Kichuguu
Platinum Member
- Oct 11, 2006
- 15,571
- 19,453
Watu wengi huamaini kuwa nchi za kiislamu huwa haziwaheshimu wanawake na haziwezi kutawaliwa na wanawake. Hata hivyo miaka ya hivi karibuni imeonakana kuwa hilo siyo kweli kwani kule Pakistani walitawaliwa na mwanamke Benazir Bhutto kwa muda mrefu kabla hawajamuua.
Ninataka kuchokonoa historia ya mtawala mmoja wa kike kule Nigeria ya kaskazini kwenye jamii ya wahausa ambayo ni ya kiislamu kwa muda mrefu sana aliyekuwa akiitwa malkia Amina. Mama huyu alitawala takriban miaka 200 kabla ya ujio wa Usman dan Fodio ambaye ndiye anyejulikana sana eno hilo kihistoria. Amina alikuwa ni mtoto kwanza wa mfalme Nikatau aliyekuwa anatawala kule kaskazini mwa Nigeria. Alikuwa na wadogo zake watatu; mdogo wake wa kiume alikuwa mtoto wa pili wa mfalme Nikatau alikuwa akiitwa Karama, halafu mdogo wake wa kike alikuwa akiitwa Zaria; leo hii kuna mji kule kaskazini mwa Nigeria unaitwa Zaria kwa sababu ya huyu mdogo wake wa kike.
Amina alijifunza kupigana vita angali kigoli wakati akiwa anaishi na babu yake; baada ya baba yake kufa, mdogo wake wa kiume ndiye aliyerithi ufalme wakati Amina akiwa anendelea na maisha ya kijeshi ya kupigana vita aliyokuwa amejifunza kutoka kwa babu yake; alikuwa msichana mrembo sana ambaye pamoja na ushujaaa wake wa kijeshi wanaume wengi walitaka kumwoa lakini hakuna aliyefanikiwa. Baada ya kukaa madarakani kwa miaka kumi, kaka yake, yaani mfalme Karama, naye alifariki, na hivyo Amina kuchukua mamlaka ya kuwa mtawala wa eneo hilo akijulikana kama malkia Aminatu.
Malkia Aminatu anakumbukuwa sana kwa kuliendeleza eneo la Zaria hadi kuwa kitovu kikubwa cha biashara kaskazini mwa Nigeria kama ilivyo leo.
Ninataka kuchokonoa historia ya mtawala mmoja wa kike kule Nigeria ya kaskazini kwenye jamii ya wahausa ambayo ni ya kiislamu kwa muda mrefu sana aliyekuwa akiitwa malkia Amina. Mama huyu alitawala takriban miaka 200 kabla ya ujio wa Usman dan Fodio ambaye ndiye anyejulikana sana eno hilo kihistoria. Amina alikuwa ni mtoto kwanza wa mfalme Nikatau aliyekuwa anatawala kule kaskazini mwa Nigeria. Alikuwa na wadogo zake watatu; mdogo wake wa kiume alikuwa mtoto wa pili wa mfalme Nikatau alikuwa akiitwa Karama, halafu mdogo wake wa kike alikuwa akiitwa Zaria; leo hii kuna mji kule kaskazini mwa Nigeria unaitwa Zaria kwa sababu ya huyu mdogo wake wa kike.
Amina alijifunza kupigana vita angali kigoli wakati akiwa anaishi na babu yake; baada ya baba yake kufa, mdogo wake wa kiume ndiye aliyerithi ufalme wakati Amina akiwa anendelea na maisha ya kijeshi ya kupigana vita aliyokuwa amejifunza kutoka kwa babu yake; alikuwa msichana mrembo sana ambaye pamoja na ushujaaa wake wa kijeshi wanaume wengi walitaka kumwoa lakini hakuna aliyefanikiwa. Baada ya kukaa madarakani kwa miaka kumi, kaka yake, yaani mfalme Karama, naye alifariki, na hivyo Amina kuchukua mamlaka ya kuwa mtawala wa eneo hilo akijulikana kama malkia Aminatu.
Malkia Aminatu anakumbukuwa sana kwa kuliendeleza eneo la Zaria hadi kuwa kitovu kikubwa cha biashara kaskazini mwa Nigeria kama ilivyo leo.