Watanzania na utetezi wa maovu

APA CHICAGO

JF-Expert Member
Oct 20, 2019
259
293
Kwa mara kadhaa katika jukwaa hili la watu tunaojiita "Great thinker" zimeletwa post hapa za kuonyesha maovu fulani kwenye jamii yetu ama yamefanya na kiongozi fulani majibu yetu yamekuwa ya ajabu kwa mfano Acha wivu wa kike wewe, mara acha Majungu au peleka TAKUKURU hiyo habari.

Huwa ninajiuliza hivi kweli? hatujui nguvu ya vyombo vya habari? Kama mitandao ya kijamii? Au hatujui umuhimu wa kupashana habari kwa njia mbalimbali kama vile facebook na twitter? Kama ni hivyo basi kwenye jukwaa hili tupo kwa bahati mbaya tu na kama tunajua umuhimu wa kupashana habari basi tupo hapa kusifia kitu chochote kile ili mradi kiko upande unao usapoti na kupinga kitu chochote ambacho kiko upande ambao wewe hausapoti,kama hili ni kweli basi naweza kusema hatupo hapa kwa masirahi ya Taifa,

Letu hivyo tusubiri kizazi kingine huenda chenyewe kitakuja na kitakuwa kwa masilahi ya taifa letu.

Nimesema haya kwa kuzingatia post kadhaa zimeletwa hapa kwa masilahi ya jamii yetu na taifa letu kwa ujumla lakini watu walianza kukoment bila kutaka kujua kwa undani zaidi. Kwa mfano kuna post moja ililetwa hapa jukwaani ikigusia mwenyekiti wa Halmashauri ya Geita mjini mhe. Bugomora kugawa fedha za wananchi kwa karibu zaidi ya asilimia hamsini kwa kikundi kimoja tu cha vijana.

Badala ya ma great thinker wa JamiiForums kuhoji na kutaka kujua fedha hizo katika halmashauri zetu zipo kwa ajili ya vikundi vya aina gani?. Mfano, akina mama na walemavu n.k. Watu walijikita katika kumshambulia mtoa post.

Mimi wakati mwingine nawaza huenda Watanzania tumeshazoea shida na imekuwa sehemu ya maisha yetu ya kawaida vikiwemo vitendo vya rushwa?.

Nitoe wito kwa wana Jamiiforums wenzangu tujitahidi kuisaidia jamii yetu kwa kusema ukweli kama mtu ameonewa ajitetee mwenyewe.
 
APA CHICAGO
Hao wanaotetea maovu ya aina yoyote nchini, wanafahamika hapa JF kwa jina maarufu la Lumumba buku 7 club...............

Hao jamaa wanachojua ni kutetea kwa nguvu zote utawala huu wa awamu ya tano, hata pale ambapo mtoto mdogo anayesoma chekechea anaona wazi kuwa serikali yetu hii inafanya mambo maovu ya waziwazi kabisa!
 
Kwa mara kadhaa katika jukwaa hili la watu tunaojiita "Great thinker" zimeletwa post hapa za kuonyesha maovu fulani kwenye jamii yetu ama yamefanya na kiongozi fulani majibu yetu yamekuwa ya ajabu kwa mfano Acha wivu wa kike wewe, mara acha Majungu ,Au peleka takukuru hiyo habari.

Huwa ninajiuliza hivi kweli? hatujui nguvu ya vyombo vya habari? Kama mitandao ya kijamii?.Au hatujui umuhimu wa kupashana habari kwa njia mbalimbali kama vile facebook na twitter? Kama ni hivyo basi kwenye jukwaa hili tupo kwa bahati mbaya tu na kama tunajua umuhimu wa kupashana habari basi tupo hapa kusifia kitu chochote kile ili mradi kiko upande unao usapoti na kupinga kitu chochote ambacho kiko upande ambao wewe hausapoti,kama hili ni kweli basi naweza kusema hatupo hapa kwa masirahi ya Taifa,
letu hivyo tusubiri kizazi kingine huenda chenyewe kitakuja na kitakuwa kwa masirahi ya taifa letu.

Nimesema haya kwa kuzingatia post kadhaa zimeletwa hapa kwa masirahi ya jamii yetu na taifa letu kwa ujumla lakini watu walianza kukoment bila kutaka kujua kwa undani zaidi.Kwa mfano kuna post moja ililetwa hapa jukwaani ikigusia mwenyekiti wa Halmashauri ya Geita mjini mhe.Bugomora kugawa fedha za wananchi kwa karibu zaidi ya asilimia hamsini kwa kikundi kimoja tu cha vijana.

