Watapeliwa viwanja Kibaha

Watapeliwa viwanja Kibaha

Dah! Siku hizi kila mtu anakula lwa urefu wa kamba yake. Ukizubaa tu, umepigwa.
Kwenye hili na Mitamba serikali inasehemu kubwa ya lawama
.Eneo liliachwa kuwa pori kwa miaka mingi
.Halmashauri ya Kibaha haikuchukua hatua mapema wavamizi na matapeli walipoanza biashara ya viwanja
. Viongozi na watendaji nao hawakuchukiliwa hatua mapema nao walipojiingiza kwenye hiyo biashara ya kitapeli
. Kwasababu zisizojulikana pori likaachwa bila kufyekwa wala kuhudumiwa na kugeuka pori la maasi, mauaji, vibaka, ujambazi na shughuli za kishirikina
Unamkumbuka yule binti aliyechomwa moto? Alichomewa huko Mitamba...
Bodaboda wengi wameuliwa huko na kuporwa pikipiki zao
Ni kawaida pori la Mitamba kuokota maiti zilizokwisha oza na kuharibika kabisa.. Hapo sijazungumzia makaburi

Baada ya Mabwepande sasa ni Mitamba.. Ukipelekwa huko.. Kutoka salama ni majaliwa ya mbingu

Viwanja vilivyouzwa na kujengwa mijengo ya maana tena kwa nyaraka halali na kupatiwa huduma zote muhimu za kijamii kama umeme na maji ni vingi sana
Serikali ikubali kukosea.. Iwawajibishe waliopiga dili lakini waliokwisha jenga na kufanya maendeleo waachwe tu maana ni wengi mno

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ukiona mambo yanaenda hovyo kwenye hili taifa tambua kule juu sio imara! janja ipo sana

Dalali anatakiwa atambulike na mahakama na awe na leseni.

Hao wenye viti wa mitaa na mabalozi njaa mingi ni rahisi kushawishika watengeeni fungu angalau posho na sheria ziwepo kali kuuza eneo bila halmashauri kuwa na taarifa nalo liwe kosa!

Migogoro ya ardhi kila kikucha haipungui zaidi ya kuongezeka ukitaka ardhi hata kama ni ya mtu binafsi nenda kwenye mamlaka husika ujiridhishe!

Kuepuka kero za kuhudhuria mahakamani na hela nayo umeshapigwa dalali nae muda huo hayupo!
 
Hili linatokana na watu wenyewe kufanya vitu bila kujiridhisha,Mfano mtu anakwambia anauza viwanja vimepimwa lakini ukimwambia akupe approved survey plan hana,anakuambia bado haijatoka ,sasa unajiuliza huo upimaji wake ana uhakika gan nao? Coz survey plan kibao huwa zinakataliwa kutokana na kukosa vigezo vilivyo ainishwa

Ukiachana na hili watu wananunua ardhi bila kujiridhisha na umiliki wa anayekuuzia
Mkuu kwa Tz ni maeneo mangapi yamepimwa??? Karibu asilimia 80 ya viwanja havijapimwa, ni maeneo holela tu, kidogo sasa hivi ndio serikali imeamka kwa lile zoezi la UMILIKISHAJI WA ARDHI.
 
Mkuu kwa Tz ni maeneo mangapi yamepimwa??? Karibu asilimia 80 ya viwanja havijapimwa, ni maeneo holela tu, kidogo sasa hivi ndio serikali imeamka kwa lile zoezi la UMILIKISHAJI WA ARDHI.
Uko sahihi mkuu .... lakini kutokana na hili wimbi kubwa la utapeli wa viwanja we unafikiri suluhisho nini?
 
Hao viongozi wa mtaa, wenyekiti hawafai wamekosa weledi watumbuliwe tu.
 
Uko sahihi mkuu .... lakini kutokana na hili wimbi kubwa la utapeli wa viwanja we unafikiri suluhisho nini?
Yaani kwa mfumo mbovu wa ardhi Tz, ni ngumu sana kujihakikishia uko salama 100% hasa kwa hivi viwanja ambavyo havijapimwa, kwani mtu atakupa hati ya mauziano ile ya serikali ya mtaa, huwezi jua kama kuna mwinginr tena anayo hiyo hiyo tena, mzozo unapoibuka muuzaji anakuwa amewaachia tatizo, mimi yalinikuta nilipambana kama miaka 3 mahakamani hadi kikaeleweka, hao wenyeviti wa mitaa, huwa hawana misaada kabisa mbele ya sheria pale panapoibuka mgogoro!!
 
Kwenye hili na Mitamba serikali inasehemu kubwa ya lawama
.Eneo liliachwa kuwa pori kwa miaka mingi
.Halmashauri ya Kibaha haikuchukua hatua mapema wavamizi na matapeli walipoanza biashara ya viwanja
. Viongozi na watendaji nao hawakuchukiliwa hatua mapema nao walipojiingiza kwenye hiyo biashara ya kitapeli
. Kwasababu zisizojulikana pori likaachwa bila kufyekwa wala kuhudumiwa na kugeuka pori la maasi, mauaji, vibaka, ujambazi na shughuli za kishirikina
Unamkumbuka yule binti aliyechomwa moto? Alichomewa huko Mitamba...
Bodaboda wengi wameuliwa huko na kuporwa pikipiki zao
Ni kawaida pori la Mitamba kuokota maiti zilizokwisha oza na kuharibika kabisa.. Hapo sijazungumzia makaburi

Baada ya Mabwepande sasa ni Mitamba.. Ukipelekwa huko.. Kutoka salama ni majaliwa ya mbingu

Viwanja vilivyouzwa na kujengwa mijengo ya maana tena kwa nyaraka halali na kupatiwa huduma zote muhimu za kijamii kama umeme na maji ni vingi sana
Serikali ikubali kukosea.. Iwawajibishe waliopiga dili lakini waliokwisha jenga na kufanya maendeleo waachwe tu maana ni wengi mno

Sent using Jamii Forums mobile app
Naona bimepandishwa TAUSI, nahisi kuna walioamua kununua mara mbili viwanja vyao kukwepa kubomolewa au huu utaratibu haupo?
 
Suruhisho tu hapa serikali ingepima viwanja vyote na vikawa vinauzwa kupitia kwenye mfumo mtandaoni au unachagua kiwanja kwenye mfumo unaomba upewe control namba unalipa ili hawa madalali wote wasiwepo na hata wenyeviti wa vijiji na watendaji kwasasa nao ni matapeli wengi tu
 
ndio maana kwa Dar au miji yote hii kununua kiwanja unahitaji uangalifu mkubwa sana ni afadhali hata kununua nyumba kabisa
 
Ununuaji wa ardhi unahitaji umakini sana
Hasa kwa maeneo ambayo yanavutia sana na yanaonekana kama hayana mwenyewe. Muda mwingi maeneo hayo yanakuwa mali ya serikali.
 
Back
Top Bottom