Watanzania wameombwa kupaza sauti zao kulaani mashambulizi ya Makombora yanayofanywa na Taifa la Israel kwenye ukanda wa Gaza eneo la Palestina

TEAM 666

JF-Expert Member
Dec 7, 2017
4,330
8,421
Rai hiyo imetolewa leo Jijini Dar es Salaam na Balozi wa Palestina nchini Tanzania, Hamdi Mansour Abuali,wakati akizungumza na waandishi wa habari akizungumzia juu ya machafuko yanaendelea kati ya Israel na Palestina.

Aidha,Balozi Abuali amesema mashambulizi hayo yamekuwa yakitoa roho za watu wasiokuwa na hatia.

Balozi Abuali,amesema mbali na kuondoa roho za watu,machafuko hayo yamewaacha zaidi ya milioni 2.2 ya Palestina wakiwemo watoto kukosa mahali pakukaa.

"Hakuna mafuta,hakuna umeme,hakuna chakula,hakuna maji yaani kila kitu kimefungwa,zaidi ya watu 1300 wamekufa,watoto wakiwemo 344,makazi 790 yameharibiwa huku zaidi ya wapalestina 339,000 wameyakimbia makazi yao"Amesema Abuali.

Hata hivyo,Balozi Abuali amezitaka jumuiya za kimataifa kupinga kile alichokiita ukatili unaofanywa na Israeli kwa wananchi wa Palestina

Naye, Mwenyekiti wa kamati ya mshikamano kati ya Tanzania na Palestina, Abdulaha Athuman, amewataka watanzania waungane kwa pamoja kulisaidia Taifa la Palestina kulaani kile kinachofanywa na Islaeri kwa Taifa la Palestina.

Athumani,Amesema Taifa la Palestina kwa miaka mingi limekuwa likisaidia mataifa ya Afrika ikiwemo ukombozi wa uhuru kwenye baadhi ya nchini za Afrika.
 
Rai hiyo imetolewa leo Jijini Dar es Salaam na Balozi wa Palestina nchini Tanzania, Hamdi Mansour Abuali,wakati akizungumza na waandishi wa habari akizungumzia juu ya machafuko yanaendelea kati ya Israel na Palestina...
Nadhani anapaswa kuwauliza hamas kwanini walilianzisha. na waache kulialia, asifikiri kila mtu hapa bongo anasapoti palestina.
 
Mimi ni mtanzani lakini siwezi kupelekeshwa na wavaa vipedo na makobazi kuilaani Israeli.Yaani wao walianzishe kuichokoza Israeli 🇮🇱 halafu sisi tuingizwe kwenye mkumbo wa kuilaani Israeli?
Walifanikiwa kum-fool Nyerere kipindi kile hadi akawa upande wa magaidi; kipindi kile tv pekee nchini ilikuwa pale Ikulu peke yake! Not nowadays!
 
Rai hiyo imetolewa leo Jijini Dar es Salaam na Balozi wa Palestina nchini Tanzania, Hamdi Mansour Abuali,wakati akizungumza na waandishi wa habari akizungumzia juu ya machafuko yanaendelea kati ya Israel na Palestina...
Nadhani tuanze kumlaani mchokizi kwanza ambaye ni HAMAS. Maana sawa na kwenda msituni ukamshika Simba sharubu au kumpiga Simba na kafimbo alafu useme Simba mbaya tumlaani. Hebu kilammoja atulie aendelee na majukumu yake ebo!
 
Atusaidie kuwaambia Hamas wawarejeshe watanzania wenzetu wawili ambao hawajulikani walipo kutokana na uvamizi wao wa Jumamosi iliyopita.
F8I5gp0WUAAlxBc.jpeg
 
Rai hiyo imetolewa leo Jijini Dar es Salaam na Balozi wa Palestina nchini Tanzania, Hamdi Mansour Abuali,wakati akizungumza na waandishi wa habari akizungumzia juu ya machafuko yanaendelea kati ya Israel na Palestina...
I stand with Palestines... Mungu aendelee kuwasimamia na adui Israel aache kukalia ardhi yao
 
Back
Top Bottom