Badala ya ma great thinker wa jamii forum kuhoji na kutaka kujua fedha hizo katika halmashauri zetu zipo kwa ajili ya vikundi vya aina gani?.Mfano, akina mama na walemavu n.k.Watu walijikita katika kumshambulia mtoa post.

Mimi wakati mwingine nawaza huenda Watanzania tumeshazoea shida na imekuwa sehemu ya maisha yetu ya kawaida vikiwemo vitendo vya rushwa?.
Nitoe wito kwa wana jamii forum wenzangu tujitahidi kuisaidia jamii yetu kwa kusema ukweli kama mtu ameonewa ajitetee mwenyewe.
Kama mtoa mada alikuwa na ushahidi na uhakika kuwa pesa zilizogawiwa ni za umma. Sasa kwa nini asiende Pccb. Japokuwa kuleta hiyo habari ni jambo jema pia. Ili hatua stahiki zichukuliwe kwa nini hakwenda Pccb kwa hatua za kisheria zichukuliwe.
 
APA CHICAGO
Hao wanaotetea maovu ya aina yoyote nchini, wanafahamika hapa JF kwa jina maarufu la Lumumba buku 7 club...............

Hao jamaa wanachojua ni kutetea kwa nguvu zote utawala huu wa awamu ya tano, hata pale ambapo mtoto mdogo anayesoma chekechea anaona wazi kuwa serikali yetu hii inafanya mambo maovu ya waziwazi kabisa!
Mkuu ningependa kuona kuleo linaitwa kolea na jembe linaitwa jembe.Sio kolea wakati fulani linaitwa jembe ama shoka.
 
Kwa mara kadhaa katika jukwaa hili la watu tunaojiita "Great thinker" zimeletwa post hapa za kuonyesha maovu fulani kwenye jamii yetu ama yamefanya na kiongozi fulani majibu yetu yamekuwa ya ajabu kwa mfano Acha wivu wa kike wewe, mara acha Majungu au peleka TAKUKURU hiyo habari.

Huwa ninajiuliza hivi kweli? hatujui nguvu ya vyombo vya habari? Kama mitandao ya kijamii? Au hatujui umuhimu wa kupashana habari kwa njia mbalimbali kama vile facebook na twitter? Kama ni hivyo basi kwenye jukwaa hili tupo kwa bahati mbaya tu na kama tunajua umuhimu wa kupashana habari basi tupo hapa kusifia kitu chochote kile ili mradi kiko upande unao usapoti na kupinga kitu chochote ambacho kiko upande ambao wewe hausapoti,kama hili ni kweli basi naweza kusema hatupo hapa kwa masirahi ya Taifa,

Letu hivyo tusubiri kizazi kingine huenda chenyewe kitakuja na kitakuwa kwa masilahi ya taifa letu.

Nimesema haya kwa kuzingatia post kadhaa zimeletwa hapa kwa masilahi ya jamii yetu na taifa letu kwa ujumla lakini watu walianza kukoment bila kutaka kujua kwa undani zaidi. Kwa mfano kuna post moja ililetwa hapa jukwaani ikigusia mwenyekiti wa Halmashauri ya Geita mjini mhe. Bugomora kugawa fedha za wananchi kwa karibu zaidi ya asilimia hamsini kwa kikundi kimoja tu cha vijana.

Badala ya ma great thinker wa JamiiForums kuhoji na kutaka kujua fedha hizo katika halmashauri zetu zipo kwa ajili ya vikundi vya aina gani?. Mfano, akina mama na walemavu n.k. Watu walijikita katika kumshambulia mtoa post.

Mimi wakati mwingine nawaza huenda Watanzania tumeshazoea shida na imekuwa sehemu ya maisha yetu ya kawaida vikiwemo vitendo vya rushwa?.

Nitoe wito kwa wana Jamiiforums wenzangu tujitahidi kuisaidia jamii yetu kwa kusema ukweli kama mtu ameonewa ajitetee mwenyewe.
Tunapambana na corona! Tukiimaliza tutakujibu!
 
