cyrustheemperor
JF-Expert Member
- Mar 13, 2015
- 297
- 358
And am proud to be in America where at least I know I'm free
Acha kubwabwaja ww! Si ungetuuliza tuliopo hospitaini tukitibu wagonjwa!? Hata sisi hatujui huu ugonjwa ulikotokomea...maana hakuna kabisa Cha korona wa mjukuu wake corona! Kula anayekuja na vijidalili tulivyotishwa navyo hapo awali akipimwa anakutwa na magojwa ya Kila siku na wanatibiwa specifically na kupona within no time! Nimemsikia Magu amiwa kibiti nafikiri akisema ni maombi tu na Mungu ameitoa corona! Mie nimeanza kuyaamini hayo! Kenya wameikuza na kuikumbatia corona na kuiona na nguvu kuliko Mungu...na Mungu kawaacha iwashughulikie! Hao wake ya naanza kuamini hata wakikatiza na corona, wakiingia Tz tu watapona papi hapo! Niiteni vyovyote vile Ila pamoja na taaluma yangu ya udaktari sioni sababu nyingine inayowafanya Kenya et Al wapate full force ya corona wakati huo huku kwetu ni full kukuachia na tunadunda salama!Mwandishi umeunganisha mengi sana yasiyohusiana na hili la sasa linaloendelea kati ya Kenya na Tanzania. Ameshindwa kujenga hoja mahususi.
Kilichopo ni hichi, Kenya ilizuia Safari za ndege na wasafiri kutoka Tanzania kutua moja kwa moja Kenya kwa sasa kwa lengo la kujilinda dhidi ya Corona (na mantiki ya hili iko wazi kabisa kwa wakenya kuwa, Tanzania tumekataa uwepo wa Corona wakati wakenya wanajua/kuamini kuwa Corona bado inalindima Tz) na hilo zuio haliihusu Tz pekee bali nchi nyingi zaidi ya 100.
Sasa pasipo kutegemewa na pasipo kutolewa sababu ya msingi, Tanzania ikazuia ndege za Kenya airways kutua Tanzania! Mimi naona hapa Tz tunafanya utoto tu.
CoolNARUDIA TENA :- WATANZANIA WAKENYA WASIWASUMBUE.
Na Thadei Ole Mushi.
Wiki hii toka jumatatu joto la kidiplomasia Kati yetu na Kenya limepanda Kiasi. Joto hili linasababishwa na vurugu za ugonjwa wa Corona. Nimejaribu kwa kiasi kuwaonyesha watanzania sababu za kuendelea kukataa mchezo wa Kenya katika Uchumi wetu. Naelewa Sana umuhimu wa diplomasia yetu na Kenya lakini linapokuja issue ambayo inalihusu Taifa langu lazima tupigane kwa pamoja.
Leo nitawapa kwa kifupi Sana kwa nini Kenya ukiangalia mwelekeo wa nchi yetu kiuchumi wanachanganyikiwa. Nitaongelea Mambo mawili kwa kifupi Sana.
1. Mradi wa SGR.
Kuna watakaojiuliza Reli ya SGR inawahusu nini wakenya? Ni swali zuri Sana na kila anayejiuliza ni haki yake ajiulize.
Kama Kuna kitu kinawasumbua Kenya ni Mradi huu wa SGR. Tukumbuke kuwa issue hapa sio mataruma ya Reli Bali issue kubwa hapa ni bandari zetu Mombasa na Daresalam
Ipo hivi
Kenya ndio wa kwanza kabisa kujenga mradi wa SGR wakishirikiana na Ethiopia kwa kukopa China. Mkopo huo waliokopa China uliziingiza nchi hizi mbili Kenya na Ethiopia kushika number mbili na number tatu kwa nchi zilizokopa Sana China Kutoka Africa. Yaani tukipanga wanaodaiwa fedha nyingi na China Africa basi kenya na Ethiopia zinashika number mbili na number tatu. Ni Mkopo ambao ni mkubwa Sana na kuulipa si kazi ndogo.
Jarida la African Report liliwahi kunukuu mtafiti mmoja aliyeandika kwenye Gazeti la Kenya (Daily Nation) kuwa:-.
"Kenya’s and Ethiopia’s SGR projects impacted significantly the amount of their debt to China and generally their ratio of debt relative to GDP,” researchers wrote in the Daily Nation in December 2019, “As of 2017, Ethiopia and Kenya ranked the second and third highest Chinese debtors on the continent respectively. Their debt relative to GDP has also risen exponentially compared to Tanzania’s.”
Further complicating matters is the fact that, despite accumulating debt and government focus over the past decade, Kenya and Ethiopia’s SGR’s have not delivered what they promised.
Pamoja na kwamba Wana Mkopo mkubwa Sana lakini hawatarajii kuvuna matunda yoyote yale kwenye mradi huo. Hawatarajii kuvuna Kama walivyopanga hapo awali. Yaani mipango yao imevurugika....
