Watanzania wengi tuna uraibu wa kukopa

ubarinolutu

JF-Expert Member
Oct 22, 2012
1,964
3,895
Suala la kuchukua mikopo ni muhimu na ni Chachu ya Maendeleo ya mtu na biashara yake kiujumla.

Ila Kuna watu hawastaili kuingia kwenye hii mikopo ambayo inasababisha vilio vya Kila siku hasa Kwa kina mama, huku wengi wao wakibaki kutumika kimapenzi bila shurti hasa Kwa mikopo midogo.

Nimekuja kugundua kumbe Kukopa ni ulevi na inaleta uraibu kama ule wa pombe, Kuna jamaa mmoja tunafanya nae kazi ofisini yeye ni Mzee wa Kukopa, mtaani Kila mtu anamdai, ofisi imemkopa, staff wamemkopa, bank mbili zimemkopa, amemshauri na mkewe nae amekopa bank. Huyu jamaa asipokopa anaumwa, ila afadhali huyu ana kazi, Kuna wale wenye biashara ndogo, Kuna ndugu yangu alikufa sukari na presha zilipanda kwakuwa alishindwa kufanya marejesho na lodge zake mbili zikauzwa.

Sasa naona Kuna rafiki yangu wa karibu sana ameshaingia kwenye hii michezo ya Kukopa na ananogewa Sasa hivi anataka akaweke nyumba na hapo awalinalikopa Kwa Kiwanja nikamsaidia kidogo Kiwanja kiende na vimkopo vya sakosi, Sasa anataka kuweka nyumba aende bank kabisa ila naona anapotea, namshaurije.

Hata matajiri wanakopa, ila Kukopa kunakuhitaji uwe na akili mnooo.

Kama unaweza kudunduliza dunduliza usikope, Kukopa Kuna wenyewe wataalamu
 
Kuna mtumishi alikopa milioni 50, 15 akanunulia gari la kutembelea KISHA akachukua milioni 5 akafanya sherehe ya eti kuaga umasikini, 30 akaziingiza kwenye biashara.

Alichokutana nacho kwenye hizi biashara zenye faida kwenye makaratasi na sio field kwenye ukweli halisi alishia kupata pressure tu
 
duh hapa nna deni la laki 2 la kamilisha nililokopa kununua mabando ya mwezi ya data ambayo yanaisha ndani ya week moja na kukamilisha miamala ya hapa na pale kwa uvivu wa kwenda ATM nikajiaminisha nitalipa baadae, ila mpaka sasa hivi ATM bila bila na Airtel sijawalipa.

Morocco HQ mkiiona hii post nihurumieni japo mnisamehe deni, maana hamna la maana nilofanya, nimekosa sana, nimekosa mimi.

Aliyegundua mikopo ana nafasi yake jehanam tena kaandaliwa kitanda cha 6*6
 
Suala la kuchukua mikopo ni muhimu na ni Chachu ya Maendeleo ya mtu na biashara yake kiujumla.

Ila Kuna watu hawastaili kuingia kwenye hii mikopo ambayo inasababisha vilio vya Kila siku hasa Kwa kina mama, huku wengi wao wakibaki kutumika kimapenzi bila shurti hasa Kwa mikopo midogo.
Mkopo (Leverage),ni silaha ambayo inaweza kukupa manufaa au kukuua kabisa kama hutajua namna ya kuihandle. Asilimia 90%+ ya wafanyabiashara unaowajua wanakopa, wanalipa halafu wanakopa tena.

Wafanyabiashara wanakopa ili kuongeza nguvu kwenye mitaji yao ambayo haiwezi ku service demand kubwa walizonazo ambazo ki uhalisia ndio vyanzo vya marejesho yao.
 
Kiukweli kabla hujachukua mkopo jiulize maswali mengi sana. Halafu chukua mkopo kipindi huhitaji kabisa mkopo. Itakuwa rahisi kuizungusha ile hela na kurudisha mkopo kwa wakati kwa sababu huna stress. Na chukua tu kidogo. Kama unaweza chukua milioni 10 basi chukua robo ya hiyo 2.5m. Hii itasaidia kutengeneza jina kwenye taasisi za fedha hasa benki. Ukichukua mkopo wakati una shida zimekubana huwa ni hatari sana.
 
Mkopo (Leverage),ni silaha ambayo inaweza kukupa manufaa au kukuua kabisa kama hutajua namna ya kuihandle. Asilimia 90%+ ya wafanyabiashara unaowajua wanakopa, wanalipa halafu wanakopa tena.
Wafanyabiashara wanakopa ili kuongeza nguvu kwenye mitaji yao ambayo haiwezi ku service demand kubwa walizonazo ambazo ki uhalisia ndio vyanzo vya marejesho yao.
Exactly
 
Back
Top Bottom