Hapo nitakupinga, awamu ya kwanza utailaumu bure. Ni sawa na mtu mzima anayemlalamikia baba yake kuwa hakumsomesha ndio sababu ya yeye kuwa na maisha magumu, anasahau wapo wenzake wamepata elimu wakiwa jela.
Ukirudi kwenye hoja yako,ni kweli awamu ya kwanza iliacha katiba mbovu,na hata Mwalimu Nyerere aliwahi kukiri hivyo waziwazi,hata hivyo hata Kenya hawakuwa na katiba nzuri,tulikuwa na tofauti ndogo tu, isipokuwa Wakenya waliamka kudai mabadiliko ya katiba bila woga,na pamoja na machafuko ya 2007 ambayo yalisukuma kupatikana kwa katiba mpya 2010, bado ukweli unabakia kwamba siye itatuchukua muda mrefu sana kuwa na katiba angalau kama ya Kenya,siye tuko too complacent.
2015 alivyoingia Magufuli,tukaridhika na utendaji wake, hata wale waliokuwa mstari wa mbele kudai katiba,km akina Polepole na Prof. Kabudi wakaridhika kwamba katiba hahitajiki tena kitu ambacho ni ujinga ulitufunika kwa kuamini mtu na kumsahau Mungu, na yaliyotokea ni historia.
Kama kweli tunahitaji mabadiliko ya kweli ni sisi kuamua na kuacha kubakia kulalamika eti tuliachiwa katiba mbovu na awamu ya kwanza, mbona tulidai vyama vingi na Mwalimu huyohuyo akaunga mkono akiwa Mwenyekiti wa ccm!!
Watawala wanatufahamu ni wepesi wa kuridhika na ndio sababu tukiona akina Makonda wakifokea watu kwenye majukwaa tunachekelea,tunasahau kuwa tunahitaji mfumo utakaosimamia mambo yetu bila ghiliba za viongozi za kutembea na makamera na waandishi machawa kutuzuga.
Katikati ya changamoto ya ukosefu wa umeme wao wako busy na vitoto vyao eti kwenye mkutano wa chipukizi,halafu utegemee kuna suluhu bila wananchi kuamka na kuwakataa na wajue tumewakataa.