda hivo hivo, hakuna malaika kabisa, tumpe nafasi Rostam, licha ya uhuni ila anasaidia, Voda ipo nchi nzima inapata mawasiliano kwa ajiili ya kazi yake kubwa, saizi tigo pia kwa ajiili yake, uhuni upo ila tunavumiliana na kukosoana tupatapo nafasi
Pumbavu kabisa wewe. Usirudie tena kutoka fyongo kama hizi. Unahalalisha wizi?
 
Mimi ni miongoni mwa watumiaji wa gesi ya Taifa Gas kwa ajili ya matumizi ya nyumbani. Wiki 4 zilizopita nilienda dukani kununua gesi [kubadilisha mtungi]. Wakati nauinua nikasikia kimiminika [gesi] ikicheza ndani kwa ombwe kubwa.

Kwa kuwa mwenye duka anao mzani [nilimshauri hivyo kufuatia agizo la serikali kuwa wauzaji wa gesib lazima waweke mizani ili wateja wahakiki ujazo] ilibidi niupime pale pale. Huwezi kuamini, kulikuwa na upungufu wa gm 950, yaani karibu kilo nzima! Akanipa mtungi mwingine, nao ukawa umepungua pia! Mtungi wa tatu ndio ukawa sawa.

Wiki iliyopita gesi ikawa imeisha, kwa kuwa sikuwa na pesa ya kutosha ikabidi nichukue mtungi mdogo kabisa, na kwa kuwa imani yangu kwa Taifa Gas ilikuwa imepungua nikaamua kuupima. Amini usiamimini, nao ukawa umepungua! Nikachukua mtungi mwingine, nao ukawa umepungua vilevile hadi nilipopata mtungi wenye uzito sahihi.

Kwa uzoefu huu nawafahamisha wateja wenzangu wa Taifa Gas kuwa makini wanapobadilisha mitungi hiyo. Wito wangu kwa Taifa Gas ni kuwa watutendee haki wateja wao, mwenye duka aliniambia Oryx ndio mitungi ya uhakika, Oryx sio kampuni ka kizalendo, faida yao kwa sehemu kubwa inaenda kwa Wazungu, sasa huyu Mtanzania mwenzetu wa Taifa Gas anavyotufanyia uzalendo unaanza kunishinda.

Vv
Bwana kagoda au richard monduli!
 
Back
Top Bottom