Mwiba
JF-Expert Member
- Oct 23, 2007
- 7,607
- 1,764
Yanaweza maisha yakabadilika iwapo watawala wapya watakuwa na msimamo wa dhati wa kuyasikiliza na kuyatii wayatakayo wananchi,wakiupiga vita ufukara na wakiwatia adabu wanaopatikana na hatia ya ufisadi. Wakati huohuo wawe na mkakati madhubuti wa kujiepusha na mitego ya ulibirali mamboleo.
Vyama vya upinzani kwa upande wao vitabidi vizidishe ushirikiano wao ili viweze na kuwa mbali kutofautiana na utawala wa kiccm.Itafurahisha kwamba vinayaangalia matatizo ya Tanzania kwa mtazamo wa kitabaka kwa sababu Tanzania ni taifa lenye ufukara mkubwa na hali za maisha za wengi wanaoishi vijijini na mijini zinazidi kudidimia na za kukatisha tamaa.
UKAWA waonyeshe kama vina mikakati madhubuti ya kuwatetea wakulima wadogowadogo vijijini au wafanya kazi wa mijini wanaoishi katika makazi duni, yaani mitaa iliyoibuka ovyo ovyo bila ya mpango. Wenzetu wa Pwani ya Kenya kwa Kiswahili chao cha Mvita huiita mitaa aina hiyo "magengeni". Asilimia 70 ya wakazi wa sehemu za mjini hapa Tanzania wanaishi katika mitaa kama hiyo.
Ubaya wa mambo ni kwamba ukuaji wa nchi, kama ulivyo ukuaji wa nchi nyingine, hauendi sambamba na upangaji madhubuti wa miji. Mipango iliyopo ni ya kiholelaholela tu ,ya kiccm toa hela jenga popote. Matokeo yake ni kutanuka ovyo ovyo na mwishowe kugeukiana na kuvunjiana. Hakuna utaratibu au nidhamu yoyote inayofuatwa.
Ukawa wajikite zaidi katika kuweka mikakati ya muda mrefu sio ya kiccm baada ya miaka selasini ,kumfanya mwananchi aridhike na maisha ya mkoani au kijijini kwake na waiondoe tabia ya kushuka DSM au kwenye miji mikuu.
Kwani wengi wao wanapotelemka mijini kutoka vijijini huwa na matumaini makubwa kwamba hali zao za maisha zitatengenea wakitumai watapata uwezo wa kufanya hivyo. Lakini kila wakilala na kuamka polepole huanza kutanabahi kwamba huo uwezo unawapiga chenga. Hawapati uwezo wowote wa kufanya chochote ila kuendelea kuishi maisha ya dhiki.Mwaka unapita, mitatu mingine inapita na hapo ndipo inapowatwanga kwamba maisha yao yataselelea vivyo hivyo.
Licha ya yote yanayowakuta watu hao hawakati tamaa. Wanapojibwaga sakafuni kwenye vigodoro vembamba au mikeka bado hulala na ndoto na huamka na ndoto. Ndoto kwamba hali zao zitabadilika ili wao pia waweze kununua bidhaa katika maduka makubwa. Ndoto ya kuwa kuna siku watakuwa wateja wa halali na sio watu wenye kuzikodolea macho tu bidhaa za anasa. Kwa bahati mbaya, tamaa huwafanya baadhi yao wawe mabazazi na wezi.
Ukawa ni lazima mucwe mnachukua ahadi za kuinua maisha ya mwananchi kwa dhati kabisa sio zile blah blah za kiccm. mwisho wa siku mnatupiga virungu,mnatuletea mgambo wa jiji,mnatuvunjia nyumba ,mnatupeleka mahakamani kwa sababu za kiuonevu kabisa zinazoshinikizwa na wenye madaraka au wenye hela. Lazima mjenge misingi ya uongozi bora kuanzia sasa .
Vyama vya upinzani kwa upande wao vitabidi vizidishe ushirikiano wao ili viweze na kuwa mbali kutofautiana na utawala wa kiccm.Itafurahisha kwamba vinayaangalia matatizo ya Tanzania kwa mtazamo wa kitabaka kwa sababu Tanzania ni taifa lenye ufukara mkubwa na hali za maisha za wengi wanaoishi vijijini na mijini zinazidi kudidimia na za kukatisha tamaa.
UKAWA waonyeshe kama vina mikakati madhubuti ya kuwatetea wakulima wadogowadogo vijijini au wafanya kazi wa mijini wanaoishi katika makazi duni, yaani mitaa iliyoibuka ovyo ovyo bila ya mpango. Wenzetu wa Pwani ya Kenya kwa Kiswahili chao cha Mvita huiita mitaa aina hiyo "magengeni". Asilimia 70 ya wakazi wa sehemu za mjini hapa Tanzania wanaishi katika mitaa kama hiyo.
Ubaya wa mambo ni kwamba ukuaji wa nchi, kama ulivyo ukuaji wa nchi nyingine, hauendi sambamba na upangaji madhubuti wa miji. Mipango iliyopo ni ya kiholelaholela tu ,ya kiccm toa hela jenga popote. Matokeo yake ni kutanuka ovyo ovyo na mwishowe kugeukiana na kuvunjiana. Hakuna utaratibu au nidhamu yoyote inayofuatwa.
Ukawa wajikite zaidi katika kuweka mikakati ya muda mrefu sio ya kiccm baada ya miaka selasini ,kumfanya mwananchi aridhike na maisha ya mkoani au kijijini kwake na waiondoe tabia ya kushuka DSM au kwenye miji mikuu.
Kwani wengi wao wanapotelemka mijini kutoka vijijini huwa na matumaini makubwa kwamba hali zao za maisha zitatengenea wakitumai watapata uwezo wa kufanya hivyo. Lakini kila wakilala na kuamka polepole huanza kutanabahi kwamba huo uwezo unawapiga chenga. Hawapati uwezo wowote wa kufanya chochote ila kuendelea kuishi maisha ya dhiki.Mwaka unapita, mitatu mingine inapita na hapo ndipo inapowatwanga kwamba maisha yao yataselelea vivyo hivyo.
Licha ya yote yanayowakuta watu hao hawakati tamaa. Wanapojibwaga sakafuni kwenye vigodoro vembamba au mikeka bado hulala na ndoto na huamka na ndoto. Ndoto kwamba hali zao zitabadilika ili wao pia waweze kununua bidhaa katika maduka makubwa. Ndoto ya kuwa kuna siku watakuwa wateja wa halali na sio watu wenye kuzikodolea macho tu bidhaa za anasa. Kwa bahati mbaya, tamaa huwafanya baadhi yao wawe mabazazi na wezi.
Ukawa ni lazima mucwe mnachukua ahadi za kuinua maisha ya mwananchi kwa dhati kabisa sio zile blah blah za kiccm. mwisho wa siku mnatupiga virungu,mnatuletea mgambo wa jiji,mnatuvunjia nyumba ,mnatupeleka mahakamani kwa sababu za kiuonevu kabisa zinazoshinikizwa na wenye madaraka au wenye hela. Lazima mjenge misingi ya uongozi bora kuanzia sasa .