Watanzania na biashara ya ukahaba nchini China

Watanzania na biashara ya ukahaba nchini China

EMT

Platinum Member
Joined
Jan 13, 2010
Posts
14,477
Reaction score
15,347
Mara kwanza nilitonywa kuhusiana na kushamiri kwa biashara ya ukahaba inayofanywa na Watanzania nchini China. Sikuchukulia seriously juu ya hili suala, lakini inaonekana kweli lisemwalo limo. Lakini bado najiuliza inawezekanaje Watanzania 40 kukutwa katika hoteli moja nchini China kwa wakati mmoja huku kila mmoja akiwa na mitikasi yake Halafu kati yao, 38 ni wanawake. Kwani kuna mkutano mwingine wa wanawake Beijing huko China?

Hii imetokea huko Macau nchini China ambapo polisi wamewakamata makahaba wa Kitanzania baada ya kutonywa kuwa kulikuwa na makahaba waliokuwa wakifanya biashara za kuuza miili yao kwenye hoteli moja iliyopo mji wa Central District. Baada ya kuwakamata makahaba wanne wa Kitanzania, polisi walianzisha msako hotelini hapo ambapo walikuta wanawake wengine 38 na wanaume wawili ndani ya vyumba vitano vya hoteli hiyo. Ajabu wote walikuwa ni raia wa Tanzania wenye umri kati ya miaka 19 na 38.

Hata hivyo, wengi wa Watanzania hao walikanusha kujihusisha na ukahaba. Wengi wao walidai kuwa walikuwa wanasubiri kuingia China au kurudi nyumbani Tanzania. Hata hivyo, kulikuwa na mwanamke mmoja wa Kitanzania ambaye aliiambia polisi kuwa alilazimishwa kufanya biashara ya ukahaba nchini China. Mwamanke huyo alidai kuwa alipewa ofa ya kufanya kazi kama mchuuzi jijini Guangzhou lakini baadae alilazimishwa kuwa kahaba. Kipato chake chote cha ukahaba kilikuwa kinachukuliwa na mwanamke mwingine. Amedai kuwa alienda Macau kwa ajili ya kuongeza visa yke.

Mwanamke huyo aliendelea kuimambia polisi kuwa Aprili 3 mwaka huu aliwambia wengine hakutaka kuendelea kuwa kahaba na kuwa alitaka kurudi nyumbani lakini akakamatwa chumbani kwake na kupigwa. Baadae polisi walimkamata mwanamke anayedaiwa kuchukua kipato chake chote na kumkuta akiwa na aina mbili za nyaraka zinazoonyesha dalili za kufanya biashara ya ukahaba. Nyaraka ya tatu ilikutwa mikononi mwa mwanamke mwingine.

[video=youtube_share;ANkRsmQcxBA]http://youtu.be/ANkRsmQcxBA[/video]
 
Hata kinondoni makaburini, jolly club na buguruni wapo pia
 
Hatutaishinda dhambi kwa kujitahidi wenyewe kwa sheria na kuboresha hali ya maisha. Tunamhitaji aliyetuumba ili atusafishe ndani kule ambako mawazo na ufahamu wa kutenda unatoka. Wako watu waliokuwa na maisha magumu lakini hawakufikiri hata kuiba seuze kuuaza mwili. Hata hivyo tatizo la mtu mmoja linatuhusu sana maana linatuonyesha kuwa kuna mahali ambako hatujafanya sawa kama jamii.
 
wachina hao wako wapi nikalipize kisasi? haiwezekani wagegedwe dada zetu tu.
 
wachina hao wako wapi nikalipize kisasi? haiwe
zekani wagegedwe dada zetu tu.

tembelea kwenye mahoteli makubwa utawapata tele wanajiuza sio wachina tu kabila yoyote duniani utapata
 
Njaa tu inawasumbua, na baada ya kugundua wachina wanavibolo vya kichina (vidogo) wakaona sio tatizo!
...
Haya maisha haya!
 