Sababu za kutokupata faida
Kutokana na mradi huo kutumia fedha nyingi Sana za Mkopo na ugumu wa kulipa Mkopo wenyewe Bandari ya Mombasa imekuwa si rafiki Tena kupitisha bidhaa kwa nchi za Africa mashariki kutokana na masharti na Kodi walizoweka ili wapate fedha za kulipa Mkopo.
Kutokana na hilo bandari Daresalam Tanzania imeendelea kuwa kivutio kwa nchi za Africa mashariki na Kati. Balaa kubwa zaidi kwa Kenya limekuja kujitokeza kwa Tanzania ilipoanza kujenga SGR yake.
Baada ya Mradi kuanza mataifa ya Burundi, Rwanda, na Congo waliingia mkataba wa Reli hii kufika kwenye nchi zao. Kwa maana hiyo Nchi hizi zitakuwa na access ya Moja kwa Moja kwa njia ya Reli na bandari ya Daresalam. Jiulize bandari ya Mombasa Kenya itabaki inahudumia nchi nchi gani? Bandari yao itamlisha Nani? Kwa hiyo SGR yetu imekuja kuwa ni maziko ya bandari ya Mombasa.
Kwa Sasa wanajaribu kutumia Hili la Corona angalau wapige pesa kwenye bandari yao ya Mombasa. Logic ndogo tu ya kujiuliza hakuna mabasi yanayokwenda Kenya? Kama yapo ulishawahi kuona abiria au madereva wa mabasi wakilia Kama wa malori? Unajua ni kwa nn wanakomaa na madereva wa malori? Huhitaji Elimu ya chuo kikuu hapa.
Justification
Baada ya Tanzania kutiliana saini na nchi za Burundi, Rwanda, na Congo kuhusu ujenzi wa SGR Gazeti la nchini Kenya linalojulikana Kama the East Africa liliandika kuwa Kenya imepata pigo kubwa kutokana na makubaliano hayo ya Tanzania na Rwanda, Burundi, na Congo. Fuata Link kusoma walichokiandika.
Blow to Northern Corridor as Tanzania signs deal to link SGR to Burundi, DRC - The East African - Blow to Northern Corridor as Tanzania signs deal to link SGR to Burundi, DRC
Hili Ni Gazeti la Kenya sio la Tanzania katika Hali Kama hii hawawezi kutufurahia sisi kupaa kiuchumi.
Habari hii ilichapishwa pia na jarida la The China Project in Africa. Unaweza pia kusoma kupitia link ifuatayo kujionea kinachoendelea.
Kenya’s Embattled SGR Suffers Major Setback as Burundi, DRC Opt for Tanzania Route to Port of Dar es Salaam
2. Mradi wa Stiglers Gorge.
Huu ni Mradi wa umeme ambao kufikia 2022 tunatarajia uwe umekamilia kabisa.
Mradi huu utatupatia megawatt 2,100 sawa na bwawa la Aswan la Misri ambalo nalo linatoa megawatt hizo 2,100.
Stiglers itakuwa bwawa Namba Moja Afrika yeye na Aswan kwa pamoja kwa kutoa megawatt nyingi na zinazolingana. Mabwawa Mengine yote yaliyobakia Afrika hayawezi kufikia kiwango hicho Cha Stiglers.
Mradi huu Rais Magufuli alipoanza kuugusia kuwa ataujenga utoke kwenye ndoto za Mwalimu Nyerere na kuwa kweli hakuna Taifa ambalo halikupinga.
Mataifa ya Ulaya na kwingineko wote waliionya Tanzania wasijaribu. Sababu kubwa wataharibu mazingira....
Mwandishi Kutoka Kenya anayeishi Lusaka Zambia anayeitwa Mike Mwenda aliandika kwenye jarida la Lifegate Mambo ya ajabu kabisa na hata kumtuhumu Rais wetu. Kisa ni sisi kutaka kutengeneza Mradi wa Stiglers. Fuata link ifuatayo kumsoma Mike Mwenda na shutuma zake.
Tanzania to build Stiegler's Gorge dam in a wildlife reserve and Unesco site - LifeGate
Linapokuja suala la kiuchumi kwa Dunia ya Sasa ni Vita. Na Kama hutoruhusu akili yako kufanya kazi Basi utajikuta ukiitikia chorus za nyimbo za mabeberu.
Stiglers itatuondoa kabisa kwenye uhaba wa umeme na kutufikisha kwenye Uchumi wa viwanda. Kila Tanzania inapojenga Kiwanda Moja kwa Moja unagusa Uchumi wa Kenya ambao hutegemea Sana soko hapa Tanzania kutokana na sisi kuwa hatuna viwanda. Hii ni Vita.....hata Panadol hatununui Tena Kenya.
Tujiulize Kama Stiglers inaharibu mazingira je viwanda vya mabeberu haviaharibu mazingira?.....
Mwaka 1992 Marekani ulikataa kusaini mkataba wa Kyoto Protocol ambao ulihusu kupunguza viwanda ambavyo vinachangia mabadiliko ya Hali ya hewa.