Kuna Wapuuzi kadhaa hapa ambao hata kama mnajadili jambo lenye maslahi kwa nchi wao hawaachi kuleta siasa za kipuuzi. Ni wapuuzi saana
 
Kama mtoa mada alikuwa na ushahidi na uhakika kuwa pesa zilizogawiwa ni za umma. Sasa kwa nini asiende Pccb. Japokuwa kuleta hiyo habari ni jambo jema pia. Ili hatua stahiki zichukuliwe kwa nini hakwenda Pccb kwa hatua za kisheria zichukuliwe.
Mkuu chagu wa Malunde kifupi iko hivi "Sheria ya Fedha ya mwaka 2008 namba 4 inazitaka halmashauri zote nchini kutenga asilimia 10 ya mapato ya ndani kwa ajili ya vijana, walemavu na wanawake.kama ifuatavyo 40:20:40.Anacholalamikiwa mheshimiwa Bugomora ni kugawa fedha za kikundi za vijana wa halmashauri ya Geita mjini kwa kikundi kimoja tu kwa zaidi ya nusu yake na kuwa watu waliopewa fedha hizo walipewa kwa upendeleo ili hali halmashauri ina vikundi vingi vya vijana.
Way forward,mimi nimeamua kuleta post hii ili kuikumbusha jamii yetu hasa jamii forum ambayo ni ya ma Great thinker tusiingie kwenye mkumbo wa kuzoea shida zetu ikiwemo rushwa na ufisadi na ikiwezekana tujibu hoja kwa weledi na facts ground then direction.
 
Kuna Wapuuzi kadhaa hapa ambao hata kama mnajadili jambo lenye maslahi kwa nchi wao hawaachi kuleta siasa za kipuuzi. Ni wapuuzi saana
Mkuu Elisha Mshana nashukuru kwa mawazo yako tusikifanye kila kitu siasa kuna mambo mengine yanahitaji facts tu na uwajibikaji.
 
Mkuu hiyo ipo sehemu yeyote huwezi ukakubalika na wote,Pia huwezi ukapingwa na wote..lazima watatokea watu ambao mitazamo itaenda tofauti..achana nao we fikisha ujumbe endelea na yako..
 
Mkuu chagu wa Malunde kifupi iko hivi "Sheria ya Fedha ya mwaka 2008 namba 4 inazitaka halmashauri zote nchini kutenga asilimia 10 ya mapato ya ndani kwa ajili ya vijana, walemavu na wanawake.kama ifuatavyo 40:20:40.Anacholalamikiwa mheshimiwa Bugomora ni kugawa fedha za kikundi za vijana wa halmashauri ya Geita mjini kwa kikundi kimoja tu kwa zaidi ya nusu yake na kuwa watu waliopewa fedha hizo walipewa kwa upendeleo ili hali halmashauri ina vikundi vingi vya vijana.
Way forward,mimi nimeamua kuleta post hii ili kuikumbusha jamii yetu hasa jamii forum ambayo ni ya ma Great thinker tusiingie kwenye mkumbo wa kuzoea shida zetu ikiwemo rushwa na ufisadi na ikiwezekana tujibu hoja kwa weledi na facts ground then direction.
Ok fine. Kama mwenyekiti wa halmashauri na ametumia madaraka na ofisi vibaya ulipaswa kwenda ofisi za Pccb ili kuripoti. Na hatua stahiki zichukuliwe.
 
Kama mtoa mada alikuwa na ushahidi na uhakika kuwa pesa zilizogawiwa ni za umma. Sasa kwa nini asiende Pccb. Japokuwa kuleta hiyo habari ni jambo jema pia. Ili hatua stahiki zichukuliwe kwa nini hakwenda Pccb kwa hatua za kisheria zichukuliwe.

..Joshua Nassari alipeleka ushahidi wa rushwa pccb haukufanyiwa kazi.

..ukishitaki wana-ccm kwa pccb malalamiko yako hayatafanyiwa kazi.
 
Ndio ujue aina ya Watu waliojazana huku JF.

Mtu anakuja na uzi wa kufichua eneo unapofanyika wizi wa aina fulani, tuseme kwa mfano mafuta ya Magari kutoka kwenye Lori, cha ajabu asilimia 70 ya wachangiaji wanamsakama Mleta huo uzi.
 
Ndio ujue aina ya Watu waliojazana huku JF.

Mtu anakuja na uzi wa kufichua eneo unapofanyika wizi wa aina fulani, tuseme kwa mfano mafuta ya Magari kutoka kwenye Lori, cha ajabu asilimia 70 ya wachangiaji wanamsakama Mleta huo uzi.
Mkuu umenena yaliyo ya kweli kwa 100%.Bahati mbaya kabisa watu wanaofanya vitendo viovu ktk jamii yetu huwa wanakuwa wana watu walio waandaa ili waje kuwatetea.
 