Mara kwanza nilitonywa kuhusiana na kushamiri kwa biashara ya ukahaba inayofanywa na Watanzania nchini China. Sikuchukulia seriously juu ya hili suala, lakini inaonekana kweli lisemwalo limo. Lakini bado najiuliza inawezekanaje Watanzania 40 kukutwa katika hoteli moja nchini China kwa wakati mmoja huku kila mmoja akiwa na mitikasi yake Halafu kati yao, 38 ni wanawake. Kwani kuna mkutano mwingine wa wanawake Beijing huko China?

Hii imetokea huko Macau nchini China ambapo polisi wamewakamata makahaba wa Kitanzania baada ya kutonywa kuwa kulikuwa na makahaba waliokuwa wakifanya biashara za kuuza miili yao kwenye hoteli moja iliyopo mji wa Central District. Baada ya kuwakamata makahaba wanne wa Kitanzania, polisi walianzisha msako hotelini hapo ambapo walikuta wanawake wengine 38 na wanaume wawili ndani ya vyumba vitano vya hoteli hiyo. Ajabu wote walikuwa ni raia wa Tanzania wenye umri kati ya miaka 19 na 38.

Hata hivyo, wengi wa Watanzania hao walikanusha kujihusisha na ukahaba. Wengi wao walidai kuwa walikuwa wanasubiri kuingia China au kurudi nyumbani Tanzania. Hata hivyo, kulikuwa na mwanamke mmoja wa Kitanzania ambaye aliiambia polisi kuwa alilazimishwa kufanya biashara ya ukahaba nchini China. Mwamanke huyo alidai kuwa alipewa ofa ya kufanya kazi kama mchuuzi jijini Guangzhou lakini baadae alilazimishwa kuwa kahaba. Kipato chake chote cha ukahaba kilikuwa kinachukuliwa na mwanamke mwingine. Amedai kuwa alienda Macau kwa ajili ya kuongeza visa yke.

Wasichana wa kitanzania wanaojiuza waliopo China, Macau, Hong Kong na Malaysia ni wengi sana. wana-operate kwa kuzunguka zunguka hizi sehemu. Vile vile wapo wa nchi nyingine kama Uganda, Kenya, wachina wenyewe, wafilipino, wahindi, waindonesia, warusi nk.
 
Waacheni watafte hela jamani hiyo siyo biashara haramu.
 
wachina hao wako wapi nikalipize kisasi? haiwezekani wagegedwe dada zetu tu.
Nilopokuwa Goungzhou,sijawai ona wachina wakinunua dada zetu,wateja ni wagana,naijerians wtz etc,usiwasingizie bwana.
 
Nisingesitika sana kama hao mabinti wangeenda kihalali na kufanya hiyo biashara kwa kufuata taratibu zote (kama zipo). Tatizo kubwa ni kwamba wajanja wachache wanafanya biashara na kujiingizia pesa nyingi kwa kuwanyanyasa wasichana wasio na hatia.

Hao mafisadi wanatakiwa kushughulikiwa kama wahalifu wengine (tena wachafu)!
 
Mara kwanza nilitonywa kuhusiana na kushamiri kwa biashara ya ukahaba inayofanywa na Watanzania nchini China. Sikuchukulia seriously juu ya hili suala, lakini inaonekana kweli lisemwalo limo. Lakini bado najiuliza inawezekanaje Watanzania 40 kukutwa katika hoteli moja nchini China kwa wakati mmoja huku kila mmoja akiwa na mitikasi yake Halafu kati yao, 38 ni wanawake. Kwani kuna mkutano mwingine wa wanawake Beijing huko China?

Hii imetokea huko Macau nchini China ambapo polisi wamewakamata makahaba wa Kitanzania baada ya kutonywa kuwa kulikuwa na makahaba waliokuwa wakifanya biashara za kuuza miili yao kwenye hoteli moja iliyopo mji wa Central District. Baada ya kuwakamata makahaba wanne wa Kitanzania, polisi walianzisha msako hotelini hapo ambapo walikuta wanawake wengine 38 na wanaume wawili ndani ya vyumba vitano vya hoteli hiyo. Ajabu wote walikuwa ni raia wa Tanzania wenye umri kati ya miaka 19 na 38.