Unaambiwa mataifa haya ya Magharibi pekee huchangia joto Duniani kwa asilimia 45 ya joto lote. Utafiti uliwahi kufanyika na kuonyesha kuwa Kama mataifa haya ya kibepari yatakubali kupunguza Viwanda vyao Basi Dunia inaweza ku maintain joto la centigrade 18°C.
Sisi kujenga Stiglers tu imekuwa kelele kubwa.
Tupunguze kulalamika tuijenge nchi Yetu. Hata Sasa wagonjwa wetu wengi hatupeleki Kenya badala yake wanapelekwa Mloganzila na Muhimbili kwa zile case za kupelekewa Nairobi Kenya.
Vijana wa Kitanzania tufahamu kuwa kwa Sasa tuna jeuri ya kutosha kabisa. Tembeeni kifua mbele, Hawa wachache walioamua kusimika kichwa kwenye mchanga Kama jogoo tuanchane nao. Najua ukiyasema haya watakuambia unatafuta Uteuzi as if kuteuliwa ni jambo baya au yeye hataki kuteuliwa au akiteuliwa atakataa..... Akili za kijinga kabisa hizi.
Unakifikiri wanafurahia.......... Ni baadhi ya watu tu hawaelewi kinachoendelea au kufuatilia Mambo hawawezi. Ndio maana tunawashauri Kama wanaona Kenya ni Bora zaidi wahamie Kenya.... Hakuna aliyenyiwa kufanya hivyo.
Ole Mushi
0712702602
Mtoa mada analeta propaganda tu. Ukweli ni kuwa wanachofanya Kenya ni sahihi kuzuia maambukizi kimataifa. Tunalaumu kutoruhusiwa kuingia Kenya lakini hatujiulizi kama tungeruhusiwa kuingia tungekuwa na uwezo wa kutekeleza masharti yaliyowekwa kwa hizo nchi 11 za kwanza!!
Je tunaweza kupima corona na kutoa certificate???? Kama hatuna uwezo huu, hata wangesema tuingie - tusingesafiri!!
Tanzania iko katika list nyinge ya UAE kuwa tupime ndani ya masaa 96 ya kusafiri na kupata cheti cha negative na tukifika Dubai tupimwe tena kuthibitisha. Je huko nako tunalaumu kuwa si sawa???
Namna tulivopambana na corona hapa nyumbani si sawa na walivofanya huko ughaibuni. Itatupasa kutimiza matakwa yao kwenda kwao.
Badala ya kupoteza nguvu nyingi kulalama, ni bora tukajijengea uwezo wa kupima na kuwathibitishia sisi sio tishio kwa maambukizi katika nchi zao! Na katika ukweli nasi pia hatutakiwi kukubali maambukizi kutoka nchi nyingine!! Nasi tuwatake wanaokuja kuthibitisha wako salama, kinyume chake ni uzembe!!
Kwani kati ya yuan na paund ipi inathamani?1 TSH ==2800 GB Pound
1KESH ==140 GB Pound
Wewe mwenyewe mgonjwa wa hiyo corona? au hapo kwa shemeji yako kuna mgonjwa aliyepatikana au ngazi ya familia na ukoo wenu mna wagonjwa na wameshakufa wangapi? na unavyoshauri tupime uliambiwa hapa kwetu hatupimwi?,je ilijaribu kubebwa na shemeji yako kwenda kupimwa corona ukaambiwa vipimo hakuna,na baada ya kupimwa kuna dawa iliyopatikana.Mtoa mada analeta propaganda tu. Ukweli ni kuwa wanachofanya Kenya ni sahihi kuzuia maambukizi kimataifa. Tunalaumu kutoruhusiwa kuingia Kenya lakini hatujiulizi kama tungeruhusiwa kuingia tungekuwa na uwezo wa kutekeleza masharti yaliyowekwa kwa hizo nchi 11 za kwanza!!
Je tunaweza kupima corona na kutoa certificate???? Kama hatuna uwezo huu, hata wangesema tuingie - tusingesafiri!!
Tanzania iko katika list nyinge ya UAE kuwa tupime ndani ya masaa 96 ya kusafiri na kupata cheti cha negative na tukifika Dubai tupimwe tena kuthibitisha. Je huko nako tunalaumu kuwa si sawa???
Namna tulivopambana na corona hapa nyumbani si sawa na walivofanya huko ughaibuni. Itatupasa kutimiza matakwa yao kwenda kwao.
Badala ya kupoteza nguvu nyingi kulalama, ni bora tukajijengea uwezo wa kupima na kuwathibitishia sisi sio tishio kwa maambukizi katika nchi zao! Na katika ukweli nasi pia hatutakiwi kukubali maambukizi kutoka nchi nyingine!! Nasi tuwatake wanaokuja kuthibitisha wako salama, kinyume chake ni uzembe!!
Mkuu sijaamini kama huyu ni wewe!Asante Mushi ni kweli zile enzi za kuwaogopa na kuwahusudu wakenya zimepita. Tena watanzania mjue kuwa mambo yetu ni mazuri zaidi kuliko ya wakenya. Tuna mengi zaidi ya kujivunia Tanzania kuliko walivyo wakenya, tuache unyonge, tujiamini na tuchape kazi.