Fumadilu Kalimanzila
JF-Expert Member
- Dec 10, 2016
- 1,651
- 5,126
Ukifuatilia mazungumzo, mijadala, mawazo na taarifa mbalimbali kutoka kwa viongozi wa kisiasa, wafanyakazi, wakulima, wanahabari, wanafunzi, na kwa usahihi zaidi tuseme wananchi wa kawaida kwa ujumla wetu, utagundua kitu kimoja kikubwa, wengi hatuna MAARIFA ya kutosha!
Ugonjwa huu wa kukosa MAARIFA ni kutokana na sisi Watanzania kutopenda kabisa KUJISOMEA!
Watanzania "WANAOWAJIBIKA KUJISOMEA) " wamebaki kuwa ni wale tu wanaokabiliwa na mitihani mbalimbali kutoka katika Mabaraza ya mitihani!
Hali hii imepelekea Nchi yetu kuwa na watu wa ajabu ajabu na hasa viongozi wa kisiasa ambao hata wanapozungumza kuhusu jambo fulani iwe ni kuhusu uchumi, siasa au utamaduni, huwezi kujua wanaongozwa au kusimamia kanuni zipi!
Hii imepelekea Nchi hii kufeli kwenye mambo ya msingi mengi tukiwa bado ni Taifa changa lenye watu takribani milioni 60, ebu fikiria kwa akili hizi tulizonazo Watanzania tukifika watu milioni 100! Hali itakuwaje?
Tumekuwa "Taifa la Kijinga" la kufuata mtu mmoja anawaza nini au ameona nini, au kikundi fulani kinawaza nini au kimeona nini na risk ya kupotea ni apparent.
Kama unaweza kupinga hii hoja yangu basi ebu nieleze kama Taifa la watu milioni 60 iweje kila mwaka tujenge madarasa kwa ajili ya watoto wetu baada ya matokeo ya mitihani kutangazwa?
Nieleze ni kwanini kama Taifa hatujitoshelezi kwa sukari,mafuta ya kula, sementi n.k lakini tumeshindwa kabisa kutumia fursa hizo kutatua tatizo la ajira kwa vijana wetu wanazagaa ovyo mitaani!
Tumekuwa watu wa ovyo wenye mawazo finyu na ya kimasikini sana! Kama Taifa hatuna ndoto kubwa (big dreams) kwa watu wetu na tunaona hata wale wachache wenye mafanikio kutokana na ndoto zao kubwa (big dreams) na jitihada zao binafsi kama maadui, wezi na watu wanaostahili kudhibitiwa kwa hali zote.
Watanzania na hasa viongozi wa kisiasa mliopewa dhamana ya kuongoza mnatakiwa kubadilika, kusimama na kutambua kuwa Tanzania kama Taifa ni kubwa na ni muhimu kuliko mtu yeyote mojamoja.
Mnapaswa kutafuta MAARIFA hasa kwa KUJISOMEA taarifa,tafiti na machapisho mbalimbali ili kujua mwelekeo sahihi wa Dunia tuliyonayo na kuacha kabisa kushupaza shingo kuwa MNAJUA KILA KITU!
Watanzania pia tunapaswa kubadilika sana na kutafuta MAARIFA kwa njia mbalimbali na hasa kwa KUJISOMEA na kuacha kutoa muda mwingi kwa mambo ya mizaha, ucheshi na vituko vingine vingi.
Kwa msingi huo tunaweza kujenga hali inayoweza kutusaidi kujenga Taifa imara lenye watu wanaojitambua kwa manufaa ya kizazi chetu na kizazi kijacho.
Ugonjwa huu wa kukosa MAARIFA ni kutokana na sisi Watanzania kutopenda kabisa KUJISOMEA!
Watanzania "WANAOWAJIBIKA KUJISOMEA) " wamebaki kuwa ni wale tu wanaokabiliwa na mitihani mbalimbali kutoka katika Mabaraza ya mitihani!
Hali hii imepelekea Nchi yetu kuwa na watu wa ajabu ajabu na hasa viongozi wa kisiasa ambao hata wanapozungumza kuhusu jambo fulani iwe ni kuhusu uchumi, siasa au utamaduni, huwezi kujua wanaongozwa au kusimamia kanuni zipi!
Hii imepelekea Nchi hii kufeli kwenye mambo ya msingi mengi tukiwa bado ni Taifa changa lenye watu takribani milioni 60, ebu fikiria kwa akili hizi tulizonazo Watanzania tukifika watu milioni 100! Hali itakuwaje?
Tumekuwa "Taifa la Kijinga" la kufuata mtu mmoja anawaza nini au ameona nini, au kikundi fulani kinawaza nini au kimeona nini na risk ya kupotea ni apparent.
Kama unaweza kupinga hii hoja yangu basi ebu nieleze kama Taifa la watu milioni 60 iweje kila mwaka tujenge madarasa kwa ajili ya watoto wetu baada ya matokeo ya mitihani kutangazwa?
Nieleze ni kwanini kama Taifa hatujitoshelezi kwa sukari,mafuta ya kula, sementi n.k lakini tumeshindwa kabisa kutumia fursa hizo kutatua tatizo la ajira kwa vijana wetu wanazagaa ovyo mitaani!
Tumekuwa watu wa ovyo wenye mawazo finyu na ya kimasikini sana! Kama Taifa hatuna ndoto kubwa (big dreams) kwa watu wetu na tunaona hata wale wachache wenye mafanikio kutokana na ndoto zao kubwa (big dreams) na jitihada zao binafsi kama maadui, wezi na watu wanaostahili kudhibitiwa kwa hali zote.
Watanzania na hasa viongozi wa kisiasa mliopewa dhamana ya kuongoza mnatakiwa kubadilika, kusimama na kutambua kuwa Tanzania kama Taifa ni kubwa na ni muhimu kuliko mtu yeyote mojamoja.
Mnapaswa kutafuta MAARIFA hasa kwa KUJISOMEA taarifa,tafiti na machapisho mbalimbali ili kujua mwelekeo sahihi wa Dunia tuliyonayo na kuacha kabisa kushupaza shingo kuwa MNAJUA KILA KITU!
Watanzania pia tunapaswa kubadilika sana na kutafuta MAARIFA kwa njia mbalimbali na hasa kwa KUJISOMEA na kuacha kutoa muda mwingi kwa mambo ya mizaha, ucheshi na vituko vingine vingi.
Kwa msingi huo tunaweza kujenga hali inayoweza kutusaidi kujenga Taifa imara lenye watu wanaojitambua kwa manufaa ya kizazi chetu na kizazi kijacho.