Hata hivyo, wengi wa Watanzania hao walikanusha kujihusisha na ukahaba. Wengi wao walidai kuwa walikuwa wanasubiri kuingia China au kurudi nyumbani Tanzania. Hata hivyo, kulikuwa na mwanamke mmoja wa Kitanzania ambaye aliiambia polisi kuwa alilazimishwa kufanya biashara ya ukahaba nchini China. Mwamanke huyo alidai kuwa alipewa ofa ya kufanya kazi kama mchuuzi jijini Guangzhou lakini baadae alilazimishwa kuwa kahaba. Kipato chake chote cha ukahaba kilikuwa kinachukuliwa na mwanamke mwingine. Amedai kuwa alienda Macau kwa ajili ya kuongeza visa yke.

Mwanamke huyo aliendelea kuimambia polisi kuwa Aprili 3 mwaka huu aliwambia wengine hakutaka kuendelea kuwa kahaba na kuwa alitaka kurudi nyumbani lakini akakamatwa chumbani kwake na kupigwa. Baadae polisi walimkamata mwanamke anayedaiwa kuchukua kipato chake chote na kumkuta akiwa na aina mbili za nyaraka zinazoonyesha dalili za kufanya biashara ya ukahaba. Nyaraka ya tatu ilikutwa mikononi mwa mwanamke mwingine.

[video=youtube_share;ANkRsmQcxBA]http://youtu.be/ANkRsmQcxBA[/video]
haya ndio madhara ya high rate of unemploymnt. Kila mtu anhitaji pesa ili atatue mahitaji yake na kumtafutia kazi raia ndio suluhisho pekee la kumtatulia mtu shida ya pesa. sasa tangia enzi za Nyerere mtu unemployed alikuwa hatafutiwi kazi bali aliitwa mzulululaji na kubwagwa vijijini ili akalime. Leo hioi kila mtu na kama hakuna kazi basi serikali ijiandae kusikia mengi sana kuhusu ukahaba na madawa ya kulevya.
 
Hapana wengine ni tamaa tu, pamoja na kuvutiwa na maelezo kama niliyoyasoma hapa toka kwa akina Ngabu, Kiranga, etc. Ile hali ya kudhani yanayotokea nje ni siri yao. Mikogo mingiii Kumbe biashara ya fedheha!
 
Kizungumkuti kweli,wachina wanakuja bongo wameona fursa hapa,ajabu sisi hatuzioni,tumeziona china,kazi kwelikweli....
 
ni kweli kabisa , kuna wakina dada ambao ni wakazi wa KURASINI nawafahamu kwa majina ( lakini sitawataja ) wanafanya biashara ya ukahaba CHINA , TENA BILA WASIWASI WOWOTE ! INASEMEKANA HUKO NI BIASHARA KAMA BIASHARA ZINGINE TU ! MASHAHIDI WAKUBWA WA HILI NI WABONGO WANAOFANYA BIASHARA CHINA , WALA SIYO SIRI HATA CHEMBE ! CHA KUSIKITISHA NI KWAMBA BAADHI YAO WAPO KATIKA ARV' S !
 
ni kweli kabisa , kuna wakina dada ambao ni wakazi wa KURASINI nawafahamu kwa majina ( lakini sitawataja ) wanafanya biashara ya ukahaba CHINA , TENA BILA WASIWASI WOWOTE ! INASEMEKANA HUKO NI BIASHARA KAMA BIASHARA ZINGINE TU ! MASHAHIDI WAKUBWA WA HILI NI WABONGO WANAOFANYA BIASHARA CHINA , WALA SIYO SIRI HATA CHEMBE ! CHA KUSIKITISHA NI KWAMBA BAADHI YAO WAPO KATIKA ARV' S !

Una maana baadhi ya hao akina dada wa Kurasini wapo katika ARV?
 
Back
Top Bottom