Kwa mara kadhaa katika jukwaa hili la watu tunaojiita "Great thinker" zimeletwa post hapa za kuonyesha maovu fulani kwenye jamii yetu ama yamefanya na kiongozi fulani majibu yetu yamekuwa ya ajabu kwa mfano Acha wivu wa kike wewe, mara acha Majungu au peleka TAKUKURU hiyo habari.

Huwa ninajiuliza hivi kweli? hatujui nguvu ya vyombo vya habari? Kama mitandao ya kijamii? Au hatujui umuhimu wa kupashana habari kwa njia mbalimbali kama vile facebook na twitter? Kama ni hivyo basi kwenye jukwaa hili tupo kwa bahati mbaya tu na kama tunajua umuhimu wa kupashana habari basi tupo hapa kusifia kitu chochote kile ili mradi kiko upande unao usapoti na kupinga kitu chochote ambacho kiko upande ambao wewe hausapoti,kama hili ni kweli basi naweza kusema hatupo hapa kwa masirahi ya Taifa,

Letu hivyo tusubiri kizazi kingine huenda chenyewe kitakuja na kitakuwa kwa masilahi ya taifa letu.

Nimesema haya kwa kuzingatia post kadhaa zimeletwa hapa kwa masilahi ya jamii yetu na taifa letu kwa ujumla lakini watu walianza kukoment bila kutaka kujua kwa undani zaidi. Kwa mfano kuna post moja ililetwa hapa jukwaani ikigusia mwenyekiti wa Halmashauri ya Geita mjini mhe. Bugomora kugawa fedha za wananchi kwa karibu zaidi ya asilimia hamsini kwa kikundi kimoja tu cha vijana.

Badala ya ma great thinker wa JamiiForums kuhoji na kutaka kujua fedha hizo katika halmashauri zetu zipo kwa ajili ya vikundi vya aina gani?. Mfano, akina mama na walemavu n.k. Watu walijikita katika kumshambulia mtoa post.

Mimi wakati mwingine nawaza huenda Watanzania tumeshazoea shida na imekuwa sehemu ya maisha yetu ya kawaida vikiwemo vitendo vya rushwa?.

Nitoe wito kwa wana Jamiiforums wenzangu tujitahidi kuisaidia jamii yetu kwa kusema ukweli kama mtu ameonewa ajitetee mwenyewe.
Mkuu hao jamaa wanakuwa kazini,wanalipwa ili wafanye kazi ya kuwatetea watafuna nchi
 
..Joshua Nassari alipeleka ushahidi wa rushwa pccb haukufanyiwa kazi.

..ukishitaki wana-ccm kwa pccb malalamiko yako hayatafanyiwa kazi.
Awamu hii iwe mwana CCM au nani anapitiwa tu na Pccb
 

Attachments

  • IMG_20200421_0001.jpeg
    IMG_20200421_0001.jpeg
    116.4 KB · Views: 1
Mimi nadhani JF ina jukumu la kulinda jukwaa hili maana kuna watu bila kificho wako humu kwa kazi maalumu. Kuhamisha mijadala (derail) kwa kuvuruga tu nyuzi hasa kwa kuingiza siasa za kipuuzi. Bahati nzuri, wanachama hawa ni rahisi kuwabaini, na mara nyingi hutumia akaunti zinazojirudia kufanya kazi hii.
Kuwafungia Kama hawajavunja taratibu za jukwaa si sawa, ni censorship na nisingependa JF ichukue hii approach. Lakini haizuii waendeshaji humu kuja na mbinu ambayo kwa mfano itawapa wanachama Power ya kubainisha wachangiaji wa namna hii kidemokrasia. Njia moja ambayo nimefikiria ni kutangaza wanachama ambao wamepewa Tofali na wanachama wengi zaidi (Most blocked members), kwa nia ya kuwapa mrejesho au disincentive wakorofi hawa kwamba wanachofanya hakina tija. Kama nia yao ni kuvuruga, wajue kwamba post zao hazisomwi kama ambavyo wangependelea. Itawalazimu kubadili akaunti au kubadili mienendo. Nyingine ni kitufe cha dislike kwa post. Nakumbuka kulisoma hili wazo humu lakini sijui kwa nini halikuonekana na tija. Kwa njia ile ile, wanachama wenye dislike nyingi wawekwe wazi.
 
Back
Top Bottom